Kanikuta nafanyiwa massage kanifanyia fujo, ni uungwana kweli?

caxton

Senior Member
May 8, 2015
145
149
Wadau nawasalimu,

Mke wangu ni mkorofi sana, naweza kusema hivyo, Jumapili nilikwenda kupata huduma za Barbershop iliyo mtaa wa pili kutoka mtaani kwangu, hii ni pamoja na kunyoa, scrub na mwisho nikaingizwa kwenye chumba cha massage

Wakati naendelea kufanyiwa huduma ya massage ghafla akatokea mke wangu na kuingia humo chumbani kwa nguvu pamoja na kuzuiliwa na vinyozi kuwa asiingie,akamkamata yule binti wa watu na kuanza kumpiga, na kuniamuru nivae nguo tuondoke, thank God tulisaidiana na vinyozi kumtoa shingoni mwa yule binti maana alikua amempiga kabali /roba.

Watu walijaa hapo nilifedheheka sana, maana picha iliyoonekana hapo ni kwamba nimefumaniwa kumbe sivyo.Wakati akiwa mjamzito alinisumbua sana kwa wivu, nikisimama na binti tu wa jirani hata kwa salam anazira kula, nikajua ni sababu labda ya mimba, lakini sasa ameshajifungua tangu mwezi March lakini tabia hii inaendelea, na hapa sijamuoa tunaishi tu sasa nikimuoa rasmi itakuweje?

Hivi wadau massage ina ubaya gani hadi nionekane kama vile nimeua mtu? Hadi leo hii sizungumzishwi ndani sasa kosa langu ni nini?
 
Wadau nawasalimu

Mke wangu ni mkorofi sana, naweza kusema hivyo, jumapili nilikwenda kupata huduma za Barbershop iliyo mtaa wa pili kutoka mtaani kwangu, hii ni pamoja na kunyoa, scrub na mwisho nikaingizwa kwenye chumba cha massage

Wakati naendelea kufanyiwa huduma ya massage ghafla akatokea mke wangu na kuingia humo chumbani kwa nguvu pamoja na kuzuiliwa na vinyozi kuwa asiingie, akamkamata yule binti wa watu na kuanza kumpiga, na kuniamuru nivae nguo tuondoke, thank God tulisaidiana na vinyozi kumtoa shingoni mwa yule binti maana alikua amempiga kabali /roba
Watu walijaa hapo nilifedheheka sana, maana picha iliyoonekana hapo ni kwamba nimefumaniwa kumbe sivyo

Wakati akiwa mjamzito alinisumbua sana kwa wivu, nikisimama na binti tu wa jirani hata kwa Salam anazira kula, nikajua ni sababu labda ya mimba, lakini sasa ameshajifungua tangu mwezi March lakini tabia hii inaendelea, na hapa sijamuoa tunaishi tu sasa nikimuoa rasmi itakuweje?

Hivi wadau massage ina ubaya gani hadi nionekane kama vile nimeua mtu? Hadi leo hii sizungumzishwi ndani sasa kosa langu ni nini?
pole sana ndugu, yeye hawezi kukufanyia hiyo mambo?
 
Kutokana na maelezo yako inaelekea hii siyo mara ya kwanza wewe kufanyiwa massage katika hiyo barber shop. Unamazoea ya kwenda hapo na kuna waliomjulisha mkeo, alikua anakulia timing tu. Inaelekea kutokana na kero za mke wako akiwa mjamzito ulijitafutia njia ya kupunguza mawazo.

1. Ni utovu wa adabu kufanya hayo uliyoyafanya mtaa wa pili kutoka kwako.
2. Kama una uwezo mchukue mkeo mwende mapumziko kama 2nd honeymoon, mkiwa mmerilax umweleze jinsi tabia yake inavyokufanya ubadilike. Kichanga kichukueni hata hivyo katika siku za kwanza maisha ya mtoto muda mwingi anakua amelala.
 
Namimi wangu alikuwa ivyoivyo ila sasa ameshika adabu, acha kumuendekeza ikiwezekana mrudishe kwao hata mwez mmoja, huyu ukioa atakuua kabisa!!!

Duc In Altum.
 
Pole sana kwa yaliyo kupata.

Kwenye maisha Kuna jambo moja la msingi. Jipambanue wewe ni mtu wa aina gani. Laiti ungekuwa umejipambanua kama wewe ni mtu makini usiependa "masihara" Basi mkeo asingefanya hayo aliyofanya.

Pamoja na hayo ni vizuri na wewe ukajitadhimini. Huenda ukawa chanzo cha hayo ama kwa historia yako ya zamani au kwa namna unavyoenenda.
 
Kutokana na maelezo yako inaelekea hii siyo mara ya kwanza wewe kufanyiwa massage katika hiyo barber shop. Unamazoea ya kwenda hapo na kuna waliomjulisha mkeo, alikua anakulia timing tu. Inaelekea kutokana na kero za mke wako akiwa mjamzito ulijitafutia njia ya kupunguza mawazo.

1. Ni utovu wa adabu kufanya hayo uliyoyafanya mtaa wa pili kutoka kwako.
2. Kama una uwezo mchukue mkeo mwende mapumziko kama 2nd honeymoon, mkiwa mmerilax umweleze jinsi tabia yake inavyokufanya ubadilike. Kichanga kichukueni hata hivyo katika siku za kwanza maisha ya mtoto muda mwingi anakua amelala.
Mama ni kweli mm ni mpenzi wa massage lakini huwa najiepusha na "happy ending" hivyo sioni tatizo kufanya massage
 
Back
Top Bottom