Kakobe atoa mpya, aitilia mkwara serikali

Kakobe atoa mpya, aitilia mkwara serikali

Herbalist Dr MziziMkavu

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,074
Reaction score
34,844
Wednesday, March 10, 2010 10:27 AM
MKUU wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Mchungaji Zachary Kakobe, amesema umeme unaopitishwa sasa kanisani kwake hautafanya kazi ipasavyo kwa maombi atakayofanya na anaamini umeme hautawaka kwa nguvu ya Mungu kwa vile hakuna nguvu zita Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Askofu Kakobe alisema ameshangazwa na kauli ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, kuutangazia umma kuwa ameridhia umeme huo kupitishwa kwenye kanisa hapo.

Alisema kwa kuwa serikali imekaidi agizo lake na yeye hana uwezo wa kukataa maamuzi hayo basi atacha ujenzi uendelee lakini hakuna umeme utkaofanya kazi mahalai hapo kut okana na maombi atakayoungurumisha kanisani hapo kupinga kupitihswa kwa ueme huo hapo.

“Huu ni uonevu wa hali ya juu, sijakubaliana na maamuzi hayo kwa kuwa vipimo vyote vilivyotolewa havikuwa vya kweli, vilikuwa ni vya kughushi na ndio mana sikukubaliana na Waziri Ngeleja alivyotoa taarifa yake ” alisema Askofu Kakobe.

Alisema hivi sasa amegundua hawatakiwi kupinga upitishaji wa umeme huo kimwili kama walivyokuwa wamefanya huko siku za nyuma bali ni kutakiwa kukaa katika maombi kupinga suala hilo na hataweza kubishana na watu wasiomtambua Mungu.

Alisema hivi sasa amepata taarifa za uhakika kuwa baadhi ya watu wamepewa taarifa kuwa wanatakiwa kuhama katika eneo hilo kupisha upitishaji wa nguvu hiyo ya umeme kitendo ambacho kinampa ishara kuwa kuna mpango wa kanisa lake kuvunjwa.

Askofu Kakobe alipingana na madai yaliyotolewa na Mshauri Mtaalam wa Kampuni ya BICO, kuwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), linatakiwa kuepukana na kona kali kwenye waya na kutounganisha sehemu yoyote kati ya nguzo namba 18 na 19.

“Nakwambia hata wakipitisha umeme huu hapa… hautawaka kwa vile nguvu ya Mungu itashinda nguvu ya umeme lakini kibaya nimesikitishwa na Waziri Ngeleja kuutangazia umma eti nimekubali umeme upitishwe hapa, nasema siyo kweli jamani,” alisema Askofu Kakobe.




http://javascript<b></b>:__doPostBack('LinkButton3','')
 
Sure, hii kauli ni nzito tupe source.Manake kama kasema hivo kweli,lol,na umeme uje kuwaka itakuwa sooo!!
 
mbona kachelewa jamani kama alijua mungu anaweza kuzuia umeme usipite kwa maombi kwanini kuwatesa watu hivyo jamani kukesha hivyo na kuwapa watu faida kwa malumbano ya vyombo vya dola ebu tuwape mda tutajua nani mkweli tanesko, kakobe au mungu ila kwa kdri nijuaavyo mungu adhiakiwi umeme ukiwashwa na ukafanya kazi mungu atokuwa mwongo ila kakobe
 
Askofu Kakobe anatishia nyau na mwisho wa siku ataaibika. Mungu wa Abraham, Isaka na Yakobo ambaye ndiye Mungu wa Israel hawezi kusikiliza hoja za kipuuzi za Kakobe. Umeme utawaka kama kawaida ili watu wapate maendeleo.
 
Kakobeeeeeeee! Haya sasa ngoja tusubiri kitakachotokea.
 
kama serikali inalitaka lile eneo kwa nn wasimhamishie eneo lingine kwa makubaliano. nadhani ni kitu kirahisi tu. hawa TANESCO si ndio walishindwa kupitisha umeme juu ya makaburi? then now watafanyaje hii hali ikijirudia? they dont consider cost?
 
Back
Top Bottom