Kama Tanzania ingeshindwa vita ya Kagera: Je, Rwanda na Uganda zingefika hapa zilipofika leo?

Labda nikumbushe tu Kagame amewahi Iteka Congo nzima wakati wa 1st congo war ya kumng'oa mobutu kutokea ziwa kivu mpaka port matadi!!

Sio hivyo tu alipotaka kumng'oa Kabila aliiteka tena congo na alifika mpaka kinshasa kabisa na kama sio msaada wa Angola basi angekua ameiteka Congo nzima ndani ya wiki 2 pekee.

Kwenye vita za kileo ukubwa wa nchi hauna maana yeyote sababu vita inapiganwa kwa teknolojia nyingi mfano matumizi ya ndege na makombora ya masafa marefu kwahiyo unaweza zingirwa kwenye anga na kumalizwa ndani ya wiki tu kabla hata majeshi ya ardhini hayajafika Dodoma.
Ni kweli mkuu ! Angola na Zimbabwe waliisaidia sana hii DRC kipindi kile.

Kuna muda huwa nafikiri kama hizi nchi mbili (Angola na Zimbabwe) zisingejiingiza kwenye ile Vita upande wa Kabila huenda hii nchi (Drc) leo hii ingekuwa imepasuka vipande vipande huku Rwanda na Uganda wakidhibiti maeneo makubwa ya Madini huko Mashariki.

Drc iliyopasuka vipande vipande ingehatarisha usalama wa eneo lote la maziwa makuu, Ukanda wote wa SADC (hasa Angola, Tanzania na Zambia) na hata Africa Mashariki (Tanzania ikiwa muathirika mkubwa).
 
Kweli kabisa mkuu
Labda nikumbushe tu Kagame amewahi Iteka Congo nzima wakati wa 1st congo war ya kumng'oa mobutu kutokea ziwa kivu mpaka port matadi!!

Sio hivyo tu alipotaka kumng'oa Kabila aliiteka tena congo na alifika mpaka kinshasa kabisa na kama sio msaada wa Angola basi angekua ameiteka Congo nzima ndani ya wiki 2 pekee.

Kwenye vita za kileo ukubwa wa nchi hauna maana yeyote sababu vita inapiganwa kwa teknolojia nyingi mfano matumizi ya ndege na makombora ya masafa marefu kwahiyo unaweza zingirwa kwenye anga na kumalizwa ndani ya wiki tu kabla hata majeshi ya ardhini hayajafika Dodoma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Tanzania ingeathirika kivipi kama hutojali nitoe tongotongo
Ni kweli mkuu ! Angola na Zimbabwe waliisaidia sana hii DRC kipindi kile.

Kuna muda huwa nafikiri kama hizi nchi mbili (Angola na Zimbabwe) zisingejiingiza kwenye ile Vita upande wa Kabila huenda hii nchi (Drc) leo hii ingekuwa imepasuka vipande vipande huku Rwanda na Uganda wakidhibiti maeneo makubwa ya Madini huko Mashariki.

Drc iliyopasuka vipande vipande ingehatarisha usalama wa eneo lote la maziwa makuu, Ukanda wote wa SADC (hasa Angola, Tanzania na Zambia) na hata Africa Mashariki (Tanzania ikiwa muathirika mkubwa).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hima Empire inahusisha ya Tanzania, Uganda, Kenya, Rwanda, Burundi na DRC Mashariki. Kenya wanao na ndio sababu kuna Mauaji yalifanyika ya Wapinzani wa PK.

Uzuri ni kuwa watu muendelee kuwaza kuwa ni stori za kijiweni ila mkae mkijiandaa kutawaliwa na Wahima. Uwekeni huu uzi kwa rejea ya siku zijazo

Bazazi
Itawezekana kama makabila yote 120 ni wajinga kiasi cha kuzidiwa akili na kabila moja na itawezekana maana propoganda kuwaonyesha wao ni bora zitawaingia watanzania kiasi cha kuamini hivyo ila sio leo labda miaka 50 ijayo wakati makabila mengi yatakuwa yamepoteza uasili wao kiasi cha kutojua asili ya mtu ila ipo siku hata technolojia ya kubaini uasili utatumika kabla ya mtu kutumikia taasisi nyeti
 
Malcom Lumumba Marehemu Baba wa Taifa mwalimu Kambarage Nyerere asingeshinda leo hii we ungekuwepo hai? au maybe mngekuwa mnaitwa waganda? who knows🤷‍♂️
hii mada imejaa ujinga mtupu, wivu, chuki, visasi, na kutojitambua.

What if Baba wa Taifa asingekukomboa kutoka kwenye unyampala wa mkoloni? we si ungekuwa bado kolokoloni tu? mbona kuna mengi ya kujiuliza tuu. Inakuwaje umeanzia matukio ya hivi karibuni? siku nyingine labda huwe unaanza tangu dunia ilivyoumbwa basi, tujue kabisa hauna agenda, just living the dream, mh? hizi mada za kijinga uwa zinaniuma sana even though sometimes huwa unaleta mada za kueleweka, hii mzee umeteleza kabisa.

Yani kwa kifupi we unaona bora mngeshindwa na Amini kuliko wanyarwanda au waganda kuishi maisha bora ya kupeta leo hii? mi mbona sikuelewi:rolleyes:. Achana na mambo ya kizamani, tupige hatua kaka, siku hizi umoja ndio nguvu.

Hebu jiulize, kama yale manterahamwe na wasaliti wanaotia matumbo yao mbele wasingekuwa na upenyo wa kuja huko nje na kuwa wanarudi mara kwa mara kuleta vita za kijingajinga, unafikiri sie tungekuwa tunaenda kuwasaka nchi za watu kwa misingi ipi? very weird post.

Btw Mheshimiwa Magufuli kawafikisha wapi kwa kuwaburuza😍, mtatia akili tu na maendeleo yatakuja hivyohivyo kinguvunguvu tu.

Acha ujinga mkuu, unataka kutwambia bila ya mwalimu TZ tungekua tunatawaliwa na Queen mpaka leo? na weye pia unajiona umeelimika 😂😂😂
 
Kwa upande wa TZ ya uhakika ambayo yangetoka ni kua tusingekua tunatawaliwa tena CCM kwa muda hii, nayo ingekua ni baraka kubwa kwetu.
 
Labda nikumbushe tu Kagame amewahi Iteka Congo nzima wakati wa 1st congo war ya kumng'oa mobutu kutokea ziwa kivu mpaka port matadi!!

Sio hivyo tu alipotaka kumng'oa Kabila aliiteka tena congo na alifika mpaka kinshasa kabisa na kama sio msaada wa Angola basi angekua ameiteka Congo nzima ndani ya wiki 2 pekee.

Kwenye vita za kileo ukubwa wa nchi hauna maana yeyote sababu vita inapiganwa kwa teknolojia nyingi mfano matumizi ya ndege na makombora ya masafa marefu kwahiyo unaweza zingirwa kwenye anga na kumalizwa ndani ya wiki tu kabla hata majeshi ya ardhini hayajafika Dodoma.
Mkuu hivi kwenye vita za kongo, Kagame alikuwa peke yake au alitumia makundi ya waasi yaliyokuwa yanampinga Kabila ?
 
Ni kweli mkuu ! Angola na Zimbabwe waliisaidia sana hii DRC kipindi kile.

Kuna muda huwa nafikiri kama hizi nchi mbili (Angola na Zimbabwe) zisingejiingiza kwenye ile Vita upande wa Kabila huenda hii nchi (Drc) leo hii ingekuwa imepasuka vipande vipande huku Rwanda na Uganda wakidhibiti maeneo makubwa ya Madini huko Mashariki.

Drc iliyopasuka vipande vipande ingehatarisha usalama wa eneo lote la maziwa makuu, Ukanda wote wa SADC (hasa Angola, Tanzania na Zambia) na hata Africa Mashariki (Tanzania ikiwa muathirika mkubwa).
Tanzania ingeathirikaje zaidi ?
Sasa kwanini haikuisaidia Kongo ?
 
Mkuu hivi kwenye vita za kongo, Kagame alikuwa peke yake au alitumia makundi ya waasi yaliyokuwa yanampinga Kabila ?
Mkuu Kataskopos ni kweli alitumia proxies kama ambavyo Tanzania ilipovamia uganda nayo ilikuwa na proxies, kiufupi hakuna full scale war mtu apeleke jeshi peke ake bila kuwa na interested parties ndani ya nchi ambao wanaweza saidia logistics na uzoefu.

Lakini hii haiondoi ukweli kuwa main army ya kufanya offense mashariki ya DRC ilikua ni RPF hta namba ya AFDL zaidi ya 50% walikua wanyarwanda hivyo twaweza sema kwa simple majority basi KAGAME alivamia DRC na kuiteka licha ya ukubwa wake
 
Malcom Lumumba,

Mjadala mzito sana huu mwalimu Malcom, lakini itabidi tu nikujibu. Tanzania haikuwa na lengo wala wazo la kuwasaidia hao unaowaita ndugu zetu.

Tanzania tulipigana Vita kulinda Utu, mipaka, na heshima yetu, hiyo kuwasaidia ni neno la diplomasia tu.

Waganda na Watutsi waliokuwepo uhamishoni wangeweza kufanya hayo bila msaada wa Tanzania, kupitia nguvu ya umma, japo ingechukua muda, ila ingekuja tu.

Tanzania ndio ilichokoza Idd Amin kwa kuhifadhi maelfu ya waasi wa Uganda na kuwapa matunzo na mafunzo, hao wote akina Museveni walianzia Tanzania. Tatizo historia huwa hamuongelei kule yalianzia, huwa mnaanzia pale Amin alivamia Kagera, lakini hamuongei kuhusu ugomvi wote ulikoanzia.
 
Tanzania ingeathirikaje zaidi ?
Sasa kwanini haikuisaidia Kongo ?
Kama Drc ingepasuka Tz ingekua mmoja ya nchi ambayo ingejikuta ikipokea maelfu ya wakimbizi kutoka huko maana ingekuwa vigumu utulivu kurejea huko.

Hawa wakimbizi wangehatarisha usalama (baadhi hujiingiza kwenye uhalifu mipakani) na hata uharibifu wa mazingira (ukataji miti na kusafisha mapori ili kuanzisha kambi).

Drc iliyopasuka vipande vipande ingekua eneo zuri la mataifa makubwa na makundi haramu ya kigaidi kulitumia kama eneo mkakati la kuratibu,kupanga na kutekeleza hujuma za kiusalama dhidi ya tawala za nchi jirani (Tz) ambazo hawatokubaliana nazo.

Ile ndoto ya waasisi na wapigania Uhuru wa hili bara ya kuwa na Africa moja iliyoungana ingezidi kuzama ikiwa Drc ingepasuka na kuzuka viji nchi vidogo vidogo ambavyo vinadhibitiwa na makundi yenye silaha.

Tanzania haikujiingiza kwenye huo mzozo kuepusha haya:

Athari za kiuchumi maana nchi jirani (Drc,Uganda,Rwanda) zenye kutumia bandari yetu zilikuwa vitani hivyo kujiingiza kwa TZ upande wowote kungevuruga biashara Kati yake na taifa moja wapo.

Kulinda hadhi na heshima yake kimataifa, sote tunafahamu jinsi Tanzania ilivyokuwa mstari wa mbele kwenye harakati za kudai uhuru wa nchi za huku Kusini mwa Africa, hivyo kujiingiza huko kungeifanya ionekana kama "aggressor" hivyo hadhi yake kama mpatanishi mwenye kuheshimiwa kimataifa ingeporomoka.

Pia ingejikuta njia panda kidiplomasia na mwishowe kulazimika kuchagua upande maana washirika wote wa ile Vita walikuwa na uhusiano naye mfano

(Angola ,Drc na Zimbabwe hawa ni wanachama wa SADC na Tz ikiwemo)

Uganda (jirani wa Tz mshirika mkubwa wa kiuchumi na nchi rafiki)

Rwanda (jirani wa karibu na kuna muingiliano wa kibiashara na kijamii Kati ya raia wake na Tz)

Sasa hili ndilo kubwa liliomzuia kuingilia Vita ya Drc kijeshi japo pia Tz ilihusika kwenye upatanishi.
 
Kama Drc ingepasuka Tz ingekua mmoja ya nchi ambayo ingejikuta ikipokea maelfu ya wakimbizi kutoka huko maana ingekuwa vigumu utulivu kurejea huko.

Hawa wakimbizi wangehatarisha usalama (baadhi hujiingiza kwenye uhalifu mipakani) na hata uharibifu wa mazingira (ukataji miti na kusafisha mapori ili kuanzisha kambi).

Drc iliyopasuka vipande vipande ingekua eneo zuri la mataifa makubwa na makundi haramu ya kigaidi kulitumia kama eneo mkakati la kuratibu,kupanga na kutekeleza hujuma za kiusalama dhidi ya tawala za nchi jirani (Tz) ambazo hawatokubaliana nazo.

Ile ndoto ya waasisi na wapigania Uhuru wa hili bara ya kuwa na Africa moja iliyoungana ingezidi kuzama ikiwa Drc ingepasuka na kuzuka viji nchi vidogo vidogo ambavyo vinadhibitiwa na makundi yenye silaha.

Tanzania haikujiingiza kwenye huo mzozo kuepusha haya:

Athari za kiuchumi maana nchi jirani (Drc,Uganda,Rwanda) zenye kutumia bandari yetu zilikuwa vitani hivyo kujiingiza kwa TZ upande wowote kungevuruga biashara Kati yake na taifa moja wapo.

Kulinda hadhi na heshima yake kimataifa, sote tunafahamu jinsi Tanzania ilivyokuwa mstari wa mbele kwenye harakati za kudai uhuru wa nchi za huku Kusini mwa Africa, hivyo kujiingiza huko kungeifanya ionekana kama "aggressor" hivyo hadhi yake kama mpatanishi mwenye kuheshimiwa kimataifa ingeporomoka.

Pia ingejikuta njia panda kidiplomasia na mwishowe kulazimika kuchagua upande maana washirika wote wa ile Vita walikuwa na uhusiano naye mfano

(Angola ,Drc na Zimbabwe hawa ni wanachama wa SADC na Tz ikiwemo)

Uganda (jirani wa Tz mshirika mkubwa wa kiuchumi na nchi rafiki)

Rwanda (jirani wa karibu na kuna muingiliano wa kibiashara na kijamii Kati ya raia wake na Tz)

Sasa hili ndilo kubwa liliomzuia kuingilia Vita ya Drc kijeshi japo pia Tz ilihusika kwenye upatanishi.

Bado nadhani Kagame ana mpango maalumu na Congo na mpango wake wa kunyakua eneo lenye wanyamurenge wengi huko Congo sidhani kama umeisha naona kama anauvutia kasi tu.
 
Bado nadhani Kagame ana mpango maalumu na Congo na mpango wake wa kunyakua eneo lenye wanyamurenge wengi huko Congo sidhani kama umeisha naona kama anauvutia kasi tu.
Hata kama huo mpango upo je unafikiri atafanikiwa?

Je serikali ya Drc na raia wa huko unafikiri watakubali hilo?

Je jumuiya ya kimataifa, nchi jirani na Drc na nchi rafiki za Drc (SADC) wataruhusu/watakubali hilo?
 
Hata kama huo mpango upo je unafikiri atafanikiwa?

Je serikali ya Drc na raia wa huko unafikiri watakubali hilo?

Je jumuiya ya kimataifa, nchi jirani na Drc na nchi rafiki za Drc (SADC) wataruhusu/watakubali hilo?

Kufanikiwa/kutofanikiwa hio itategemea mkuu.

Serikali ya Drc/wananchi wake hawana chochote cha kufanya maana PK alishawavamia mara 2 na hawakufanya chochote cha maana na mpk sasa bado huko maporini Congo ana vijana wake.

Serikali ya Congo bado haijawa imara kijeshi na hata Georgraphy ya Congo ilivyokaa si ya mchezo,lkn pia kuitawala nchi kubwa kama Congo yenye ukubwa wa mara 2.5 ya Tanzania inabidi uwe na taasisi imara kweli kweli kitu ambacho Congo bado hawajawa na uwezo huo.Angalia mfano tu Msitu wa Congo pekee ume cover (1,145,000 sq km) yaani ni mkubwa kuliko nchi yote ya Tz(945,087 sq km) nadhani mpk hapo tu unaweza kuelewa nchi ya dizaini hio ni ngumu kiasi gani kuitawala au waasi wakijificha humo shughuli yake inakuaje.

Kipindi cha vita vya pili vya Congo walioifanya Congo isikamatwe tena na PK mostly ni angola,Zimbabwe na kiasi flani Namibia ambapo kipindi hicho mahusiano yao binafsi ya kina Mugabe na Dos Santos vs na PK yalikua ni mabaya saana lkn PK ni kama alishaona umuhimu/nguvu ya Sadc na akaamua kujenga urafiki nao na sasa wamekua washkaji zake sana tu.

Rais wa sasa wa Angola Lourenço ni mshkaji wake sana tu na Kagame na ni msuluhishi mgogoro wa Rwd vs Uganda na hata Uganda inalalamika urafiki binafsi wa PK na Lourenço ni mkubwa,trip za kigali/ haziishi.

Rais wa Zimbabwe Mnangagwa(akijulikana kama the crocodile kipindi cha vita hio ya Congo alikua front na majeshi ya Zimbabwe) nae ni mshkaji wake kila siku trip zao za kigali/harare na hata sasa madini ya Zimbabwe ambapo yaliwekewa vikwazo kuna michalato inafanyikia Kigali,yanauzika fresh huko wanakojua wao.

Rais wa Tz naona nae wana mahusiano mazuri tu ya kikazi/kibiashara,Magu amefanikisha 90% ya mizigo yote ya Rwanda kupitia Bandari ya Dar lkn pia sera za Magu ni za kuangalia sisi tunafaidika nini na kutokujiingiza kwny migogoro ya watu maana yeye mwenyewe hua anasema nchi hii tumesaidia nchi nyingi sana lkn in return tumepata zero.

Zambia Rais wao Lungu n PK wako fresh kabisa.

Namibia pia wako nayo kwny mahusiano bora kuliko kipindi chochote kile.

South Africa ndio mahusiano yao na PK hua yako 50%|50% sababu ya wakina Nyamwasa kuishi kule na Karegeya alivyouwawa kule,lkn South Africa inapitisha sheria kwamba Mkimbizi yoyote wa kisiasa atayeishi nchini kwao hataruhusiwa kujihusisha na siasa za nchi kwao alikotoka either kwa kuunda chama chake/kufanya vuguvugu zozote akiwa nchini humo la sivyo atanyang’anywa hio hadhi ya ukimbizi na tayari wakina Nyamwasa wameshalamikia jambo hilo so maji yatakua shingoni hapo.Na kwa maana hio uhusiano wa Rwanda na SA utaboreka maana hakutakua na sababu ya msingi ya PK kutuma vijana wake huko SA.

Malawi pia sio kama wana inshu yoyote na PK na wanyalu wengi sana wako huko wanaishi huko malawi wakipiga biashara zao.

Comoro wako nayo poa sana na hata muasi wa Rwanda aliyekua anajiita major Sankara walimdakia hapo hapo Comoro.

Nchi nyingine kama Mauritius,Madagaskar,Eswatin etc sijazotaja sababu sijaona kama hua wanajihusisha sana kijeshi kwny migogoro ya sadc,hata hio Comoro nimeitaja tu sababu ya huyo Sankara.

So nadhani PK kua na mahusiano bora na Key players wa Sadc(Tz,Angola,Zimbabwe,Malawi,S/Africa,Zambia) inamuweka kwny nafasi bora siku ikifika akitaka kufanya mambo huko Congo.

Ni mtizamo tu.
 
Kama Drc ingepasuka Tz ingekua mmoja ya nchi ambayo ingejikuta ikipokea maelfu ya wakimbizi kutoka huko maana ingekuwa vigumu utulivu kurejea huko.

Hawa wakimbizi wangehatarisha usalama (baadhi hujiingiza kwenye uhalifu mipakani) na hata uharibifu wa mazingira (ukataji miti na kusafisha mapori ili kuanzisha kambi).

Drc iliyopasuka vipande vipande ingekua eneo zuri la mataifa makubwa na makundi haramu ya kigaidi kulitumia kama eneo mkakati la kuratibu,kupanga na kutekeleza hujuma za kiusalama dhidi ya tawala za nchi jirani (Tz) ambazo hawatokubaliana nazo.

Ile ndoto ya waasisi na wapigania Uhuru wa hili bara ya kuwa na Africa moja iliyoungana ingezidi kuzama ikiwa Drc ingepasuka na kuzuka viji nchi vidogo vidogo ambavyo vinadhibitiwa na makundi yenye silaha.

Tanzania haikujiingiza kwenye huo mzozo kuepusha haya:

Athari za kiuchumi maana nchi jirani (Drc,Uganda,Rwanda) zenye kutumia bandari yetu zilikuwa vitani hivyo kujiingiza kwa TZ upande wowote kungevuruga biashara Kati yake na taifa moja wapo.

Kulinda hadhi na heshima yake kimataifa, sote tunafahamu jinsi Tanzania ilivyokuwa mstari wa mbele kwenye harakati za kudai uhuru wa nchi za huku Kusini mwa Africa, hivyo kujiingiza huko kungeifanya ionekana kama "aggressor" hivyo hadhi yake kama mpatanishi mwenye kuheshimiwa kimataifa ingeporomoka.

Pia ingejikuta njia panda kidiplomasia na mwishowe kulazimika kuchagua upande maana washirika wote wa ile Vita walikuwa na uhusiano naye mfano

(Angola ,Drc na Zimbabwe hawa ni wanachama wa SADC na Tz ikiwemo)

Uganda (jirani wa Tz mshirika mkubwa wa kiuchumi na nchi rafiki)

Rwanda (jirani wa karibu na kuna muingiliano wa kibiashara na kijamii Kati ya raia wake na Tz)

Sasa hili ndilo kubwa liliomzuia kuingilia Vita ya Drc kijeshi japo pia Tz ilihusika kwenye upatanishi.
Sasa kwanini Tanzania ilingilia zile za kumtoa Hyabarimana 1994 na Mobutu 1997, vipi hizi athari hazikuwepo ?
 
Ni kweli mkuu & the point to note huu ukanda toka enzi za mwalimu jk ulijengwa ktk misingi ya matabaka ya wahima au nilotics na wabantu ambapo hawa kina mwalimu walitaka kuzitawala Tz , Brndi , Rwnda, Congo ,Ugnda then Kenya na kwa ushahidi tu wa hilo 1.Idd Amin mwalimu hakumpenda kwakua bantu 2.Marais wakibantu toka Burnd & Rwnda walidunguliwa wakitokea Tz na walipandishwa ndge moja ili mpango uende vizuri 3. Rais Kabila 'bantu'wa Congo aliuliwa na kina kagame na m7 sababu zile zile ili waishike nchi NDADAYE wa Burndi alichinjwa mchango wa kagame upo 4. Juzi Nkurunziza aliandaliwa mapinduz kwakua tu ni mhutu walio andaa zoezi likashindwa walikimbilia kwa kagame mpaka leo wamehifadhiwa huko 5. kagame huyo alitaka kumkagame Mh JK Kikwete n.k n.k hivyo kifupi hima empire ni mpango ulikuwepo ila kwa neema ya MWENYEZI tu.
Hivi mkuu kwanini Tanzania haikufanya chochote wakati yale mauaji makubwa dhidi ya watutsi yakiendelea kule nchini Rwanda ??? Ikumbukwe kwamba Tanzania alikuwa ni mhusika mkubwa sana kwenye usuluhishi wa mgogoro dhidi ya Watutsi na Wahutu: Lakini kwanini hakufanya chochote kile ???
 
Vita ya Kagera ilizaa mambo mengi sana kwenye ukanda huu ambayo yanatokea leo hii.

..labda RWANDAN GENOCIDE isingetokea.

..kusingekuwa na DRC, bali kungekuwa na Zaire.

..kusingekuwa na wanaojulikana kama waasi wa mashariki mwa DRC.

..Mwalimu angeondoka madarakani mapema kabla hajaanza ukorofi wake dhidi ya WB, na IMF.

..Tanzania tusingepitia vikwazo vya WB na IMF hivyo uchumi wetu usingeathirika kama ilivyotokea.

..Huenda Zanzibar ingejitoa kwenye muungano.
 
..labda RWANDAN GENOCIDE isingetokea.

..kusingekuwa na DRC, bali kungekuwa na Zaire.

..kusingekuwa na wanaojulikana kama waasi wa mashariki mwa DRC.

..Mwalimu angeondoka madarakani mapema kabla hajaanza ukorofi wake dhidi ya WB, na IMF.

..Tanzania tusingepitia vikwazo vya WB na IMF hivyo uchumi wetu usingeathirika kama ilivyotokea.

..Huenda Zanzibar ingejitoa kwenye muungano.
Ndugu yangu JokaKuu una uono mkubwa sana; Watanzania wengi hawalioni hili kabisa.
Ile vita ilizaa mambo mabaya sana kwenye huu ukanda ambayo yanaitesa Tanzania hadi leo.
 
Back
Top Bottom