Kamala Harris ndiye mgombea mwenza wa Joe Biden

Alisumbuliwa sana na "The Privileged White America" hasa wale wa upande wa pili pamoja na vyombo vyao vya habari: Binafsi naamini kuna mambo mengi mazuri angeyafanya yule mzee lakini hakufanikiwa kwasababu ya hujuma za kisiasa. Alipokea nchi ambayo tayari ilikuwa iko kwenye vita na anaingia madarakani mwaka 2008 akakaribishwa na anguko la kiuchumi: Mwisho wa siku yeye ndiye aliyelaumiwa kwa matatizo ya Marekani ambayo yalikuwepo kwa muda mrefu.
80% ya media za marekani ni liberal wing medias na zote zilikuwa upande wake(democrats),Kwa sasa hiyo 80% ndio kila kukicha ina mu attack Trump,white privilege iko wapi hapo?.Obama alikuta nchi iko vitani ndio still aliendelea na hizo vita na 2011 alitoa order ya kuivamia Liblya kwa mwavuli wa NATO,unataka na hicho asilaumiwe?.Website ya Ikulu inatumika kutangaza mambo ya LGBTQ,unafikiri wamarekani wote wanakubaliana na mambo ya LGBTQ??,Kwa nini wasimlaumu?,Kipindi cha Obama ndio kipindi Iran ilijitanua,Russia ilijitanua,China ilipata nguvu kubwa ya kiuchumi kutokana na mkataba wa TPP ambao Obama aliingia na China,Unataka na hiyo wasiseme?.Obama alifanya mambo mazuri mengi sana tu,ila kama ilivyo binadamu yeyote alifanya makosa yake na ilibidi alaumiwe,sio kwa sababu ya rangi yake hapana ila kwa sababu ya makosa yale..Pale US kuna ujinga kwamba eti mtu wa rangi nyiingine akifanya makosa akilaumiwa wanasema ni Racism,sio sawa.Wngekuwa US ni wabaguzi kiasi hicho hakuna mweusi angekanyaga Ikulu wala bungeni pale USA,angekatwa na mapema na hiyo unayoiita white privileged system.Racism ipo ila iko exaggerated sana kuliko kawaida..
 
Bob mbona unapanic kizembe sana :D :D ,,seems uko weak sana on emotional control.Umeuliza maswali ambayo ni reseach base questions,anaweza tumia hata week kukuletea majibu,mfano kama alisoma comments mitandaoni,unataka aende kuhesabu comments zoote na hao watu wametokea maeneo gani USA??..BTW huyu niliyemjibu hapo hata simjui na wala sinaga muda mchafu wa kujipendekeza kwa watu mitandaoni,.
Mzee baba una akili sana.
Mfano hapo comments mbili za mwanzo wamemponda huyo maza, na zina likes 10k na zaidi. Hiyo inatosha kabisa kwamba huyu Mzee mama hajapokelewa fresh.
IMG_20200812_121211_326.JPG
 
80% ya media za marekani ni liberal wing medias na zote zilikuwa upande wake(democrats),Kwa sasa hiyo 80% ndio kila kukicha ina mu attack Trump,white privilege iko wapi hapo?.
Umeonge mambo mengi sana kwenye hoja yako lakini mimi ninaomba kuuliza maswali machache ambayo yanatokana na mambo niliyoyaona kwenye hoja zako hapo. Ili kurahisisha mambo naomba nianze na yale ya Sera ya Mambo ya nje (Foreign Policy):

Mosi, Mkataba wa TPP (Trans-Pacific Partnership Agreement) haukusainiwa na Uchina bali uliandaliwa dhidi ya Uchina. Washirika vinara ni Marekani na Japani, na lengo lao kubwa lilikuwa kutimiza mkakati dhidi ya Uchina uitwao The Pivot to Asia (The Asian Strategy of 2012). Aliyeanzisha mkakati wa kupambana na Uchina alikuwa ni Barack Obama na siyo Donald Trump kama ambayo anasema hapa. Hivyo nadhani hapa tuweke rekodi sana kwamba Uchina hahusiani kabisa na TPP kama unavyosema hapa.

Pili, Uchina ni lazima angekuwa na nguvu tu na hili halikusababishwa na serikali ya Barack Obama kama ambavyo wewe unasema hapa. Hata Donald Trump angekuwepo kwenye mtikisiko wa Uchumi wa mwaka 2008 ni lazima angeenda kukopa fedha nje ya nchi hasahasa Uchina ili kuendesha nchi. Ndiyo maana wakati Hillary Clinton ni Secretary Of State alivyoulizwa kwanini hampambani na Uchina akajibu hivi "How do you fight against your Banker" Ikumbukwe hapa ndipo tatizo lilianza. Mwaka moja baadae Uchina ndiyo ikawa The Leading Exporter of Merchandise. Sasa unadhani Trump ndiyo angekuwepo mwaka 2008 angefanya tofauti na haya ya kukopa Uchina ???

Tatu, Obama alikosea sana kwenye Sera ya Mashariki ya Kati: Akakiri kabisa makosa kwamba "Libya was a disaster" Donald Trump akasema kwamba angerekebisha matatizo kule Syria, Libya na Iraq na kuvitoa kabisa vikosi vya Marekani lakini unadhani mpaka kufika mwaka 2019 mwishoni alikuwa amefanikiwa kwa kiwango gani ukimlinganisha na Barack Obama ???

Nne, kuhusu Iran nadhani umeyaangalia mambo kwa juu-juu sana. Hivi kuna kipindi ambacho serikali ya Iran imefanya fujo bila kuguswa na Marekani kama kipindi hiki cha Donald Trump ??? Kulipua manowari za mafuta, kulipua ndege za jeshi (Drone) za Marekani, kuvamia Saudi Arabia na kulipua vinu vya mafuta na kulipua kambi ya jeshi la Marekani kule Iraq. Labda nikuulize mkuu, wewe unaamini kabisa kwamba Donald Trump amewaminya Iran kipindi hiki ???

Tano (Nitakuachia maswali tu): Ukilinganisha Barack Obama na Donald Trump unahisi ni nani ambaye amekuwa na Sera nzuri sana ya mambo ya nje hasa kwenye suala zima la Ulinzi wa Maslahi ya Marekani Barani Ulaya ??? Unavyojibu hili swali kaa kabisa ukikumbuka kwamba bila Ulaya Marekani haitaweza kuwa taifa lenye nguvu duniani.

Turudi sasa ndani ya Marekani. Hapa nitaongea kidogo na kukuachia maswali machache ambayo nadhani pia wadau wenye ufahamu na Marekani watatusaidia kuyajibu:

Mosi, katika kuangalia utawala wa Raisi Trump nilitegemea ungeanza kuzungumzia jinsi ambavyo ameshughulika na suala zima la ugonjwa wa Corona (Covid-19). Unadhani yeye kama Raisi alitakiwa afanye mambo ambayo aliyafanya kipindi hiki ??? Ugonjwa huu umeidhihirishia dunia kile ambacho Barack Obama alikisema kwa muda mrefu kwamba "The American Health System is broken and needs to be fixed"

Pili, kuhusu ubaguzi wa Rangi nchini Marekani. Nimekuwa napatwa na ukakasi na Diaspora wengi wa Afrika ambao wanakaa Marekani hasa pale wanapojaribu kusema kwamba nchini Marekani ubaguzi unakuzwa. Kuna dada yangu mkubwa ni daktari anafanya kazi huko Marekani, zamani alihisi kwamba ubaguzi unakuzwa kwasababu hakupitia yale ambayo weusi wazawa wa Marekani wamekuwa wakiyapitia. Yeye kasoma kamaliza chuo kabakizwa na kupewa GREEN-CARD hapohapo huku akiwa na mshahara mnono.

Nadhani tutakuwa tunakosea sana kama tukitaka kuwasemea watu weusi ambao babu zao walikuwa watumwa vizazi na vizazi kwamba wanaukuza ubaguzi wa rangi huku wewe mwenzangu ni mtanzania ambaye umezaliwa kwenye nchi yenye watu weusi kama wewe. Labda nikuulize ni kwanini labda unahisi kwamba watu weusi wanaukuza ubaguzi ???

NB: Hili la LGBTQ limeeleweka na wala sitalizungumzia kabisa kwasababu siyo kwangu naona siyo la kuligeuza ajenda ya huu mjadala. Lakini kaa ukifahamu kwamba matatizo ya Marekani ni makubwa mno na yana mizizi mirefu (Yako kimfumo zaidi kuliko kisera), hivyo hayawezi kutatuliwa na sera za uchaguzi za kipindi kimoja za Donald Trump wala Joe Biden.

Juzi nilikuwa namsikiliza Professor John Mearsheimer ambapo alisema maneno haya "The Neo-Liberal Global Order of 1945 has failed miserably" hili ni tatizo ambalo halipo Marekani tu, bali kwenye nchi zote za Magharibi.

Dunia inabadilika sana na mzani wa nguvu unahama Magharibi hivyo ili Marekani na wengine waweze kukaa vizuri ni lazima wakubaliane na uhalisia kwamba "The Era of Pax-Americana is coming to an end" na hili halimaanishi kwamba "This is the end of America as we know her" kama ambavyo wengi wetu tunahisi. America is so many great things which China is not, lakini ni lazi a tukubali dunia imebadilika sana.
 
Hata Bush Sr aliingia kimajaribio na akavurunda kama alivyovurunda Trump ila yeye hakuvurunda kwa kiwango cha Trump kwa kuwa alikuwa na background ya kuwa boss wa CIA ila naye alikaa term moja. Siyo siri Trump ni Rais wa hovyo kuliko wote kuwahi kutokea kwenye historia ya Marekani.
...kwanini unamwita Trump Rais wa hovyo?
 
Ila Trump apunguze lawama yaani yy kila kitu analaumu tu.

Angekuwa jf basi jukwaa la mmu na siasa lingemkoma maana huko ndio wanaume daily kulaumu tu.
 
Alisumbuliwa sana na "The Privileged White America" hasa wale wa upande wa pili pamoja na vyombo vyao vya habari: Binafsi naamini kuna mambo mengi mazuri angeyafanya yule mzee lakini hakufanikiwa kwasababu ya hujuma za kisiasa. Alipokea nchi ambayo tayari ilikuwa iko kwenye vita na anaingia madarakani mwaka 2008 akakaribishwa na anguko la kiuchumi: Mwisho wa siku yeye ndiye aliyelaumiwa kwa matatizo ya Marekani ambayo yalikuwepo kwa muda mrefu.
Matatizo mengine aliyaanzisha yeye mwenyewe hivyo anastahili lawama. Mfano Sera zake huko Syria, Libya na Misri wakati wa Arab spring.
 
......kama unazo hizo taarifa mjibu tu..
Kwa mfano naanza wawili wapo CA, wanne wapo Florida, 7 wapo Texas etc?
Mbali ya niliowasikia mimi ambao hawezi kuthibitisha kama ni kweli niliwasikia hata nikitaja idadi na kila mmoja anaishi wapi, lakini ukisoma maoni kwenye mitandao ni rahisi sana kupata jibu. Mfano mzuri kuna member ameweka screenshot huko juu Proved.
 
Simple Biology by Gregory Mendel: Black is Dominant, White is Recessive!
Mbona Obama alikuwa ana uzungu lakini bado tulimuita mweusi ???
Obama walikuwa wakielezea uzungu wake na jinsi alivyolelewa Hawaii, huyu Kamala wanaficha kabisha uhindi wake, hujiulizi ni kwa nini?
Hao black uliowasikia wewe,umewasikilia wapi? na idadi yao ni ipi? na wanatoka maeneo yapi ndani ya US?
Kumekuwa na msukumo mkubwa Marekani wa weusi kujitambua, hivyo wamekuwa hawaangalii sura za viongozi bali wanaanagalia ni mtu wa aina gani.

Hii ilikuja baada ya Obama, ambapo walimpigia kampeni lakini baada ya kuwa rais hakufanya chochote kwa weusi. Serikali yake iliwafanyia wema makundi yote (latino, LGBT, wayahudi, weupe n.k) lakini haikufanya chochote kwa weusi, tena kwenye utawala wake ndiyo kulikuwa na mauaji mengi ya weusi kutoka kwa polisi. Hii imesababisha vikundi vingi vya uamsho vya weusi kusambaza ujumbe kuwataka wote wanaoomba kura kueleza watawafanyia nini endapo watashinda uchaguzi.
ila wamewaacha wakaenda kumchagua Kamala Haris huku wakijua ana history tata kidogo na black kipindi akiwa Judge.
Kamala hajawahi kuwa jaji bali aliwahi kuwa mwendesha mashitaka.
Jioe Biden ana historia tata kwa wanawake kama alivyo Trump,Pia kipindi akiwa mmbunge miaka ya 80s ana historia ya matamshi ya kibaguzi kwa blacks,Kikubwa kitachowatofautisha Biden naTrump kwa sasa ni sera mathubuti,ambacho hadi sasa Joe hajaonyesha serambadala kuzidi za Trump.Ila bado DNC wanakomaa nae tu,Naamini kule DNC kuna mamluki anawashauri vibaya kuhakikisha Trump ana pata upinzani dhaifu.
Toka mwezi wa 5 joe biden alikuwa akiongoza kwenye poll kwa mbali sana kitaifa na kwenye majimbo,ila mwezi huu wa nane hali imeanza kubadilika Trump anaonekana ku level ground kwenye baadhi ya majimbo na taifa..kuna kitu kule DNC hakiko sawa
DNC hawataki black agenda hata moja ndiyo maana waliowachagua wote wanamitazamo mibaya na historia chafu dhidi ya weusi.
 
Yametimia, Joe Biden keshachagua mgombea mwenza. Nilikuwa nasoma sehemu kwamba Democrats walishauri achague mgombea mwenza mwanamke tena mweusi: Binafsi nilihisi labda wanatania au wameenda mbali sana lakini yametimia. Hapa inamaanisha kwamba huyu babu Joe Biden mwenye miaka zaidi ya 77 akiwa Rais na akifia madarakani basi taifa la Marekani litakuwa na Raisi mwanamke wa kwanza, tena mweusi.

Sasa kama huyu babu Biden ameshauriwa vizuri au vibaya, binafsi sifahamu. Lakini ambacho nina uhakika nacho asilimia 100% ni kwamba watu wakifikiria kwamba endapo huyu babu atashinda na bahati mbaya akafia madarakani basi Kamala Harris ndiyo atakuwa Rais wao, nadhani italeta sana shida.

Japo kimkakati inaweza kuwasaidia kupata kura za weusi na zile za wanawake, lakini nikiangalia kile ambacho alifanywa Hillary Clinton kwasababu ya jinsia yake na kile ambacho alifanywa Raisi Obama kwasababu ya rangi yake nachelea kusema kwamba huyu mama atakuwa na kipindi kigumu sana. Mfumo siyo rafiki kwa mwanamke mweusi, hivyo kama ni chuma cha pua anatakiwa awe chuma cha pua haswaa.


----
Sina cha kuchangia mkuu, maana umeni pre empty hapo kwenye paragraph ya mwisho.
 
Simple Biology by Gregory Mendel: Black is Dominant, White is Recessive!
Mbona Obama alikuwa ana uzungu lakini bado tulimuita mweusi ???
Sidhani kama ni sababu ya dominant bali ni sababu ya weakness hivyo akifanikiwa kuchanganya kidogo tu kwake inakuwa ni zaidi ya ushindi.
 
Obama walikuwa wakielezea uzungu wake na jinsi alivyolelewa Hawaii, huyu Kamala wanaficha kabisha uhindi wake, hujiulizi ni kwa nini?
Yote tisa, weusi wake ndiyo silaha inayotumika kwenye hizi kampeni.
Kama kumuangusha kisiasa kitakachomuangusha ni huo weusi wake.
Kama kumuinua kisiasa kitakachomuinua ni huo huo weusi wake.
Hoja za msingi hana, ndiyo maana alishindwa mapema kabisa.
 
Yote tisa, weusi wake ndiyo silaha inayotumika kwenye hizi kampeni.
Kama kumuangusha kisiasa kitakachomuangusha ni huo weusi wake.
Kama kumuinua kisiasa kitakachomuinua ni huo huo weusi wake.
Hoja za msingi hana, ndiyo maana alishindwa mapema kabisa.
Kwenye ishu ya Obama wapanga mikakati walicheza miguu yote, weupe walipozwa kwa kuambiawa "huyu tulimlea sisi, hivyo msiwe na tabu". Weusi walipozwa kwa kuambiwa "huyu anafanana na nyinyi hivyo mtaweka historia" ila agenda za wapanga mikakati zikabaki pale pale, kuilinda na kuitetea"petro dollar" .
 
Unaweza kutaja hata kitu kimoja alichoharibu Trump?

Trump kwa takwimu ndie rais bora kuwahi kutokea Marekani. Mwezi Jue alitengeneza ajira milioni 4.8, haijawahi kutokea toka Dunia imeumbwa.

Achana na hadithi za vijiweni.
Wapingaji wake wamekariri tu
 
Back
Top Bottom