Kakakuona agoma kutabiri, achapa usingizi mzito

Kakakuona agoma kutabiri, achapa usingizi mzito

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Hadi Kakakuona amegoma kutiki🤣🤣🤣 kasema "No Reforms?... bora nilale😂😂"
================
Mnyama adimu kuonekana, Kakakuona ameonekana akiwa na mtoto wake katika Kijiji cha Lilondo Halmashauri ya Wilaya ya Madaba wilayani Songea mkoani Ruvuma, huku akitarajiwa kutabiri mambo mbalimbali ikiwemo Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29 mwaka huu, ambapo hata hivyo licha ya kuwekewa vitu mbambali alishindwa kutabiri na kubaki amelala.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Bw. Wilman Ndile, amesema wanamchukua mnyama huyo na mtoto wake na kumpeleka kwenye bustani ya wanyamapori ya Ruhila kumhifadhi.
 
Mkuu wa wilaya anaitwa nani
Kiongozi mwenye imani za kishirikina huku akihudhuria sawia nyumba za ibada
 
Uchaguz hamna mwaka huu sababu waliopanga kuuvuruga ni ccm maana mwenyekit sio chaguo lao ni urithi tu unafanya awe mwenyekiti wamechukia balaaaa
 
Back
Top Bottom