Kama Mzazi, Hili limeniumiza Sana Sana.

Kama Mzazi, Hili limeniumiza Sana Sana.

bampami

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2011
Posts
5,700
Reaction score
4,126
Habarini waungwana!

Jana nilikutana na jamaa
yangu mmoja ambaye ni
muhudumu wa afya,
akanipa ofa (si kawaida
yake). Kwa hali hiyo ikabidi
nimdadisi, ndo akaniambia amepewa ahsante baada ya
kumfanyia uchunguzi na
councelling mtoto mmoja
wa form 1 (13yrs) katika
shule fulani ya boarding!
Baada ya kudadisi vizuri zaidi akaniambia kuwa
huyo mtoto amelatiwa na
mtu mzima (possibly mlinzi
wa shule) ila ameambiwa
amfanyie councell mtoto
asije kutangaza (Shiit) ili kuharibu jina la shule hiyo!
Sasa kama mzazi najiuliza
usalama wa watoto wetu
huko mashuleni,
tunawapeleka bado
wadogo sana then inakuwa ni mbali halafu wanakaa
muda mrefu,
Jambo hili limeniuma ndo
maana nikalileta hapa!
Ushauri wangu Kama mzazi,
muangalie watoto wenu, Msijifanye mko biiize
kutafuta hela mpaka
mnawatupa boarding
school wakiwa wadogo
(hata kujitetea hawawezi)
Naandika ikiwa bado nimeumia as if ni mtoto
wangu ndo amefanyiwa
hivo!
 
Ukweli unaouma ni kwamba waharibifu wakubwa wa watoto wetu ni wale tunaowaamini sana na wala hatutarajii wafanye hayo!!Wapo walimu na watumishi wa shule na vyuo,wapo ndugu wa karibu majumbani kama binamu,baba wadogo,houseboys na housegirls,shambaboys na hata madereva wetu,hata walimu wa tuition majumbani; NB;Kama mzalendo hata wewe unaweza kututajia jina la shule na huyo councellor ili tupate kuwafanyia kazi kama kweli imekuuma kama mzazi! IT BEGINS WITH YOU bampami!
 
Kama kweli imekuuma yaweke wazi , japo utakuwa umemuharibia then tubu kwa sbb hy hela ya ofa mlotumia ndo hy alopewa kuficha ukweli , zinduka bampami!!!
 
Ungeitaja hiyo shule ili tulio na wana huko tukaanza kumulika. Usishirikiane nao kwenye uovu wao.
Eti mtoto wa miaka minne naye unapeleka boarding, kisa ili na wewe uonekane unasomesha shule ya gharama; hiyo ni akili au matope?
 
Ungeitaja hiyo shule ili tulio na wana huko tukaanza kumulika. Usishirikiane nao kwenye uovu wao.
Hicho ndiyo nilichokuwa nakifikiria. Kutuambia inakuuma halafu unaliacha libaki hivyo hivyo ni sawa na kusema kwamba unakubaliana na hayo yaliyotendeka. Katika kuonyesha kwa dhati kwamba huungi mkono, yafaa ututajie jina la hiyo shule ili hatua zichukuliwe. JF the place we dare to talk openly. Sema usiogope.
 
Siku hizi ndo mtindo,akiacha kunyonya boarding,clinic atamalizia akiwa shule,utaipanda to digital!!
 
Bampami, kwa ujasiri uleule uliotumia kushindana na konda wa daladala pale mwenge jana alietaka nauli ya buku ukatoa mia 3. Nimesoma thread yako ya "kilichotokea mwenge stand toa maoni yako"
Basi itaje hiyo shule km mzazi tukomeshe hiyo tabia,
 
1.Shule hata ikitajwa haisaidii hapa TANZANIA.

2.Watuhumiwa wakitajwa pia HAWACHUKULIWI HATUA

3.Mtoto akitajwa naye atanyanyapaliwa na wenzake.

4.Hata mashahidi wakiletwa mbele ya baraza la shule watatolewa kafara ili shule kulinda jina lake na wanahisa wake.

5.Kwa kifupi kesi za namna hii zikishawekwa ndani ya kapeti ni ngumu kuzitoa.

Jamii nzima inayomzunguka mtoto huyu imefeli hapa kuanza juu board members wa shule,mkuu wa shule,walimu n.k wote chali.

Kama tunaweza kuuana kwa kugombania kuchinja wanayama,kama tunaweza kuchoma nyumba za ibada,pia tunaweza kuchochea chuki kati ya dini fulani au kabila fulani au ukanda fulani na ukanda mwingine au chama fulani na kingine inakuaje jamii ile ile inashindwa kumshughulikia mtuhumiwa kama kashatajwa ni mlinzi?

Hatuwatendei haki victims katika nchi hii.
 
Back
Top Bottom