Song of Solomon
JF-Expert Member
- Aug 5, 2021
- 2,751
- 5,623
HAYA MAISHA!
Siku ya kwanza nilipo ingia mochwari (mortuary), nilichokiona Ni ngumu mno kueleza. Kwanza niliona maneno yameandikwa (TULIKUWA KAMA WEWE) na kuelekea mlango wa kutokea niliona maneno yameandikwa (HIVI KARIBUNI UTAUNGANA NASI).
Mh..! Kwa hakika niliogopa Sana kuona miili ya watu ikiwa imelazwa katika sakafu pasipo kufunikwa kitu. Kulikuwa na maiti zaidi ya hamsini mingine imelazwa katika vitoroli (Jerry cans), mingine katika meza za kuoshea maiti, mingine ndani ya majokofu. Kulikuwa na miili ya watu wa jinsia zote.
Tukasonga ndani zaidi kuelekea mahali ulipo hifadhiwa mwili wa ndugu yangu. Tulipoufikia mhudumu wa mortuary alifunua na ulikuwa haujavishwa nguo na umelazwa juu ya ubao.
Nilimuangalia Sana marehemu ndugu yangu akiwa amelala pale utupu, hakuweza hata kufunika utupu wake kwa mikono yake, Wala kupinga chochote kile. Nikajiuliza Sana NINI MAANA YA MAISHA.?
Kwanini tunatumia nguvu nyingi kutaka kumiliki kila kitu katika dunia hii na wakati mwingine hata kwa kuwaumiza wengine?
Kwanini tunakiburi, majivuno na ubinafsi Kama tunaimiliki dunia na pumzi ya uhai wetu?
Kwanini hatuwezi hata kuwasamehe watu wanaotukosea huku tukijihesabia haki kana kwamba Ni malaika?
Kwanini hatuwezi hata kumkumbuka Muumba wa Mbingu na nchi tunapokuwa hai?
Niliona matajiri waliokuwa na majumba, waliokuwa na degree na PhD, waliokuwa na magari ya kifahari, waliokuwa viongozi majasiri na mashupavu, matajiri na masikini, wanawake wazuri wenye mitindo mbalimbali ya nywele wote wakiwa wamelazwa humo ndani kimyaa kabisa.
Nikajisemea moyoni kumbe maisha sio kitu na niyamuda tu, cheo Ni Cha muda, utajiri na heshima vyote Ni vya muda tu. Sijui lini nitaondoka katika dunia hii lakini niliona vile nitakavyokuwa siku pumzi yangu itakapoondolewa.
Ninatamani na kutaka kuwa Bora zaidi ya Jana yangu katika unyenyekevu,kusamehe,kupenda na kujali wengine, kumuabudu Mungu na kumtumikia. Kwa kuwa maisha niliyonayo Ni ya muda na tena kifo hakitazami status ya mtu.
GOD ABOVE ALL
Siku ya kwanza nilipo ingia mochwari (mortuary), nilichokiona Ni ngumu mno kueleza. Kwanza niliona maneno yameandikwa (TULIKUWA KAMA WEWE) na kuelekea mlango wa kutokea niliona maneno yameandikwa (HIVI KARIBUNI UTAUNGANA NASI).
Mh..! Kwa hakika niliogopa Sana kuona miili ya watu ikiwa imelazwa katika sakafu pasipo kufunikwa kitu. Kulikuwa na maiti zaidi ya hamsini mingine imelazwa katika vitoroli (Jerry cans), mingine katika meza za kuoshea maiti, mingine ndani ya majokofu. Kulikuwa na miili ya watu wa jinsia zote.
Tukasonga ndani zaidi kuelekea mahali ulipo hifadhiwa mwili wa ndugu yangu. Tulipoufikia mhudumu wa mortuary alifunua na ulikuwa haujavishwa nguo na umelazwa juu ya ubao.
Nilimuangalia Sana marehemu ndugu yangu akiwa amelala pale utupu, hakuweza hata kufunika utupu wake kwa mikono yake, Wala kupinga chochote kile. Nikajiuliza Sana NINI MAANA YA MAISHA.?
Kwanini tunatumia nguvu nyingi kutaka kumiliki kila kitu katika dunia hii na wakati mwingine hata kwa kuwaumiza wengine?
Kwanini tunakiburi, majivuno na ubinafsi Kama tunaimiliki dunia na pumzi ya uhai wetu?
Kwanini hatuwezi hata kuwasamehe watu wanaotukosea huku tukijihesabia haki kana kwamba Ni malaika?
Kwanini hatuwezi hata kumkumbuka Muumba wa Mbingu na nchi tunapokuwa hai? Niliona matajiri waliokuwa na majumba, waliokuwa na degree na PhD, waliokuwa na magari ya kifahari, waliokuwa viongozi majasiri na mashupavu, matajiri na masikini, wanawake wazuri wenye mitindo mbalimbali ya nywele wote wakiwa wamelazwa humo ndani kimyaa kabisa.
Nikajisemea moyoni kumbe maisha sio kitu na niyamuda tu, cheo Ni Cha muda, utajiri na heshima vyote Ni vya muda tu. Sijui lini nitaondoka katika dunia hii lakini niliona vile nitakavyokuwa siku pumzi yangu itakapoondolewa.
Ninatamani na kutaka kuwa Bora zaidi ya Jana yangu katika unyenyekevu,kusamehe,kupenda na kujali wengine, kumuabudu Mungu na kumtumikia. Kwa kuwa maisha niliyonayo Ni ya muda na tena kifo hakitazami status ya mtu. GOD ABOVE ALL
