Kama wote waliosaini mikataba ya uozo TANESCO bado wanadunda, Magufuli hajapambana na ufisadi

Nazareti

JF-Expert Member
Apr 1, 2016
413
443
Ni vichekesho na vituko ndiyo vimejaa hapo TANESCO, hili ndiyo shimo la kuzimu lisiloweza kujazwa na vijisenti vyote vya Watanzania. Watu wanaofahamika walibeba magunia ya mabillion ya shilingi na bado leo wanatanua mitaani tu huku tukiambiwa kuwa mahakama ya mafisadi eti imekosa kesi za kushughulikia? maanake ni kwamba Tanzania hakuna mafisadi.

Jana Rais wa Jamhuri ya Muungano ya watu wa Tanzania akiwa Bukoba alitengua uteuzi wa Mkurugenzi wa TANESCO bwana Mramba kwa kutaka kuongeza bei ya umeme kwa 8%.

Inawezekana kabisa ongezeko hili linachagizwa na ukweli kwamba hapo TANESCO kuna mikataba isiyo na faida kwanza kwa shirika lenyewe na kwa taifa kwa ujumla.

Na hili ndilo tatizo kubwa linalolikumba hili shirika kushindwa kujiendesha na kuwapatia watanzania umeme wa bei ya chini maana limezungukwa na ufisadi usioelezeka. Mramba anajua vizuri ni kwanini kuna mikataba ya aina hiyo. Muhongo hawezi kukwepa juu ya uwepo wa hiyo mikataba, na hawa ndiyo watu tunaowategemea watusaidie kupatikana kwa umeme nafuu?

Hebu fikiria ni kwanini watu walichota escrow bado wapo tena wanajulikana vizuri tu huku tukisema tunapambana na ufisadi?

Kweli tunahitaji kumuombea tu Rais ili moyo wake na niya ya kupambana na ufisadi ishike kasi zaidi. Bila mkono wa Mungu kumtia nguvu Rais, IPTL, Symbion, na mengine mengi ni ngumu mno kuufikia umeme wa bei nafuu kwa Watanzania. Bado faru John hajulikani aliko, bado mzungu anamiliki sehemu katikati ya mbuga zetu za wanyama, bado mwarabu wa loliondo,

Mungu mbariki na umtie nguvu Rais ili afanikiwe kuishinda hii dhuruma tuliyoifanya sisi na viongozi waliopita juu ya taifa letu sisi wenyewe.
 
Mahakama ya Mafisadi imekosa wateja mpaka sasa halafu bado unafikiri kulikuwa au kuna ufisadi Tanzania!!

Kabla ya uchaguzi inaelekea Rais aliamini kuwa Kuna Mafisadi ... sasa kagundua kuwa hao wote walikuwa ni wapi game deal tu. Ndiyo maana hazungumzii tena ufisadi bali wapi game deal!!

Ndiyo Tanzania ya CCM hiyo.... spinning na propaganda ni sehemu ya maisha!!
 
Magufuli hawezi na kamwe hatomaliza ufisadi kama ataendelea kutumbua majipu na kuacha viini vyake.

Jipu la Tanesco siyo Felchismi bali mikataba mibovu ya IPTL na Symbion inayotafuna mabilioni kwa siku hata bila kuzalisha unit moja.
 
Magufuli hawezi na kamwe hatomaliza ufisadi kama ataendelea kutumbua majipu na kuacha viini vyake.

Jipu la Tanesco siyo Felchismi bali mikataba mibovu ya IPTL na Symbion inayotafuna mabilioni kwa siku hata bila kuzalisha unit moja.
 
Ni vichekesho na vituko ndiyo vimejaa hapo TANESCO, hili ndiyo shimo la kuzimu lisiloweza kujazwa na vijisenti vyote vya Watanzania. Watu wanaofahamika walibeba magunia ya mabillion ya shilingi na bado leo wanatanua mitaani tu huku tukiambiwa kuwa mahakama ya mafisadi eti imekosa kesi za kushughulikia? maanake ni kwamba Tanzania hakuna mafisadi.

Jana Rais wa Jamhuri ya Muungano ya watu wa Tanzania akiwa Bukoba alitengua uteuzi wa Mkurugenzi wa TANESCO bwana Mramba kwa kutaka kuongeza bei ya umeme kwa 8%.

Inawezekana kabisa ongezeko hili linachagizwa na ukweli kwamba hapo TANESCO kuna mikataba isiyo na faida kwanza kwa shirika lenyewe na kwa taifa kwa ujumla.

Na hili ndilo tatizo kubwa linalolikumba hili shirika kushindwa kujiendesha na kuwapatia watanzania umeme wa bei ya chini maana limezungukwa na ufisadi usioelezeka. Mramba anajua vizuri ni kwanini kuna mikataba ya aina hiyo. Muhongo hawezi kukwepa juu ya uwepo wa hiyo mikataba, na hawa ndiyo watu tunaowategemea watusaidie kupatikana kwa umeme nafuu?

Hebu fikiria ni kwanini watu walichota escrow bado wapo tena wanajulikana vizuri tu huku tukisema tunapambana na ufisadi?

Kweli tunahitaji kumuombea tu Rais ili moyo wake na niya ya kupambana na ufisadi ishike kasi zaidi. Bila mkono wa Mungu kumtia nguvu Rais, IPTL, Symbion, na mengine mengi ni ngumu mno kuufikia umeme wa bei nafuu kwa Watanzania. Bado faru John hajulikani aliko, bado mzungu anamiliki sehemu katikati ya mbuga zetu za wanyama, bado mwarabu wa loliondo,

Mungu mbariki na umtie nguvu Rais ili afanikiwe kuishinda hii dhuruma tuliyoifanya sisi na viongozi waliopita juu ya taifa letu sisi wenyewe.
Huyo prof.muhongo hutamwezi tafuta wengine
 

Attachments

  • 1483340471744.jpg
    1483340471744.jpg
    52.9 KB · Views: 25
Kweli JPM ameonyesha njia na niya ya kupambana na ufisadi nadhani kuliko awazu zote zilizopita labda Mwalimu Nyerere sasa wengine tulikuwa bado ndiyo tunajifunza kutembea tu, mliokuwa macho hizo enzi tusaidieni kulinganisha. Nashangaa watu kama kina Ngeleja, Werema, chenge na wale wa EWURA bado waanamkia majumbani mwao huku zigo kubwa walishaibebesha hii nchi, hawa wakishughulikiwa ipasavyo wataisaidia kupatikana kwa ufumbuzi bila kufanya hivyo bado tu pengine bei ya umeme itapanda vinginevyo serikali iendelee kutumia kodi kuilisha Tanesco maana imebeba zigo juu ya mamizigo mengine. Mungu amtie nguvu Rais wetu katika hili maana si kazi nyepesi kivile kama wengi tunavyofikiri na kulaumu tu.

Bado nas
 
Penye uzuri tuuseme. Jamaa anapambana sana na ufisadi ukilinganisha na aliyepita. Sema ufisadi mwingine ka escrow unagusa uhai wa chama.

Mkuu ufisadi anaotakiwa kupambana nao ni huo unaogusa uhai wa chama. Huu mwingine anaopambana nao hata Makonda anaumudu. Kimsingi anajitahidi lakini bado ana safari ndefu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom