nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[h=2][/h]JUMAMOSI, SEPTEMBA 08, 2012 08:48 NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM
MAHAKAMA Kuu, Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali ombi dogo la pingamizi la kesi ya msingi ya kupinga kuvuliwa uanachama wa NCCR-Mageuzi, lililowasilishwa mahakamani hapo na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila.
Kwa mujibu wa Mwanasheria wa NCCR-Mageuzi, Mohamed Tibanyendera, ombi hilo dogo lilikataliwa jana mahakamani hapo, baada ya kasoro za kisheria kubainika katika hati ya kiapo cha Kafulila alichokiwasilisha katika mahakama hiyo.
Tibanyendera alisema kwamba, kesi hiyo namba 218 ya mwaka 2011 inayosikilizwa na Jaji Alice Chinguwile, pamoja na kukataliwa kwa ombi hilo la Kafulila, shauri hilo liliaihirishwa hadi Novemba 22, mwaka huu.
Alisema kesi ya msingi ya pingamizi lililopelekwa mahakamani hapo na Kafulila, akipinga kuvuliwa uanachama kupitia kikao cha dharula cha Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho, haijaanza kusikilizwa.
Kwa upande wake, Kafulila, alipoulizwa na MTANZANIA ili kupata maoni yake, alisema hana taarifa za ombi hilo dogo kutupwa na mahakama hiyo kwa sababu, hakuwapo mahakamani hapo na wala hajui kama kesi hiyo ilisikilizwa jana.
Hata hivyo, alisema atawasiliana na wakili wake kisha atatoa taarifa za kilichoendelea mahakamani hapo.
Kafulila na wajumbe wengine sita akiwamo aliyekuwa mgombea urais wa chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, Hashim Rungwe, walivuliwa uanachama wa NCCR-Mageuzi Desemba mwaka jana.
Kafulila, Rungwe na wenzao walivuliwa uanachama baada ya wajumbe wa NEC kudaiwa kutoridhishwa na mwenendo wao kisiasa.
Wakati wanachama hao wa chama hicho cha upinzani wakivuliwa uanachama, kulikuwa na taarifa za kutokea kwa vurugu, ambapo askari polisi walifika eneo uliokuwa ukifanyika mkutano, Kinondoni Dar es Salaam na kukuta hali ni tulivu.
Wakati Kafulila na wenzake hao wakifutiwa uanachama, Mbunge wa Muhambwe, Felix Mkosamali kupitia chama hicho, alipewa onyo kali baada ya wajumbe hao kuonyesha kutoridhishwa na mwenendo wake kisiasa.
MAHAKAMA Kuu, Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali ombi dogo la pingamizi la kesi ya msingi ya kupinga kuvuliwa uanachama wa NCCR-Mageuzi, lililowasilishwa mahakamani hapo na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila.
Kwa mujibu wa Mwanasheria wa NCCR-Mageuzi, Mohamed Tibanyendera, ombi hilo dogo lilikataliwa jana mahakamani hapo, baada ya kasoro za kisheria kubainika katika hati ya kiapo cha Kafulila alichokiwasilisha katika mahakama hiyo.
Tibanyendera alisema kwamba, kesi hiyo namba 218 ya mwaka 2011 inayosikilizwa na Jaji Alice Chinguwile, pamoja na kukataliwa kwa ombi hilo la Kafulila, shauri hilo liliaihirishwa hadi Novemba 22, mwaka huu.
Alisema kesi ya msingi ya pingamizi lililopelekwa mahakamani hapo na Kafulila, akipinga kuvuliwa uanachama kupitia kikao cha dharula cha Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho, haijaanza kusikilizwa.
Kwa upande wake, Kafulila, alipoulizwa na MTANZANIA ili kupata maoni yake, alisema hana taarifa za ombi hilo dogo kutupwa na mahakama hiyo kwa sababu, hakuwapo mahakamani hapo na wala hajui kama kesi hiyo ilisikilizwa jana.
Hata hivyo, alisema atawasiliana na wakili wake kisha atatoa taarifa za kilichoendelea mahakamani hapo.
Kafulila na wajumbe wengine sita akiwamo aliyekuwa mgombea urais wa chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, Hashim Rungwe, walivuliwa uanachama wa NCCR-Mageuzi Desemba mwaka jana.
Kafulila, Rungwe na wenzao walivuliwa uanachama baada ya wajumbe wa NEC kudaiwa kutoridhishwa na mwenendo wao kisiasa.
Wakati wanachama hao wa chama hicho cha upinzani wakivuliwa uanachama, kulikuwa na taarifa za kutokea kwa vurugu, ambapo askari polisi walifika eneo uliokuwa ukifanyika mkutano, Kinondoni Dar es Salaam na kukuta hali ni tulivu.
Wakati Kafulila na wenzake hao wakifutiwa uanachama, Mbunge wa Muhambwe, Felix Mkosamali kupitia chama hicho, alipewa onyo kali baada ya wajumbe hao kuonyesha kutoridhishwa na mwenendo wake kisiasa.