nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
BAADHI ya wananchi wa Jimbo la Kahama wamemuangukia Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, kufika jimboni kwao ili ajionee kero na changamoto za kimaisha zinazowakabili.
Wananchi hao wamedai kuwa wamefikia hatua hiyo baada ya kubaini mbunge waliomchagua ameendekeza malumbano ya kisiasa yasiyo na tija kwa maendeleo ya wilaya yao.
Wakieleza sababu za kumhitaji Zitto wananchi hao wakiongozwa na wazee kwa nyakati tofauti walisema wanatambua uchapakazi wa mbunge huyo unaolenga maslahi ya taifa, tofauti na Mbunge wa Jimbo lao James Lembeli, waliodai kuwa ameishajipambanua kuwa hana muda wa kushughulikia matatizo yao zaidi ya kujiingiza katika malumbano ya kisiasa na viongozi wake wa Chama Cha Mapinduzi.
Walisema kuwa wanasikitishwa na Mbunge wao Lembeli ambaye anatambua fika kuwa msimu huu wa kilimo kuna hatari ya wapiga kura wake kukabiliwa na janga la njaa kutokana na baadhi ya maeneo mbalimbali katika jimbo lake kukabiliwa na upungufu mkubwa wa mvua ilihali mbunge wao akishindwa kuchukua hatua stahiki.
" Tunashangaa toka miaka mitano iliyopita kwa mbunge wetu kukalia mambo haya haya haya ya marumbano huku wananchi wa jimbo lake tukikabiliwa na changamoto nyingi za maendeleo zikiwemo barabara mbovu, huduma za msingi za kijamii haziridhishi katika maeneo mbalimbali ya jimbo hili; sasa sijui tukimbilie kwa nani? Labda kwa Zitto Kabwe aliyeonyesha uzalendo kwa kujali maslahi ya Buzwagi," alisema.
Walizitaja changamoto nyingine zinazowakabili ikiwamo wakulima kupatiwa pembejeo za ruzuku zisizo na ubora ambazo pia haziwafikii kwa wakati.
Hali kadhalika mzozo wa bei ya tumbaku ambayo licha ya uzalishaji kuwa mkubwa lakini makampuni yamegoma kununua zao hilo kwa bei ya msimu uliopita tena yakisisitiza kutonunua kiwango cha uzalishaji uliofikiwa msimu huu.
Pia wananchi hao wamelalamikia tatizo la ajira katika mgodi wa Buzwagi. Kwa upande wa elimu, wamelalamika baaadhi ya walimu wa sekondari za kata katika jimbo hilo ambao waliajiriwa Januari 31 mwaka huu kutolipwa posho za kujikimu pamoja na nauli zao huku wakicheleweshewa mishahara yao, hali ambayo inawafanya maisha yao katika shule wanazofundisha vijijini kuwa magumu.
Walisema badala ya mbunge huyo kushughulikia kero hizo amekalia malumbano ambayo hayasaidii kuleta maendeleo katika Jimbo la Kahama na ustawi wa taifa zima.
Wananchi hao wamedai kuwa wamefikia hatua hiyo baada ya kubaini mbunge waliomchagua ameendekeza malumbano ya kisiasa yasiyo na tija kwa maendeleo ya wilaya yao.
Wakieleza sababu za kumhitaji Zitto wananchi hao wakiongozwa na wazee kwa nyakati tofauti walisema wanatambua uchapakazi wa mbunge huyo unaolenga maslahi ya taifa, tofauti na Mbunge wa Jimbo lao James Lembeli, waliodai kuwa ameishajipambanua kuwa hana muda wa kushughulikia matatizo yao zaidi ya kujiingiza katika malumbano ya kisiasa na viongozi wake wa Chama Cha Mapinduzi.
Walisema kuwa wanasikitishwa na Mbunge wao Lembeli ambaye anatambua fika kuwa msimu huu wa kilimo kuna hatari ya wapiga kura wake kukabiliwa na janga la njaa kutokana na baadhi ya maeneo mbalimbali katika jimbo lake kukabiliwa na upungufu mkubwa wa mvua ilihali mbunge wao akishindwa kuchukua hatua stahiki.
" Tunashangaa toka miaka mitano iliyopita kwa mbunge wetu kukalia mambo haya haya haya ya marumbano huku wananchi wa jimbo lake tukikabiliwa na changamoto nyingi za maendeleo zikiwemo barabara mbovu, huduma za msingi za kijamii haziridhishi katika maeneo mbalimbali ya jimbo hili; sasa sijui tukimbilie kwa nani? Labda kwa Zitto Kabwe aliyeonyesha uzalendo kwa kujali maslahi ya Buzwagi," alisema.
Walizitaja changamoto nyingine zinazowakabili ikiwamo wakulima kupatiwa pembejeo za ruzuku zisizo na ubora ambazo pia haziwafikii kwa wakati.
Hali kadhalika mzozo wa bei ya tumbaku ambayo licha ya uzalishaji kuwa mkubwa lakini makampuni yamegoma kununua zao hilo kwa bei ya msimu uliopita tena yakisisitiza kutonunua kiwango cha uzalishaji uliofikiwa msimu huu.
Pia wananchi hao wamelalamikia tatizo la ajira katika mgodi wa Buzwagi. Kwa upande wa elimu, wamelalamika baaadhi ya walimu wa sekondari za kata katika jimbo hilo ambao waliajiriwa Januari 31 mwaka huu kutolipwa posho za kujikimu pamoja na nauli zao huku wakicheleweshewa mishahara yao, hali ambayo inawafanya maisha yao katika shule wanazofundisha vijijini kuwa magumu.
Walisema badala ya mbunge huyo kushughulikia kero hizo amekalia malumbano ambayo hayasaidii kuleta maendeleo katika Jimbo la Kahama na ustawi wa taifa zima.