Kanda ya Ziwa vs Kaskazini

Kanda ya Ziwa vs Kaskazini

Ngokongosha

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2011
Posts
3,400
Reaction score
7,610
Nimesoma comment nyingi sana zikilaumu Kanda ya Ziwa kwamba wamekuwa wasaliti na ukabila, hii naona kama ni silaha inayotumiwa na wanachama wa CHADEMA ili kuwatisha wale wenye mpango wa kumpigia kura Magufuli waonekane wakabila na wasaliti.

Lowassa anatoka Kaskazini, kipindi anahonga pesa watu walikuwa kimya wanasema huyu ndie rais, na walisahau kwamba wao kipindi cha nyuma walisema CCM hakuna msafi ila kwa Lowassa wakawa kimya, kwa sababu nia yao ni rais atoke Kaskazini, ndio maana alipoangukia pua ikawa kaonewa na sasa wanamkaribisha kwenye chama chao, ingawa hilo sijui kama litatokea.

Kwa kifupi kwa watu wa Kaskazini, Magufuli ni mchafu na Lowassa ni msafi.

Huko kunakoitwa kwa wabaguzi ndio kuna wabunge hadi wenye asili ya Kaskazini, tofauti na huko Kaskazini ambako asilimia kubwa ya wabunge ni wenyeji wa huko.

Imefikia hatua watu wanasema Lowassa akija CHADEMA anakuwa rais, Mbowe Waziri Mkuu, Slaa Waziri wa fedha, Mbatia, Mnyika.

Huu sio ubaguzi wa kikanda jamani?

Wanasema Magufuli hawezi fanya lolote kwa sababu ya system ya CCM, je, huyo Lowassa angepitishwa yeye angetumia system ipi?

Sitaki kuamini sana mambo haya kwamba ni ubaguzi ila naamini kama watu wa Kanda ya Ziwa wameamua kumuunga mkono Magufuli, labda kuna mazuri wameyaona, ingekuwa ni ukanda Jonh Momese Cheyo angekuwa rais toka zamani tu.

Mtu kukubalika eneo atokako ni kitu cha kawaida popote pale duniani, hata angepita Mwandosya watu wa Nyanda za Juu wengi wangemuunga mkono.

Angepita Ngeleja watu wasingekuwa wanasema kuhusu ukabila bali wapinzani wangeshangilia maana hana mvuto hata kule atokako pamoja na kwamba ni wa Kanda ya Ziwa.

Uchaguzi wa Uingereza mwezi May mwaka huu watu wamegombea mara moja wakashindwa wakajiuzulu, Tanzania watu wanagombea walewale miaka nenda rudi, halafu wanajiita wanademokrasia.

Ni hayo tu.
 
Wewe ni mtu mzima acha siasa za kugawa nchi zungumzia sera zipi zinafaa,kumbuka kuwa nyie ccm ndo mlianza na neno kanda ya kaskazini kwangu mimi nilijua mikoa tu ukanda nilikuwa sijui ndani ya nchi acha kugawa nchi
 
Kwa uzoefu wangu wa kuishi hizi kanda zote mbili na kuitarakti na watu wa pande hizi mbili nimegundua tofauti mojawapo kubwa ya watu wa kaskazini na watu wa kanda ya ziwa ni kwamba watu wa kanda ya ziwa si wanafiki, mtu kama hufai watakwambia wazi kuwa hufai. Lakini wa kaskazini wa kwao huwa hafai hata afanyeje
 
Wewe ni mtu mzima acha siasa za kugawa nchi zungumzia sera zipi zinafaa,kumbuka kuwa nyie ccm ndo mlianza na neno kanda ya kaskazini kwangu mimi nilijua mikoa tu ukanda nilikuwa sijui ndani ya nchi acha kugawa nchi

Hivi akina RITZ na wengine wanapotoa kauli ya rais hawezi toka kaskazini kamwe humaanisha nini??/ Sio ukabila huo??
 
..mgombea apigiwe kura kwasababu ya uwezo wake, siyo kabila, au kanda anayotoka.

..hapa siyo suala la kanda x vs kanda y.
 
CCM tayari imeshawatia ujinga watu wa kanda ya ziwa sera ya "devide and rule" imeanza kufanya kazi kwa kuwajaza ukanda poleni ila mtakuja kujitambua wakati wenzenu tuko mbali.
 
Hilo no kweli johne, hao ccm wamegundua kaskazni hakuna kitu kwao ndio maana wanakuja na mbinu hiyo na mawazo yao yanawatuma kuwa kwa vle kanda ya ziwa ni wengi basi tuwafitinshe na wa kaskzin ili washinde wao, mim nawambia ccm mmechelewa mno
 
Arusha imewahi kuwa na mbunge mmoja tu mzawa tangu enzi za Tanganyika,Mmeona mambo ya udini hayatawasaidia tena mmeanza ukanda
 
Kwa uzoefu wangu wa kuishi hizi kanda zote mbili na kuitarakti na watu wa pande hizi mbili nimegundua tofauti mojawapo kubwa ya watu wa kaskazini na watu wa kanda ya ziwa ni kwamba watu wa kanda ya ziwa si wanafiki, mtu kama hufai watakwambia wazi kuwa hufai. Lakini wa kaskazini wa kwao huwa hafai hata
afanyeje

...N g 'w a n o k o !!!


1l-image.jpg
 
Mkuu hawa ndugu zetu wa kaskazini wanashida sana. huoni juzi mramba kafungwa wamekuja kumtetea humu japo jamaa kalitia taifa hasara ya bil 11.7?
 
Waulizwe baraza la UVCCM Mkoa wWa Pwani ndiyo waasisi wa hoja ya ukanda kwenye mbio za urais ndani ya CCM na hawajawi kukemewa. Tulishasema hoja kama hizi za kijinga sio za kupuuzwa. Hii ingeepukwa mapema kwa wale vijana kukemewa.

Tayari watu wanaamini kuwa kamati ya maadili ya CCM iliendekeza hoja ya ukanda ndani ya vikao vyake kwa kuteu wagombea watatu wenye asili ya ukanda wa Pwani. Tujitahidi tusinaswe kwenye mtego huu wa ubaguzi utatugawa kama taifa. Hoja hizi zimejaa ukakasi, hazizungumziki kimya kimya na mbele za halaiki zinatia kinyaa. Tujitahidi kuziepuka hazitujengi bali kutubomoa Kama taifa.

Wasisi wa hoja hii kwa kujua au kutokujua wabanwe mbavu ili wawatake Watanzania radhi kwa ulimi wao kuteleza. Hii itasaidia kuifuta hoja ile!
 
I support CHADEMA and the opposition in general, lakini kama Wapinzani mtaendelea kufanya siasa zenu ktk mtindo huu wa kutegemea hisani kutoka CCM, basi itawachukua miaka 100 kuingia ikulu. Let's be honest here, ili chama chochote kiweze kushinda uchaguzi kinapaswa kuwa flexible, kibadilike kuendana na hali halisi ya kisiasa ilivyo.

Kuna mahali CHADEMA wamejifunga pingu, sasa wanategemea hatima kufikia malengo yao, hakuna mikakati wala plan B. CHADEMA walishaamua Dr Slaa awe mgombea wao iwe isiwe, sababu wanayotoa ni kwamba alifanya vizuri ktk uchaguzi wa mwaka 2010. Sote tunajua kwamba Dr Slaa alifanya vizuri mwaka 2010, but things are changing over a course of time, na tunafahamu fika kwamba hali halisi ya kisiasa imebadilika sana mwaka huu tangu CCM wamchague Dr Magufuli.

Tunajua fika kwamba kete kubwa (talking point) ya Dr Slaa ingekuwa ni ufisadi, sasa anapokwenda hoja ya namna hii kwa wananchi dhidi ya mtu kama Dr Magufuli atapuuzwa kiaina, kwasababu wananchi nao wanaamini Dr Magufuli ndio suluhisho la ufisadi nchini.

Sasa basi, CHADEMA na UKAWA walipaswa kuja na plan B, nayo ni Tundu Lissu, mwenye hoja ya katiba mpya, Tundu Lissu akiingia ktk uchaguzi na hoja ya rasimu ya Warioba, wananchi wanaweza kubadilisha mawazo yao na kuwafanya waanze kufikiria tena kuhusu chaguo lao la urais.

Right now wananchi washasahau kabisa kuhusu suala la katiba mpya, wao wanachoamini ni kwamba Dr Magufuli atainyoosha nchi kutokana na misimamo yake. Ni vyema UKAWA wakaingia ktk uchaguzi na Tundu Lissu huku akiibeba ajenda yake ya katiba mpya aliyoipigania akiwa bungeni, katiba mpya bado ni kete muhimu ya kisiasa ya Upinzani, na CCM waliamua kuachana na mchakato wa kura za maoni kwasababu waliogopa wangeshindwa kwa aibu wakati wa kura za maoni.

Kila kitu kina zama zake, Dr Slaa na slogan yake ya ufisadi (2010) na ilikuwa na nguvu sana. Naye Tundu Lissu na katiba mpya, hii ina nguvu sana japo UKAWA hamuonekani kutambua.
 
Ukabila, ukanda, udini vyote havifai.

Mi sitoki kanda ya kaskazini na sijawahi fika mkoa wowote wa kanda ya kaskazini lakini nilijiunga JF hasa hasa kumuunga mkono Dr Magufuli. Unaweza angalia post zangu zote za nyuma

Kabla ya hapo nilikuwa msomaji tu wa post za watu humu JF, nilikuwa sichangii

Kiufupi tusifuate mkumbo, magufuli anafaa na Lowassa hakustahili kupitishwa na CCM

Tuache ubinafsi
 
Wewe ni mtu mzima acha siasa za kugawa nchi zungumzia sera zipi zinafaa,kumbuka kuwa nyie ccm ndo mlianza na neno kanda ya kaskazini kwangu mimi nilijua mikoa tu ukanda nilikuwa sijui ndani ya nchi acha kugawa nchi
Waambie labda watasikia
 
Back
Top Bottom