Kaisho secondari kwawaka moto

Kamakabuzi

JF-Expert Member
Dec 3, 2007
2,861
1,302
Kuna taarifa kuwa bweni la wavulana wa kidato cha sita Kaisho sekondari iliyoko Karagwe limeunguzwa usiku wa kuamkia leo 8.2.2011 lakini hakuna mwanafunzi aliyejeruhiwa kwa kuwa wote walikuwa madarasani kwenye prep.
Fujo zilianza jumamosi baada ya mechi ya mpira wa miguu kati ya form six na form IV ambapo kidato cha nne walishinda. Tambo zilianzia hapo lakini zilififia.
Kwa kuwa kila jumamosi huwa ni siku ya vijana kuangalia TV, muda ulipofika wakamuomba second master awawashie TV waangalie, lakini yeye aliwambia kuwa kwa kuwa wanatarajia kupokea ugeni toka Karagwe sec kesho yake, muda huo wautumie kufanya maandalizi, Form IV hawakuridhika (wakipandishwa jazba na ushindi wa mpira) ndipo walizima umeme na kuwalazimisha form III, II na I kujiunga nao na kuanza vurugu.
Chumba cha computer na photocopy machines kilivunjwa na vyote kuharibiwa, ream za karatasi zkachanwachanwa; duka la shule lilivunjwa na walipokuta humo vinywaji wakalewa kabisa kisha wakavamia stoo ya vyakula na kuharibu maharage, sukari mchele nk kwa kuvitupa nje, magari mawili ya waalimu yalivunjwa vioo! nk.
Jana baada ya kikao,. kidato cha nne wakaamriwa kurudi makwao; lakini la ajabu ni usiku wa leo kutokea hayo ya kuchoma moto bweni.
Habari hizi nimezisikia toka Radio Fadeco ya Kayanga Karagwe.
Inasemekana malalamiko ya wanafunzi ni pamoja na kutaka mkuu wa shule aliyeacha kazi hivi karibuni arudishwe.
 
Kuna taarifa kuwa bweni la wavulana wa kidato cha sita Kaisho sekondari iliyoko Karagwe limeunguzwa usiku wa kuamkia leo 8.2.2011 lakini hakuna mwanafunzi aliyejeruhiwa kwa kuwa wote walikuwa madarasani kwenye prep.
Fujo zilianza jumamosi baada ya mechi ya mpira wa miguu kati ya form six na form IV ambapo kidato cha nne walishinda. Tambo zilianzia hapo lakini zilififia.
Kwa kuwa kila jumamosi huwa ni siku ya vijana kuangalia TV, muda ulipofika wakamuomba second master awawashie TV waangalie, lakini yeye aliwambia kuwa kwa kuwa wanatarajia kupokea ugeni toka Karagwe sec kesho yake, muda huo wautumie kufanya maandalizi, Form IV hawakuridhika (wakipandishwa jazba na ushindi wa mpira) ndipo walizima umeme na kuwalazimisha form III, II na I kujiunga nao na kuanza vurugu.
Chumba cha computer na photocopy machines kilivunjwa na vyote kuharibiwa, ream za karatasi zkachanwachanwa; duka la shule lilivunjwa na walipokuta humo vinywaji wakalewa kabisa kisha wakavamia stoo ya vyakula na kuharibu maharage, sukari mchele nk kwa kuvitupa nje, magari mawili ya waalimu yalivunjwa vioo! nk.
Jana baada ya kikao,. kidato cha nne wakaamriwa kurudi makwao; lakini la ajabu ni usiku wa leo kutokea hayo ya kuchoma moto bweni.
Habari hizi nimezisikia toka Radio Fadeco ya Kayanga Karagwe.
Inasemekana malalamiko ya wanafunzi ni pamoja na kutaka mkuu wa shule aliyeacha kazi hivi karibuni arudishwe.

Mkuu wa shule ameacha kazi,arudishwe?au una maana ameachishwa kazi?
 
Wakuu hizi habari ni mbaya ukizingatia jana wamewatimua kidato cha nne kwa mda usiojulikana, rakini viongozi wa ccm ndo wanahusika maana diwani wa Kata ya Rutunguru na mmiliki wa hotel ya western Estate ambaye ni mbunge ndo wamekuwa wanapewa tenda mbalimbali hapo shuleni kwa hiyo wanahamasiha vujo kama wote tukose hasa baada ya uongozi kukerwa na headmaster kuondolewa. Tenda za kuni, sherehe, vyakula, usafiri n.k vimekuwa vikitolewa kwa hao wafanyabiashara hasa diwani wa rutunguru. Na wakati wa uchaguzi baadhi ya walimu walishiriki kura za maoni za ccm kwa udiwani na kupiga kampeni hizo waziwazi ilihali ambao hawakusupport ccm walibanwa na kutishiwa kufukuzwa kazi. kata ya Isingiro diwani alipa kura nyingi kupitia mgongo wa hiyo shule na Headmaster anayeondoka alikuwa mmoja wa waliokuwa wanajumlisha matokeo ya jumla ya wilaya ya karagwe majimbo ya kyerwa na karagwe.
 
Mkuu wa shule ameacha kazi,arudishwe?au una maana ameachishwa kazi?

Mkuu wa shule aliacha kazi mwenyewe; sababu hasa hazijulikani.
Ni mtu ambaye wanafunzi na wazazi walikuwa wakimwamini na kumpenda, shule alikuwa ameipandisha chati.
Kimkoa ilikuwa ya 10 kati ya 155 na kitaifa ilikuwa 180 kati ya 3196
 
Wakuu hizi habari ni mbaya ukizingatia jana wamewatimua kidato cha nne kwa mda usiojulikana, rakini viongozi wa ccm ndo wanahusika maana diwani wa Kata ya Rutunguru na mmiliki wa hotel ya western Estate ambaye ni mbunge ndo wamekuwa wanapewa tenda mbalimbali hapo shuleni kwa hiyo wanahamasiha vujo kama wote tukose hasa baada ya uongozi kukerwa na headmaster kuondolewa. Tenda za kuni, sherehe, vyakula, usafiri n.k vimekuwa vikitolewa kwa hao wafanyabiashara hasa diwani wa rutunguru. Na wakati wa uchaguzi baadhi ya walimu walishiriki kura za maoni za ccm kwa udiwani na kupiga kampeni hizo waziwazi ilihali ambao hawakusupport ccm walibanwa na kutishiwa kufukuzwa kazi. kata ya Isingiro diwani alipa kura nyingi kupitia mgongo wa hiyo shule na Headmaster anayeondoka alikuwa mmoja wa waliokuwa wanajumlisha matokeo ya jumla ya wilaya ya karagwe majimbo ya kyerwa na karagwe.
Hilo la tenda za vyakula kupewa karagwe estate linawezekana kwani mara nyingi wakati kikiwa na mkutano wa wazazi chakula hupikwa pale (karagwe estate)
Suala la tenda ya kuni sina uhakika nalo ila nakumbuka kuna wakati shule ilinunua canter kwa ajili hiyo ya kuni na mizigo mingine.
 
Hilo la tenda za vyakula kupewa karagwe estate linawezekana kwani mara nyingi wakati kikiwa na mkutano wa wazazi chakula hupikwa pale (karagwe estate)
Suala la tenda ya kuni sina uhakika nalo ila nakumbuka kuna wakati shule ilinunua canter kwa ajili hiyo ya kuni na mizigo mingine.

Namaanisha tenda za mahindi ,maharage. Ambavyo ndo chakula cha wanafunzi mda wote
 
Hilo la tenda za vyakula kupewa karagwe estate linawezekana kwani mara nyingi wakati kikiwa na mkutano wa wazazi chakula hupikwa pale (karagwe estate)
Suala la tenda ya kuni sina uhakika nalo ila nakumbuka kuna wakati shule ilinunua canter kwa ajili hiyo ya kuni na mizigo mingine.

hakuna harufu ya kisiasa hapo? vipi kuhust cdm, kuna uwezekano maandamano ya amani yalipita jirani na maeneo ya Karagwe Estate! Jeshi la polisi lishirikishwe kuwasaka wote waliohusika na uharibifu shuleni hapo.
 
hakuna harufu ya kisiasa hapo? vipi kuhust cdm, kuna uwezekano maandamano ya amani yalipita jirani na maeneo ya Karagwe Estate! Jeshi la polisi lishirikishwe kuwasaka wote waliohusika na uharibifu shuleni hapo.

Maandamano ya amani hayakufika huko; ni karibu km 80 toka wilayani.
Kikao cha bodi ya shule kilichokaa jana, kimeamua kuifunga shule kwa muda usiojulikana. Wanafunzi wote wameelekea makwao; shida sasa inabaki kwa wazazi -walilipa karo mwezi january wengine kwa kuuza sehemu ya mashamba au mifugo nk, leo shule inafungwa; uwezo wa kutafuta shule nyingine haupo - shida sana!
 
Maandamano ya amani hayakufika huko; ni karibu km 80 toka wilayani.
Kikao cha bodi ya shule kilichokaa jana, kimeamua kuifunga shule kwa muda usiojulikana. Wanafunzi wote wameelekea makwao; shida sasa inabaki kwa wazazi -walilipa karo mwezi january wengine kwa kuuza sehemu ya mashamba au mifugo nk, leo shule inafungwa; uwezo wa kutafuta shule nyingine haupo - shida sana!

pole sana! Migomo yakuaribu mali ilisha pitwa na wakati.
 
Hivi hii shule imegeuzwa seminari au?make wanafunzi wanadai shule imeshikiliwa na mapadre. dah sijui na huo ni uchakachuaji!
 
Back
Top Bottom