Kafulila: Mwekezaji anayesambaza maji Jiji la Kigali Rwanda ameonesha nia ya kuwekeza kwa Ubia na Serikali ya Tanzania

Mwananchi Huru

JF-Expert Member
Nov 20, 2021
1,555
1,153

Mkurugenzi Mkuu wa PPP nchini Bw David Kafulila kupitia kipindi cha DK 45 kinachorushwa na runinga ya ITV ameeleza kuwa Mwekezaji aliyewekeza kwa Ubia na Serikali ya Paul Kagame ya Rwanda kwa thamani ya zaidi US$ 60M ameonesha nia ya kutaka kuwekeza katika Sekta hiyo ya maji hapa nchini.

Aidha, Mkurugenzi huyo Mkuu Bw David Kafulila amesema watakaa na kuangalia kama tunaweza kumpokea na kuingia nae mkataba ili asaidie kusambaza katika baadhi ya Majiji ili kuongeza kasi ya ushindani katika Usambazaji na utoaji wa maji na salama kwa wananchi wetu.
 
Nakumbuka wakati NBC inauzwa tena kwa bei chee sana nilimchukia sana Hayati Benjamini Mkapa.

Baada ya NBC kuuzwa ikazaliwa NMB,

NMB tena ikauzwa kwa Waholanzi wa Rabo bank,

Leo NMB ndio BANK kubwa Tanzania,

Leo NBC inaimarika na ndio mfadhili mkubwa wa NBC PREMIUM LEAGUE

UBIA NI MZURI, UNAPUNGUZA WIZI NA UJAMBAZI
 
Ina maana makusanyo yoote, na mapesa yote tunayokopa kila leo jumlisha na mali tulizonazo hapa bongo tumeshindwa hata usambazaji wa maji tu? Yaani mfano Mwanza hapo wamezungukwa na ziwa ila maji ni shida balaa, Bongo nyoso.
Tatizo Kila mmoja anaona huu ni mradi wa Serikali ndio maana,

Subiri waje wa Bia hapo Mwanza utaona kama utakutana tena na shida ya maki
 
Ina maana makusanyo yoote, na mapesa yote tunayokopa kila leo jumlisha na mali tulizonazo hapa bongo tumeshindwa hata usambazaji wa maji tu? Yaani mfano Mwanza hapo wamezungukwa na ziwa ila maji ni shida balaa, Bongo nyoso.
Shida sio makusanyo shida ni kuongeza tija ya Wananchi kupata maji safi, salama na ya uhakika.
 
Kwahiyo huyo Mbia atakuja kuparner na mamlaka ipi hapa kwetu?
Si kweli kuwa mamlaka zote za maji hapa kwetu zinafanya Vibaya zipo ambazo zipo vizuri.
Na mamlaka zenye Changamoto ya operation hata huyo mbia hatoziweza kama experience pekee aliyonayo ni Rwanda.
 
Unaweza elezea ni kivipi nmb ni nbc?
NBC baada ya kuingia Ubia na Rabo zile NBC za vijijini zilikataliwa na Mbia ndio chanzo Cha NMB kuanzishwa na serikali,

Baadae ikakua Rabo tena wakainunua NMB,

NMB ndio hiii unaiona Leo,

NMB NI MATOKEO YA UBIA.
 
Kwahiyo huyo Mbia atakuja kuparner na mamlaka ipi hapa kwetu?
Si kweli kuwa mamlaka zote za maji hapa kwetu zinafanya Vibaya zipo ambazo zipo vizuri.
Na mamlaka zenye Changamoto ya operation hata huyo mbia hatoziweza kama experience pekee aliyonayo ni Rwanda.
Watafanya kazi kwa Ubia,
 
View attachment 2992532

Mkurugenzi Mkuu wa PPP nchini Bw David Kafulila kupitia kipindi Cha DK 45 kinachorushwa na runinga ya ITV ameeleza kuwa,

Mwekezaji aliyewekeza kwa Ubia na Serikali ya Paul Kagame ya Rwanda kwa thamani ya zaidi US$ 60M ameonesha nia ya kutaka kuwekeza katika Sekta hiyo ya maji hapa nchini.

Aidha, Mkurugenzi huyo Mkuu Bw David Kafulila amesema watakaa na kuangalia kama tunaweza kumpokea na kuingia nae mkataba ili asaidie kusambaza katika baadhi ya Majiji ili kuongeza kasi ya ushindani katika Usambazaji na utoaji wa maji na salama kwa wananchi wetu.

Mimi sio CCM ila huwa namkubali sana Kafulila na Zitto
 
Back
Top Bottom