Kada wa CHADEMA kuiaga SAUT leo


kweli si wote wanaosoma wanaondokana na ujinga...Kwani kukosoa SERIKALI ni vibaya ..

Jifunze hili .Serikali siyo mbaya ila watendaji wake baba ee.!!!!
 
Kitima ni kiongozi wa mfano.

1. Alifanikiwa kuendesha chuo kwa ada ndogo kuliko vyuo vikuu vyote (vikiwemo vya serikali) huku akilipa mishahara mikubwa kuliko vyuo vyote. Ikumbukwe kuwa kwa vyuo vya serikali ada za wanafunzi hazitumiki kulipa mishahara (mishahara hulipwa toka Hazina), wala hazitumiki kukarabati na kujenga majengo. Kitima ameweza kutumia ada za wanafunzi hizo hizo kuendesha chuo, kulipa mishahara, kukarabati na kujenga (40% kwa kuongezea misaada).

2. Kitima hakuwa na makuu, na hakutumia mali za chuo ovyo. Tangu amekuwa VC amekuwa anatumia gari yake mwenyewe. Alianza na Toyota Hilux Surf. Anapewa na chuo lita 50 za dizeli kwa wiki na zinamtosha kwa matumizi ya gari la VC. Simu pia ana fungu maalum na hazidishi, zinazozidi anatumia mshahara wake.

3. Kitima amekuwa mtetezi sana wa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote tu Tanzania hasa kwa mambo ya mikopo. Wanaojua hili watamkumbuka sana bila kujali walisoma chuo gani. Kauli nyingi kali dhidi ya serikali amezitoa akitetea watoto wa maskini.

4. Kitima ana msimamo na hayumbishwi hata na Rais. Wakati wa uchaguzi mwaka 2010 Rais alitoa amri kwa vyuo vikuu kutofungua kabla ya uchaguzi. Iwapo Kitima angetii, chuo chake kingepata hasara ya zaidi ya TSh. Billioni mbili kwa kulipa gharama bila ku operate. Kitima aliamua kufungua tu chuo na akaokoa hizo Billioni mbili za chuo.

na mengine mengi....
 
Fr.Pius Mgeni Masikini...mtu makini na mweledi,mpole na mwenye busara...mwalimu mzuri sana!sikuwa najua kama ndo atakuwa mkuu wa SAUT....Ana mapungufu yake kama binadamu,lakini amestahili...ngoja nitafute picha ya kumbukumbu yetu miaka hiyo!Jitu makini sana
 
Unadhani wewe umekombolewa?bora mimi kuliko wewe unaewaza kwenda kugombea kwenu uibe hata kilichobaki kwa mgongo huu huu wa kuwasaidia wanyonge,tumeona wengi waliosema hivyo,Lissu,Wenje,Kiwia,Msigwa,n.k ambao hadi leo hakuna walichofanya zaidi ya kuwanunulia maskini viroba wakazomee ccm na kufanya fujo,so wewe ndo bado hujakombolewa,wezi nyie,mmetapeli M4C mnadhani hatuoni?mjinga wewe.
 
Nina mashaka na uwezo wako wa kung'amua mabo,sina shaka kuwa wewe ni juaji na ni type ya wezi ambao hawajapata nafasi ya kuiba sasa wanaitaka kwa nguvu zote hata kwa kumwaga damu,weka hoja hapa nini nikufafanulie,mtaji wa siasa ni maneno na facts,twende,cdm mmefanya nn hadi sasa kwa hivyo viti vichache tulivyowapa bungeni?
 
Nina mashaka na uwezo wako wa kung'amua mambo,sina shaka kuwa wewe ni juaji na ni type ya wezi ambao hawajapata nafasi ya kuiba sasa wanaitaka kwa nguvu zote hata kwa kumwaga damu,weka hoja hapa nini nikufafanulie,mtaji wa siasa ni maneno na facts,twende,cdm mmefanya nn hadi sasa kwa hivyo viti vichache tulivyowapa bungeni?
 
mgeni ni mwadilifu ataweza kuleta mapinduzi makubwa pale saut namjua ni mtu anayefaa.
 
Kama nilivyowajibu wenzako,naona pia na wewe upo mlengo wa watenda maovu ambao hata wakiona uzuri wao huuhesabu kama ubaya,sasa wakikuta mtu asiye na uwezo wa kupangua hoja na kuumbua hali yao ya kupindisha ukweli na kujihami huchukua point 3 muhimu,ila ujumbe umefika.
 
Habari ilitakiwa kuwa" Makamu Mkuu wa chuo-SAUT amestaafu" lakini kwa kuwa siku hizi bila kutaja CHADEMA baadhi yenu hamshindi wala kulala basi umeona ni vema Rev.Dr.Charles Kitima umuite kada ya CHADEMA. Kumbuka makada wapo CCM na siyo CHADEMA, najua viongozi wengi wa chama tawala wanamchukia kwa kuwa anaikosoa serikali na kusimamia ukweli anaoamini.Sijawahi kushuhudia makamu mkuu wa chuo chochote Tanzania akiwatetea wananchi wake atokako lakini nimemshuhudia mara kadhaa makamu mkuu wa chuo cha SAUT akiwatetea hadi walima alizeti wa Singida dhidi ya sera mbovu za CCM zisizowainua wakulima. Nimjuavyo Dr.Kitima ni mpenda mabadiliko, miaka ya nyuma viongozi wa serikali za wanafunzi walikuwa mapandikizi wa CCM (Rejea TAHLISO ya 2010 walipoungana na CCM TBC kupinga wanachuo kupiga kura popote) lakini Dr.Kitima aliamuru chuo kifunguliwe mapema ili waliojiandikisha chuoni wapige kura.Pia alishirikiana vizuri na SAUTSO licha ya kuwa mikononi mwa Pro-CHADEMA.
 

You are very true with the Catholic Priest,well said Man
 

Ulikuwa na hoja lakini unakoelekea sasa unakosea.Huwezi kuona kazi ya mbunge mmoja wa Chadema na wabunge 10 wa CCM walivyotofauti?Kama Chadema isingekuwa inabweka kila mara basi mali zetu watanzania zingeliwa bila kificho japo bado zinaliwa licha ya Chadema kupiga kelele.Jaribu kusimamia hoja uliyoleta.Kwanza mimi kama niliyepita hapo Nyegezi na nikamwona Padre Kitima najua kazi yake ilivyo nzuri.Lakini la ziada ni kuwa hakuna sheria inayomkataza Padre kuwa mwanachama wa chama cha siasa.Elewa hilo
 

Muda uliojiunga hapa pengine ungetumia kujifunza zaidi kuliko kutaka kubishana na watu hapa jamvini.Inaonekana kuna mtu alikulazimisha kujiunga JF.Huyo kakudanganya.Huwezi kuingia nyumbani kwa mtu na kuanza kutukana watoto wa mwenye nyumba
 
hivi kuna padri wa kikatoliki ambaye si Chadema kweli?

 
ndio maana maaana hata kabla hamjapondwa mshalia,kisa watoto wa mwenye nyuma,sasa huyo mwenye nyumba ni nani?
 
Na bado, wembe ni huo huo, mtu kaajiriwa SAUT, badala ya kufanya yaliyopo kwenye job description yake anakomaa na kuikashfu serikali..! Hilo ni onyo kwa wasumbufu wa aina yake..!
 
labda useme anautetea UKATOLIKI na si wananchi, nani asiyemjua huyu mzee alivyo na chuki dhidi ya uislam wala hafichi.

 
Kada lazima amiliki kadi ya chama otherwiz ni mshabiki tuu...na hapa unabisha tuu hauna proof kuwa jamaa ni cdm...me najua jamaa ni tlp na alishawahi kudiclare na
 
je,cuf,wahariri na wabunge particularly wa ccm na watetezi wa haki za binadam nao ni wana m4c?
Hapa ndo tunakuja kuamini kuwa m4c ni chama makin,cha wanyonge,ukweli na uhakika tukiunge mkono vilivyo.

kukosoa na kusema maovu yanafanywa na ccm sio lazima uwe mwanachama wa chadema. acha ukada wa chama. unajua haya pesa EPA. Kashfa ya Richmund, twiga kupelekwa urabuni, mgodi wa kiwira na maisha magumu kwa sasa ni wewe kada wa ccm unasima ni poa tu. wewe na unaiifaidi keki ya taifa ndiyo maana unaisifia serikali ya magamba.ujue yana mwisho.
 
je,cuf,wahariri na wabunge particularly wa ccm na watetezi wa haki za binadam nao ni wana m4c?
Hapa ndo tunakuja kuamini kuwa m4c ni chama makin,cha wanyonge,ukweli na uhakika tukiunge mkono vilivyo.

kukosoa na kusema maovu yanafanywa na ccm sio lazima uwe mwanachama wa chadema. acha ukada wa chama. unajua haya pesa EPA. Kashfa ya Richmund, twiga kupelekwa urabuni, mgodi wa kiwira na maisha magumu kwa sasa. wewe kada wa ccm unasema ni poa tu. wewe unaiifaidi keki ya taifa ndiyo maana unaisifia serikali ya magamba.ujue yana mwisho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…