Kadiri unavyoukimbia mwangwi ndivyo unavyoukaribia

Kadiri unavyoukimbia mwangwi ndivyo unavyoukaribia

Nakumbuka miaka ya nyuma "Ila sio zamani kwa maana zamani Mimi sikuwepo; tulikuwa Mimi na marafiki zangu tunaingia ndani ya maghorofa ya kale (Magofu)ndio tunasikiliza Mangwi. Ukishaingia ndani ndio unapiga Ukwenje mkali sana, ile ukimaliza tu ndio unasikia sauti yako inajirudia vilevile ulivyotamka, basi tunatishana kuna Shetani humu!! Aisee Hizo mbio zinaazoanzishwa hapo asikwambie MTU kitu...
Utotoni tulifurahia sana tulipokuwa tunaenda mapangoni kusikiliza sauti zetu kupitia mwangwi mapangoni. Yaani Ilikuwa ni kama vile mapango yanatugeza sauti zetu na kutusikilizisha kwa sauti ya juu zaidi.

Siku hizi mapango yamepungua sana na mwangwi hakuna tena. Kuna wengine hapa wanaweza hata kushangaa mwangwi ni nini.

Tulienjoy sana tulipokuwa tukipiga ukunga wa uuuuuuuuuu. Na tunapoishia tu mwangwi nao unakupokea uuuuuuuuuu uuuuuuuuu. Mwangwi unaanzia mbaali unakuja karibu kabisa halafu unaishia hukooo unatokomomea kabisa.

Kuna mwangwi wa kifo ujue. Kadiri unavyoukimbia ndio unavyozidi kuukaribia Mwangwi asili yake ni wewe mwenyewe. Kuukimbia ni kujikimbia. Mwisho watu wataanza kukushangaa. Huyu anakimbia nini?

Unaweza kutoka kwako kwa hofu tu na kero ya mwangwi ukaenda kwa jirani ili usiusikie. Ukifika hapo unaukuta. Unaona hapa hapafai unaondoka tena unaenda nje ya mji upo. Unaona kero tena. Unahama mji bado mwangwi upo. Unaamua kwenda mbali.. Mwisho unamaliza miji na kuamua kuingia mwituni. Mwangwi haukimbiwi. Unaweza kuingia mwituni na usirudi. Mwituni kuna mengi.

Wataalamu wa madawa wanaweza kutusaidia kwenye hili. Ukitumia madawa makali kwa muda mrefu huleta athari kwenye mfumo wa fahamu. Mfumo wa fahamu ukiathirika huweza kuathiri hata uwezo wa mtu kwenye maamuzi hasa yale muhimu.

Tumejaaliwa kuwa na mgonjwa ghali zaidi duniani. Ambaye anaweza kuingia kwenye Guinness Book of Records. Lakini kwa anayofanya sasa nadhani anatafuta rekodi nyingine.

Halafu nimepita mahali watu wanapongezana. Huyu anasema kama sio mimi kusema hivi. Hali ingekuwa vile. Halafu yule mwingine anamshukuru. Mmoja ni mkubwa kuliko mwingine. Wanapongezana kuficha ukweli.

Tabia ya uvundo hauvundi mpaka unuke sana. Na kadiri unavyoufutika mchagoni ndio kadiri unavyotoa harufu kali. Ni kama pembe la ng'ombe -- HALIFICHIKI!

Jr
 
Utotoni tulifurahia sana tulipokuwa tunaenda mapangoni kusikiliza sauti zetu kupitia mwangwi mapangoni. Yaani Ilikuwa ni kama vile mapango yanatugeza sauti zetu na kutusikilizisha kwa sauti ya juu zaidi.

Siku hizi mapango yamepungua sana na mwangwi hakuna tena. Kuna wengine hapa wanaweza hata kushangaa mwangwi ni nini.

Tulienjoy sana tulipokuwa tukipiga ukunga wa uuuuuuuuuu. Na tunapoishia tu mwangwi nao unakupokea uuuuuuuuuu uuuuuuuuu. Mwangwi unaanzia mbaali unakuja karibu kabisa halafu unaishia hukooo unatokomomea kabisa.

Kuna mwangwi wa kifo ujue. Kadiri unavyoukimbia ndio unavyozidi kuukaribia Mwangwi asili yake ni wewe mwenyewe. Kuukimbia ni kujikimbia. Mwisho watu wataanza kukushangaa. Huyu anakimbia nini?

Unaweza kutoka kwako kwa hofu tu na kero ya mwangwi ukaenda kwa jirani ili usiusikie. Ukifika hapo unaukuta. Unaona hapa hapafai unaondoka tena unaenda nje ya mji upo. Unaona kero tena. Unahama mji bado mwangwi upo. Unaamua kwenda mbali.. Mwisho unamaliza miji na kuamua kuingia mwituni. Mwangwi haukimbiwi. Unaweza kuingia mwituni na usirudi. Mwituni kuna mengi.

Wataalamu wa madawa wanaweza kutusaidia kwenye hili. Ukitumia madawa makali kwa muda mrefu huleta athari kwenye mfumo wa fahamu. Mfumo wa fahamu ukiathirika huweza kuathiri hata uwezo wa mtu kwenye maamuzi hasa yale muhimu.

Tumejaaliwa kuwa na mgonjwa ghali zaidi duniani. Ambaye anaweza kuingia kwenye Guinness Book of Records. Lakini kwa anayofanya sasa nadhani anatafuta rekodi nyingine.

Halafu nimepita mahali watu wanapongezana. Huyu anasema kama sio mimi kusema hivi. Hali ingekuwa vile. Halafu yule mwingine anamshukuru. Mmoja ni mkubwa kuliko mwingine. Wanapongezana kuficha ukweli.

Tabia ya uvundo hauvundi mpaka unuke sana. Na kadiri unavyoufutika mchagoni ndio kadiri unavyotoa harufu kali. Ni kama pembe la ng'ombe -- HALIFICHIKI!

Jr
Aha ha ha nani huyo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Tabia ya uvundo hauvundi mpaka unuke sana. Na kadiri unavyoufutika mchagoni ndio kadiri unavyotoa harufu kali"
 
Nahisi wajeda wajeda wanatulia timing
Karibu tutafanya UTurn
Imeisha iyo
IMG-20210315-WA0085.jpg
 
Gharama za matibabu ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, nchini India kwa kipindi cha miezi mitano kufuru!

Kwa uchambuzi wa ripoti ya CAG, Bw. Job Ndugai alikaa India kwa miezi mitano, sawa na siku 150. Kwa siku moja alilipwa posho ya dola 500 sawa na Sh. 1,160,100.00, na hivyo kwa miezi mitano alilipwa dola 75,000 sawa na Sh. 174,015,000.00.

Akiwa India alikuwa na wasaidizi wawili – maana alihamishia ofisi yake huko huko hotelini. Kwa gharama ya dola 450 sawa na Sh. 1,044,090.00 kila moja kwa siku, walilipwa dola 900 sawa na Sh. 2,088,180.00 kwa siku. Kwa siku 150 walizokaa India, walilipwa dola 135,000 sawa na Sh. 292,950,000.

Kwa ujumla, matibabu ya Ndugai kwa miezi mitano huko India yalitumia posho za sh. 466,965,000. na hapo bado gharama za hospitali huko India, na tiketi za ndege kwa watu wote hao, na bado gharama alizokuwa anatumia mkewe.

Takwimu hizi zilikuwa ni kwa mujibu wa ukaguzi wa CAG katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika hospitali za India.

Wakati huo huo tusisahau kuwa Bw. Job Ndugai aliendelea kupata mshahara wake na posho zake kama Spika wa Bunge ambazo idadi yake naomba kama kuna watu humu wanazijua watusaidie kuzitoa.

Hakuna anayejua kwa uhakika Bw. Job Ndugai alikuwa anaumwa ugonjwa gani uliosababisha hadi ofisi yake ihamishiwe 5-star hotel nchini India ambako alichukua VIP suite nzima. Mpaka sasa gharama za matibabu yake ni siri kama ulivyo ugonjwa wake.

Ana apartments 78 dodoma,ivi CAG huku hafiki??

Mungu tupe nguvu....

Veronica France
 
Utotoni tulifurahia sana tulipokuwa tunaenda mapangoni kusikiliza sauti zetu kupitia mwangwi mapangoni. Yaani Ilikuwa ni kama vile mapango yanatugeza sauti zetu na kutusikilizisha kwa sauti ya juu zaidi.

Siku hizi mapango yamepungua sana na mwangwi hakuna tena. Kuna wengine hapa wanaweza hata kushangaa mwangwi ni nini.

Tulienjoy sana tulipokuwa tukipiga ukunga wa uuuuuuuuuu. Na tunapoishia tu mwangwi nao unakupokea uuuuuuuuuu uuuuuuuuu. Mwangwi unaanzia mbaali unakuja karibu kabisa halafu unaishia hukooo unatokomomea kabisa.

Kuna mwangwi wa kifo ujue. Kadiri unavyoukimbia ndio unavyozidi kuukaribia Mwangwi asili yake ni wewe mwenyewe. Kuukimbia ni kujikimbia. Mwisho watu wataanza kukushangaa. Huyu anakimbia nini?

Unaweza kutoka kwako kwa hofu tu na kero ya mwangwi ukaenda kwa jirani ili usiusikie. Ukifika hapo unaukuta. Unaona hapa hapafai unaondoka tena unaenda nje ya mji upo. Unaona kero tena. Unahama mji bado mwangwi upo. Unaamua kwenda mbali.. Mwisho unamaliza miji na kuamua kuingia mwituni. Mwangwi haukimbiwi. Unaweza kuingia mwituni na usirudi. Mwituni kuna mengi.

Wataalamu wa madawa wanaweza kutusaidia kwenye hili. Ukitumia madawa makali kwa muda mrefu huleta athari kwenye mfumo wa fahamu. Mfumo wa fahamu ukiathirika huweza kuathiri hata uwezo wa mtu kwenye maamuzi hasa yale muhimu.

Tumejaaliwa kuwa na mgonjwa ghali zaidi duniani. Ambaye anaweza kuingia kwenye Guinness Book of Records. Lakini kwa anayofanya sasa nadhani anatafuta rekodi nyingine.

Halafu nimepita mahali watu wanapongezana. Huyu anasema kama sio mimi kusema hivi. Hali ingekuwa vile. Halafu yule mwingine anamshukuru. Mmoja ni mkubwa kuliko mwingine. Wanapongezana kuficha ukweli.

Tabia ya uvundo hauvundi mpaka unuke sana. Na kadiri unavyoufutika mchagoni ndio kadiri unavyotoa harufu kali. Ni kama pembe la ng'ombe -- HALIFICHIKI!

Jr
mmmh hii kali
 
Back
Top Bottom