johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,944
- 141,920
Kamanda mstaafu wa polisi kanda maalumu ya Dsm mzee Suleiman Kova ameelezea mafanikio aliyoyapata alipokuwa katika utumishi.
Kamanda Kova amesema yeye alikuwa akipelekwa maeneo yaliyoshindikana kwa uhalifu na alipofika alifanikiwa kuleta amani na Upendo.
Ametolea mfano mkoa wa Kigoma ambao ulikithiri kwa ujambazi wa kutumia silaha lakini alipofika alifanikiwa kukamata silaha zote, pili Mbeya kulikokithiri imani za kishirikina za uchunaji ngozi na upigaji nondo vichwani lakini alipowasili alilimaliza tatizo hilo.
Akijibu swali la mtangazaji Hasan Ngoma aliyetaka kujua endapo Rais Magufuli angemteua kuwa IGP angefanya mambo gani mahususi ya kuacha alama, Kova amesema angehakikisha askari polisi na raia wanakuwa kitu kimoja as a team wakiishi kwa kusaidiana na kupendana.
Chanzo: Clouds 360
Maendeleo hayana vyama!
Kamanda Kova amesema yeye alikuwa akipelekwa maeneo yaliyoshindikana kwa uhalifu na alipofika alifanikiwa kuleta amani na Upendo.
Ametolea mfano mkoa wa Kigoma ambao ulikithiri kwa ujambazi wa kutumia silaha lakini alipofika alifanikiwa kukamata silaha zote, pili Mbeya kulikokithiri imani za kishirikina za uchunaji ngozi na upigaji nondo vichwani lakini alipowasili alilimaliza tatizo hilo.
Akijibu swali la mtangazaji Hasan Ngoma aliyetaka kujua endapo Rais Magufuli angemteua kuwa IGP angefanya mambo gani mahususi ya kuacha alama, Kova amesema angehakikisha askari polisi na raia wanakuwa kitu kimoja as a team wakiishi kwa kusaidiana na kupendana.
Chanzo: Clouds 360
Maendeleo hayana vyama!