hurrem_sultana
Senior Member
- Sep 6, 2018
- 136
- 361
Mimi ni Mama wa watoto watatu, kabla ya kuoana na mume wangu nilikua na mwaaume mwingine ambaye tulikaa kwenye ndoa kwa miaka sita akafariki dunia, mimi nimemzidi mume wangu miaka mitatu, kabla ya kuoana tulikaa kwenye mahusiano kwa miezi sita, nilipoona nazidini nikaamua nimuambie kuwa anioe. Alikubali kweli akanichumbia na kunioa, Mama yake hakutaka kwa madi kubwa mwanae bado mdogo na kuona kama vile namlazimisha.
Kipindi hicho alikua akiishi kwake kapanga lakini alikua hana kazi maamu, kwakua mimi nimejenga naishi kwangu mume wangu alihamia kwangu tukawa tunaishi vizuri tu na tukapata watoto wawili. Nilimtafutia kazi ikashindikana nikamfungulia biashara ambayo sasa imekua kubwa na anaweza kujitegemea. Tatizo nikuwa baada ya kumpa mtaji, kumsimamia mpaka akwa na epsa zake amekua akifanya mambo yake kimya kimya, amekua hanishirikishi, amejenga bila kuniambia, kanunua gari kimya kimya bila kuniambia.
Nikimuuliza ananiambia kuwa hanitaki, anataka kuoa mwanamke wa umri wake mwanamke anayempenda, anadai kuwa kipindi namuambia anioe ni kama nilimdanganya akilia hana uwezo wa kufanya maamuzi yake. Anataka kuniacha lakini Baba yake hataki hivyo ananiambia kuwa kilichoshikilia ndoa yetu ni Baba yake tu. Nimechanganyikiwa, ana wanawake wengine na ananionyesha dhahiri hata hafichi, kibaya zaidi nasikia anataka kuoa mwanamke mwingine, nimechanganyikiwa kwani nimemtoa mbali, nishauri nifanye nini?
Kipindi hicho alikua akiishi kwake kapanga lakini alikua hana kazi maamu, kwakua mimi nimejenga naishi kwangu mume wangu alihamia kwangu tukawa tunaishi vizuri tu na tukapata watoto wawili. Nilimtafutia kazi ikashindikana nikamfungulia biashara ambayo sasa imekua kubwa na anaweza kujitegemea. Tatizo nikuwa baada ya kumpa mtaji, kumsimamia mpaka akwa na epsa zake amekua akifanya mambo yake kimya kimya, amekua hanishirikishi, amejenga bila kuniambia, kanunua gari kimya kimya bila kuniambia.
Nikimuuliza ananiambia kuwa hanitaki, anataka kuoa mwanamke wa umri wake mwanamke anayempenda, anadai kuwa kipindi namuambia anioe ni kama nilimdanganya akilia hana uwezo wa kufanya maamuzi yake. Anataka kuniacha lakini Baba yake hataki hivyo ananiambia kuwa kilichoshikilia ndoa yetu ni Baba yake tu. Nimechanganyikiwa, ana wanawake wengine na ananionyesha dhahiri hata hafichi, kibaya zaidi nasikia anataka kuoa mwanamke mwingine, nimechanganyikiwa kwani nimemtoa mbali, nishauri nifanye nini?