peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 12,799
- 21,370
Kampuni ya uendelezaji na uendeshaji wa Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KADCO) imetoa gawio la Sh2.9 bilioni kwa Serikali kwa mwaka 2016 hadi 2019.
Hayo yameelezwa leo Oktoba 11, 2022 na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Christine Mwakatobe wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa bajeti na mwelekeo wa Kampuni hiyo kwa mwaka wa Fedha 2022/23.
Christine amesema mchanganuo wa gawio hilo ni kwa mwaka 2016/17 Kampuni ilitoa zaidi ya Sh555 milioni, mwaka 2017/18 ilitoa zaidi ya Sh583 milioni, mwaka 2018/19 ilitoa Sh1 bilioni na mwaka 2019/20 ilitoa Sh850 milioni.
Aidha amesema sambamba na gawio hilo Kampuni hiyo imelipa kodi ya Sh6.1 bilioni katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2020.
"Kiasi hicho kimelipwa kama kodi kwa Serikali kuu lakini kuna Sh541 milioni ambayo imelipwa kama kodi kwa Mamlaka ya Serikali za mitaa na Halmashauri ambapo kiwanja chetu kinapatikana," amesema.
Akizungumzia kuhusu mkakati wa Kampuni hiyo amesema ni kuongeza idadi ya abiria na kukarabati eneo la uwanja ili kuchukua magari 200 kutoka magari 83 yanayoweza kuchukuliwa kwa sasa kwenye uwanja huo.
“Mpaka sasa mkataba wa ukarabati wa ujenzi huu umeshasainiwa na hivi karibuni ujenzi utaanza na utagharimu Sh2.7 bilioni”amesema.
Chanzo: Mwananchi
Hayo yameelezwa leo Oktoba 11, 2022 na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Christine Mwakatobe wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa bajeti na mwelekeo wa Kampuni hiyo kwa mwaka wa Fedha 2022/23.
Christine amesema mchanganuo wa gawio hilo ni kwa mwaka 2016/17 Kampuni ilitoa zaidi ya Sh555 milioni, mwaka 2017/18 ilitoa zaidi ya Sh583 milioni, mwaka 2018/19 ilitoa Sh1 bilioni na mwaka 2019/20 ilitoa Sh850 milioni.
Aidha amesema sambamba na gawio hilo Kampuni hiyo imelipa kodi ya Sh6.1 bilioni katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2020.
"Kiasi hicho kimelipwa kama kodi kwa Serikali kuu lakini kuna Sh541 milioni ambayo imelipwa kama kodi kwa Mamlaka ya Serikali za mitaa na Halmashauri ambapo kiwanja chetu kinapatikana," amesema.
Akizungumzia kuhusu mkakati wa Kampuni hiyo amesema ni kuongeza idadi ya abiria na kukarabati eneo la uwanja ili kuchukua magari 200 kutoka magari 83 yanayoweza kuchukuliwa kwa sasa kwenye uwanja huo.
“Mpaka sasa mkataba wa ukarabati wa ujenzi huu umeshasainiwa na hivi karibuni ujenzi utaanza na utagharimu Sh2.7 bilioni”amesema.
Chanzo: Mwananchi