DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,131
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mwibara kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Alphaxard Kangi Lugola amepanda jukwaani kuzungumza na wananchi wa Mkoa wa Mara waliojitokeza kumpokea Mgombea Mwenza wa nafasi ya Makamu wa Rais Dkt. Emmanuel Nchimbi leo Agosti 30, 2025 mara baada ya kuwasili mkoani Mara.
Kama kawaida, yake Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa zamani, amewauliza mara kadhaa Wana-Mara: “Rais Samia ni jembe, si jembe?” Umati wa watu ukawa unaitikia; “Ni jembe.”
Dkt. Nchimbi ambaye anamnadi mgombea urais kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan na ilani ya uchaguzi ya chama hicho, katika msafara wake mkoani Mara ameambatana na wagombea ubunge wa majimbo mbalimbali ya mkoa huo; Dkt. Charles Mahera (Butiama), Profesa Sospeter Muhongo (Musoma Vijijini), Ester Bulaya (Bunda Mjini), Boniphace Getere (Bunda Vijijini) na Mgore Kigera (Musoma Mjini).
Soma Pia:
Kama kawaida, yake Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa zamani, amewauliza mara kadhaa Wana-Mara: “Rais Samia ni jembe, si jembe?” Umati wa watu ukawa unaitikia; “Ni jembe.”
Dkt. Nchimbi ambaye anamnadi mgombea urais kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan na ilani ya uchaguzi ya chama hicho, katika msafara wake mkoani Mara ameambatana na wagombea ubunge wa majimbo mbalimbali ya mkoa huo; Dkt. Charles Mahera (Butiama), Profesa Sospeter Muhongo (Musoma Vijijini), Ester Bulaya (Bunda Mjini), Boniphace Getere (Bunda Vijijini) na Mgore Kigera (Musoma Mjini).
Soma Pia: