Anonymous Caller
JF-Expert Member
- Sep 8, 2016
- 1,220
- 1,632
Asante mwalimu kwa ufafanuzi.Nimeona mjadala watu wakilalamika kuhusiana na yusuph kagoma kwamba kiungo chake ni outdated na kwamba anacheza kizamani tuangalie kwanza aina za DM halafu tuwekane sawa
Defensive midfielder(DM)Huyu ni ni kiungo mkabaji ambaye majukumu yake purely ni majukumu ya ulinzi ambapo anasaidia kulinda backline,kuintercept passes,kuvunja counter attacks,kuretain possession na kusambaza mipira kutokea chini
Sasa huyu DM wamegawanyika kuna
1 Destroyer au ball winning midfielder
2 deep lying playmaker wengine wanawaita regista
3 anchor man midfielder
1 Tukianza na destroyer hapa huyu focus yake ni kuwin mpira anaweza asiwe passer mzuri lakini sifa zake kuu anakua aggressive/mkatili mvunja kuni na hana mambo mengi
mfano hapa kuna fabinho,casemiro,gattuso kibongo bongo
Alikuwepo taddeo lwanga,zawadi mauya,hata kanoute kipindi anacheza no 6 na currently namuona kagoma akiwa ni aina hii ya DM
2 deep lying playmaker/regista
Huyu anaamua tempo ya mchezo anatakiwa kua na high passing accuracy long balls,tactical na Kubwa awe na vision hawa sio wakatili sana wanalenga zaidi kuchezesha timu kutokea chini
Mfano utamkuta busquet,jorginho au pirlo,kimmich
Kwa bongo aucho,bitegeko hata huyu okejepha wanaweza kua regista wazuri
3 anchor man midfielder
Huyu anakua Mara nyingi yupo chini analinda ukuta na hawatoki sana nje ya eneo lao Mara nyingi wanakua na discipline nzuri na tactical awareness
Mfano wao hapa ni nemanja matic
Sasa kila kocha kulingana na mfumo wake anakua anaprefer aina Fulani ya DM mfano klop alikua anapenda zaidi wakata kuni kuna mourinho,Deschamps na etc
Taifa stars chan ukiangalia kocha anaprefer zaidi destroyer kagoma ambaye mbele yake anasimama mudathir kama deep lying au sometimes box to box kwahiyo binafsi naona kagoma yupo sahihi labda tu ni vile anacheza rafu ambazo zinazidi Ila ukiachana na hiyo kagoma ni kiungo ambaye ningechagua kwenda naye binafsi anaprefer zaidi viungo no 6 wakatili,wagumu
Karibuni
Sasa nina maswali.
1. Kiungo Himid Mao anaingia kwenye sifa zipi kati ya ulizotaja.....kwasabu wengi huwa hatuoni anachokifanya uwanjani...in short hana mvuto kabisa....lakini nimemfuatilia kule Misiri anaaminiwa sana..kila club inayoenda ni lazima aanziswe panga pangua..amecheza club 4 kule.
2. Yupo kiungo mwingine mkameruni pale Napoli anaitwa Frank Zambo Anguissa..huyu nae walimu huwa wanampenda sana..yupo kwny kundi lipi.
3. Kuna mchambuzi mmoja niliwahi kumsikiliza redioni anasema Viungo wakabaji wenye kimo cha wastani au kifupi wanafanya vizuri zaidi majukumu yao kuliko viungo wakabaji warefu....kwasababu ya quick mobility....huku akimtolea mfano Kante.
Je msingi huo unakubaliana naye?
Na kama ndiyo. huoni urefu wa viungo wa chini warefu kama kagoma, Ngoma, au kanoute ni wa aina moja ileile.