Kama kweli unanipenda tukapime UKIMWI

Kama kweli unanipenda tukapime UKIMWI

Crucial b

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2015
Posts
276
Reaction score
110
Wanajamvi,

Kama kawaida yangu mgeni nisiyekosa neno nimerudi tena na tafakuri hii, kutokana na kusalitiana na mahusiano mengi kulega lega sana hasa kwa vijana wa kileo a.k.a. Makeup boys n' girls je? ni sahihi kweli kipimo cha mapenzi ya kweli kibaki kupima UKIMWI kwanza kabla na baada ya kuanza mahusino tena mara kwa mara ukizingatia kitapunguza sana tatizo la watu kuchepuka kulikokithiri na kusabisha magonjwa yanayoepukika.

Mimi ukinipenda au nikakupenda moja kwa moja kwenye vipimo kwanza mengine baadae au ndo nitawakosa kabisa mabinti?, sijui vijana wenzangu imekaaje hapo maana tunajuana wanaume tulivyowabishi kupima UKIMWI na ukitaka talaka isiyo na maelezo ya kutosha au upigwe kibuti mchana kweupeee! mwambie mtu wako mkapime UKIMWI uone shughuli yake ilivyo pevu, mabinti kwanini hamuwakomalii watu wenu wapime ukimwi?

Hebu naomba tukumbushane siku ya kwanza uliyopima UKIMWI hali ilikuwaje upande wako ?

Ni hayo tu wakuu.
 
Yaan wewe nimekupenda aisee cna jns imebid nkwambie ukwel tu,, endelea na msimamo huohuo hata cc tupo tunaotaka mahucan yawe ivo potelea mbal hata tukibadili wanaume / wanawake kama magaun ilmrad tunanusuru uhai wetu.
 
Siku hizi ukimwi so ishu kabisa... Umepima Mara ya kwanza huna Mara ya pili ukarudi huna Mara ya tatu huna mjomba unachokitafuta utakipata
 
Hivi dunia ya sasa kuna watu kweli wanaingia kwenye mahusiano pasipo kupima ukimwi!
 
usisahau kupima ujazo wa maji na kina cha bahari mana siku hizi vijana wanataka kujiridhisha kabla ya yote.
 
Yaan wewe nimekupenda aisee cna jns imebid nkwambie ukwel tu,, endelea na msimamo huohuo hata cc tupo tunaotaka mahucan yawe ivo potelea mbal hata tukibadili wanaume / wanawake kama magaun ilmrad tunanusuru uhai wetu.

akhsante! mee too.
 
Siku hizi ukimwi so ishu kabisa... Umepima Mara ya kwanza huna Mara ya pili ukarudi huna Mara ya tatu huna mjomba unachokitafuta utakipata
kipi bora sasa hapo madame s kupima au kuendelea kuishi kwa matumaini kuwa huna huku unao na unaendelea kuua watu bila kujua tena kila sku za ibada unaenda kanisani au mskitini kusali acha uoga bhana kapime isitoshe unadai siyo issue coz haujakukuta, msiba usikie kwa jirani siyo kwako madame s
 
Hivi dunia ya sasa kuna watu kweli wanaingia kwenye mahusiano pasipo kupima ukimwi!

hivi unaongelea mahusiano gani mamii yaani kama ni haya ya kukutana shule, mitaani, vyuoni au kwingine kuna cha kupima ukimwi kweli labda ya kuoana kama mke na mme
 
kipi bora sasa hapo madame s kupima au kuendelea kuishi kwa matumaini kuwa huna huku unao na unaendelea kuua watu bila kujua tena kila sku za ibada unaenda kanisani au mskitini kusali acha uoga bhana kapime isitoshe unadai siyo issue coz haujakukuta, msiba usikie kwa jirani siyo kwako madame s


Kuna maradhi mengi Sana ukiacha ukimwi kuna hadi magrupu mengine ya damu mkioana kupata watoto inakua ngumu watu hatuelewi tumekomalia ukimwi me napima bila kushurutishwa and f.y.i nimepima mwezi huu WA kum na moja narudi mwezi WA pili mwakani roho zikowa hai
 
Kuna maradhi mengi Sana ukiacha ukimwi kuna hadi magrupu mengine ya damu mkioana kupata watoto inakua ngumu watu hatuelewi tumekomalia ukimwi me napima bila kushurutishwa and f.y.i nimepima mwezi huu WA kum na moja narudi mwezi WA pili mwakani roho zikowa hai

usipanic ni mawazo tu madame s
 
usisahau kupima ujazo wa maji na kina cha bahari mana siku hizi vijana wanataka kujiridhisha kabla ya yote.

kuna haja ya kufanya utaratibu wa kujuana hata kwa jinsia maana itafikia hatua mjomba ataitwa shangazi humu jf
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom