Nipe Maji
JF-Expert Member
- Mar 25, 2025
- 335
- 190
Wakuu
Hii mitambo ya kutengeneza barabara inanunuliwa sana kipindi hiki kuelekea uchaguzi, siku zote wanakuwa wapi? au ndo kura zinatafutwa kwa kuhadaa wananchi. Alafu mtambo huo huo baada ya uchaguzi utakuta unaharibika
=====
Mbio za Mwenge wa Uhuru umezindua mtambo wa kutengeneza barabara (Motor Grader) wenye thamani ya shilingi bilioni 1.2 ambao utatumika kwenye shughuli za ujenzi na ukarabati wa barabara katika wilaya Kaliua iliyopo mkoani Tabora.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Dk. Gerald Mongela, amesema mtambo huo utawezesha barabara za wilaya hiyo kupitika katika kipindi chote.
“Kama unavyofahamu wilaya yetu idadi kubwa ya wananchi wake wanajishughulisha na kilimo, hivyo mtambo huu utafungua barabara hadi zile za mashambani kuwawezesha wananchi kusafirisha mazao yao hususan tumbaku bila kikwazo,” amesema Dk. Mongella.
Hii mitambo ya kutengeneza barabara inanunuliwa sana kipindi hiki kuelekea uchaguzi, siku zote wanakuwa wapi? au ndo kura zinatafutwa kwa kuhadaa wananchi. Alafu mtambo huo huo baada ya uchaguzi utakuta unaharibika

=====
Mbio za Mwenge wa Uhuru umezindua mtambo wa kutengeneza barabara (Motor Grader) wenye thamani ya shilingi bilioni 1.2 ambao utatumika kwenye shughuli za ujenzi na ukarabati wa barabara katika wilaya Kaliua iliyopo mkoani Tabora.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Dk. Gerald Mongela, amesema mtambo huo utawezesha barabara za wilaya hiyo kupitika katika kipindi chote.
“Kama unavyofahamu wilaya yetu idadi kubwa ya wananchi wake wanajishughulisha na kilimo, hivyo mtambo huu utafungua barabara hadi zile za mashambani kuwawezesha wananchi kusafirisha mazao yao hususan tumbaku bila kikwazo,” amesema Dk. Mongella.