Boniphace Kichonge
JF-Expert Member
- Jul 31, 2017
- 1,605
- 1,956
NOVEMBA 9, 2019
Raisi wa Rwanda Paul Kagame amejibu shutuma kuwa amekuwa akiwapeleleza wapinzani wake kupitia simu zao, amesema teknolojia inayohitajika kufanya hivyo ni ghali sana.
Akizungumza na waandishi wa habari katika mji mkuu wa Rwanda, Kigali siku ya Ijumaa, raisi Kagame amesema anatamani angekuwa na uwezo wa kununua teknolojia hiyo ''kujua zaidi'' kuhusu adui zake.
Raia wa Rwanda anayeishi nchini Uingereza aliiambia BBC juma lililopita kuwa anaamini kuwa alikuwa muathiriwa wa udukuzi uliofanyika kwa WhatsApp.
Faustine Rukundo alisema yeye na wafuasi wenzake wa chama cha Rwanda National Congress- kundi linaloipinga serikali ya Rwanda walikuwa wanalengwa kwa kutumia huduma za ujumbe.
Maabara ya Citizen, kundi la utafiti katika Chuo Kikuu cha Toronto, imethibitisha kuwa alikuwa anafuatiliwa.
WhatsApp imeishutumu Kampuni ya NSO Group kwa kuweka programu kwenye simu karibu 1,400 kwa nia ya kufanya upelelezi. Programu yake ya Pegasus inaweza kufanya kazi hiyo hata ikiwa mbali.
Idadi kubwa ya watu wanaofuatiliwa wanadaiwa kuwa raia wa Rwanda.
Kampuni ya NSO Group imekana madai dhidi yao, ikisema kuwa programu ya Pegasus imekuwa ikiuzwa kwa wateja waliohakikiwa na si wenye nia mbaya.
BBC
Raisi wa Rwanda Paul Kagame amejibu shutuma kuwa amekuwa akiwapeleleza wapinzani wake kupitia simu zao, amesema teknolojia inayohitajika kufanya hivyo ni ghali sana.
Akizungumza na waandishi wa habari katika mji mkuu wa Rwanda, Kigali siku ya Ijumaa, raisi Kagame amesema anatamani angekuwa na uwezo wa kununua teknolojia hiyo ''kujua zaidi'' kuhusu adui zake.
Raia wa Rwanda anayeishi nchini Uingereza aliiambia BBC juma lililopita kuwa anaamini kuwa alikuwa muathiriwa wa udukuzi uliofanyika kwa WhatsApp.
Faustine Rukundo alisema yeye na wafuasi wenzake wa chama cha Rwanda National Congress- kundi linaloipinga serikali ya Rwanda walikuwa wanalengwa kwa kutumia huduma za ujumbe.
Maabara ya Citizen, kundi la utafiti katika Chuo Kikuu cha Toronto, imethibitisha kuwa alikuwa anafuatiliwa.
WhatsApp imeishutumu Kampuni ya NSO Group kwa kuweka programu kwenye simu karibu 1,400 kwa nia ya kufanya upelelezi. Programu yake ya Pegasus inaweza kufanya kazi hiyo hata ikiwa mbali.
Idadi kubwa ya watu wanaofuatiliwa wanadaiwa kuwa raia wa Rwanda.
Kampuni ya NSO Group imekana madai dhidi yao, ikisema kuwa programu ya Pegasus imekuwa ikiuzwa kwa wateja waliohakikiwa na si wenye nia mbaya.
BBC