Kabla ya Kuwashtaki kwa "Uhujumu Uchumi" Wachawi Wetu; Swali hili Serikali ilijibu kwanza..

Kabla ya Kuwashtaki kwa "Uhujumu Uchumi" Wachawi Wetu; Swali hili Serikali ilijibu kwanza..

Kwani huyo ndo wa kwanza kuidai serikali? Kwani serikali haijazoea madeni?

Lazima wawajibishwe waliosuka mchongo kuibua swala ambalo muhusika binafsi hakua na mpango nalo, ingekua ni kwania njema angetoa taarifa kwanza kwa serikali ila kwakua alikua hajui chochote ni wanasheria wasio na nia njema walimjaza ujinga na kumshinikiza
Una uhakika kwamba mdai hakuwa na mpango wa kudai deni lake? mbona mnatumia nguvu nyingi sana kusema uwongo kwenye jambo ambalo lipo wazi kabisa.kudaiwa wala sio shida shida ni kukataa kulipa deni
 
Ikithibitika kuna Mtanzania yoyote aliyemsaidia Muzungu na najua wapo na wanajulikana kwa namna yoyote ile kukamata Mali yetu, hiyo ni treason.

Kwa maoni yangu wala Serikali isimfungulie mashitaka na kuanza kukimbizana Mahakamani na kuwapa umaarufu, Serikali iende stealth na kudili nao kimafia, kama ni Mawakili futa kibali cha Uwakili JMTZ, kama wana biashara no leseni na watumiwe TRA walipe deni lolote lililopo, marufuku kutumia kumbi yoyote hapa TZ hata kwa harusi ya wanafamilia, watoto wao wawe blacklisted hakuna kuajiriwa TZ hata watu binafsi na atakaye waajiri TRA imvae, pensheni yao futa, wakiomba passport ya JMTZ wao na familia zao hakuna kupata, ardhi yoyote hata kama ni ya familia irudi Serikalini, marufuku kutumia Airport yetu mpya n.k.

Kama anaweza kwenda mbali kiasi hicho halafu tunachekeana? What’s next? Hapa ni lazima fundisho litolewe vinginevyo tutakuwa hatuna nchi!
Badala ya kutumia akili kutatua tatizo unatumia nguvu. Yaani ndio akili za kiccm ndio maana hatusongi mbele.
 
Lipeni deni la watu. Ndege iachiwe.

Ndege ikiachiwa hiyo hela hamtalipa.

Toka lini jiwe akafuata makubaliano?
 
Ikithibitika kuna Mtanzania yoyote aliyemsaidia Muzungu na najua wapo na wanajulikana kwa namna yoyote ile kukamata Mali yetu, hiyo ni treason.

Kwa maoni yangu wala Serikali isimfungulie mashitaka na kuanza kukimbizana Mahakamani na kuwapa umaarufu, Serikali iende stealth na kudili nao kimafia, kama ni Mawakili futa kibali cha Uwakili JMTZ, kama wana biashara no leseni na watumiwe TRA walipe deni lolote lililopo, marufuku kutumia kumbi yoyote hapa TZ hata kwa harusi ya wanafamilia, watoto wao wawe blacklisted hakuna kuajiriwa TZ hata watu binafsi na atakaye waajiri TRA imvae, pensheni yao futa, wakiomba passport ya JMTZ wao na familia zao hakuna kupata, ardhi yoyote hata kama ni ya familia irudi Serikalini, marufuku kutumia Airport yetu mpya n.k.

Kama anaweza kwenda mbali kiasi hicho halafu tunachekeana? What’s next? Hapa ni lazima fundisho litolewe vinginevyo tutakuwa hatuna nchi!
Nyie ndo washauri wa jiwe.

Mambo yakibuma mnaanza kulia uzalendo.

Nchi haipelekwi kishamba hivi. JK alikula bata na mambo yakawa sawa.
 
Leo imebidi nikupe like wanguwangu Kati ya mada ulizo wahi kuandika Hapa jukwaani Leo umeongea ukweli sisi Kama watanzania tunapaswa kua wakweli maana wanaotuongoza hawapendi ukweli basi tusimame katika ukweli ili wanaoona kusema ukweli ni kukosa uzalendo waenderee kuumia mpaka waujue ujinga walionao
 
Ikithibitika kuna Mtanzania yoyote aliyemsaidia Muzungu na najua wapo na wanajulikana kwa namna yoyote ile kukamata Mali yetu, hiyo ni treason.

Kwa maoni yangu wala Serikali isimfungulie mashitaka na kuanza kukimbizana Mahakamani na kuwapa umaarufu, Serikali iende stealth na kudili nao kimafia, kama ni Mawakili futa kibali cha Uwakili JMTZ, kama wana biashara no leseni na watumiwe TRA walipe deni lolote lililopo, marufuku kutumia kumbi yoyote hapa TZ hata kwa harusi ya wanafamilia, watoto wao wawe blacklisted hakuna kuajiriwa TZ hata watu binafsi na atakaye waajiri TRA imvae, pensheni yao futa, wakiomba passport ya JMTZ wao na familia zao hakuna kupata, ardhi yoyote hata kama ni ya familia irudi Serikalini, marufuku kutumia Airport yetu mpya n.k.

Kama anaweza kwenda mbali kiasi hicho halafu tunachekeana? What’s next? Hapa ni lazima fundisho litolewe vinginevyo tutakuwa hatuna nchi!
Duuh ama kweli madikiteta wapo kwenye alizi ya mzanaki wewe kweli hata kwako unaishi na watu au wewe sio binadam maana inavyooneka unaweza fungia watu wasile mwezi mzima
 
Ikithibitika kuna Mtanzania yoyote aliyemsaidia Muzungu na najua wapo na wanajulikana kwa namna yoyote ile kukamata Mali yetu, hiyo ni treason.

Kwa maoni yangu wala Serikali isimfungulie mashitaka na kuanza kukimbizana Mahakamani na kuwapa umaarufu, Serikali iende stealth na kudili nao kimafia, kama ni Mawakili futa kibali cha Uwakili JMTZ, kama wana biashara no leseni na watumiwe TRA walipe deni lolote lililopo, marufuku kutumia kumbi yoyote hapa TZ hata kwa harusi ya wanafamilia, watoto wao wawe blacklisted hakuna kuajiriwa TZ hata watu binafsi na atakaye waajiri TRA imvae, pensheni yao futa, wakiomba passport ya JMTZ wao na familia zao hakuna kupata, ardhi yoyote hata kama ni ya familia irudi Serikalini, marufuku kutumia Airport yetu mpya n.k.

Kama anaweza kwenda mbali kiasi hicho halafu tunachekeana? What’s next? Hapa ni lazima fundisho litolewe vinginevyo tutakuwa hatuna nchi!
Kuna mijitu mijinga kwelikweli.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna watu wanasema ‘lipeni deni la watu’ na wengine wanasema ‘dawa ya deni ni kulipa’. Katika sakata la kushikiliwa ndege ya Tanzania huko Afrika Kusini kambi mbili kubwa zimeibuka zikiwagawa Watanzania. Kambi hizi zinaonekana zinafuata mwelekeo wa kisiasa. Kuna kambi ya wanaoona kuwa serikali imejitakia na hivyo inastahili inachokipata na kambi nyingine ambayo inaonekana kuwa serikali inahujumiwa na kikundi Fulani.

Kukamatwa kwa ndege hiyo wiki iliyopita kumeacha maswali ya aina nyingi na hisia nyingi miongoni mwa wananchi. Ukimsikiliza msemaji wa Serikali Dkt. Abbas alipozungumza na waandishi wa habari leo unaweza kuona kuwa hata ndani ya serikali watu wamegawanyika na kuwa kuna hisia kuwa kilichotokea ni njama Fulani za kumkwamisha Rais Magufuli. Msimamo wa serikali kuwa itawashughulikia wale wote waliohusika katika kufanikisha kukamatwa kwa ndege hili kwa ‘kuhujumu uchumi’ linahitaji kuangaliwa kwa karibu na kufikiriwa kwa umakini mkubwa.

Mchawi Wetu ni Nani?

Swali kubwa ni kuwa ni nani alisababisha ndege hii ikamatwe kwa deni ambalo sreikali ilikuwa inalijua? Hili ni swali moja tu. Kukamatwa kwa ndege hii inaonekana kulifanywa kimkakati wa kisheria na waliohusika na waliinyemelea ndege bila vyombo vyetu vyovyote kujua au kuwa na taarifa na matokeo yake ni kile kilichotokea.

Je, mchawi wetu ni mdeni wetu Bw. Steyn? Au mchawi wetu ni wale wanasheria (wakiwemo Watanzania) ambao walibuni mkakati huu mkali? Au wachawi wetu ni vyombo vya Afrika ya Kusini ambao majuzi tu tumepokea ugeni wao na kuwaonesha ukarimu wetu na udugu wa damu? Je, Afrika Kusini ingejaribu hata kutukonyeza tu kutuambia ndege isiende Afrika Kusini kwa sababu kuna watu wanainyemelea? Au wachawi wetu ni serikali yenyewe ambayo ikijua kuwa imetia saini makubaliano ya kutekeleza hukumu za nchi za SADC na ilijua inadaiwa na kuwa mahali popote katika nchi ya SADC watu wanaweza kudai hukumu itekelezwe? Kwamba AG hakutoa ushauri mzuri wa matokeo ya kupeleka ndege huku bado kuna deni na madai dhidi ya serikali?

Haya si Maswali Muhimu Kivile

Naomba kupendekeza kuwa maswali haya siyo muhimu kivile kuliko hili swali linalofuatia. Binafsi swali ambalo ningependa nione linajibiwa na serikali ni hili: Kwanini deni la Bw. Steyn liliachwa kulipwa wakati tayari serikali ilishakubali, ilishaanza kulipa na ilikuwa inaendelea kulipa? Ndugu zangu hatuwezi kumpata mchawi au msaidizi wa mchawi bila kujua kwanza mchawi alitumia ungo gani! Hili ni swali muhimu sana; kama tuliacha kulipa deni ambalo ni deni halali basi hakuna mchawi. Mdai wetu alikuwa katika haki zake zote za kudai na kutulazimisha kumlipa. Lakini naomba kupendekeza yafuatayo katika kuangalia hili la kuamua kutokulipa deni.

1. Tuliacha Kulipa kwa Sababu Hatulipendi Deni

Hakuna mtu anayependa kudaiwa. Kudaiwa kunadhalilisha, kunafedhehesha na kwa kila kipimo kunafanya uwe unawiwa kihisia na kiakili. Ukiwa na deni kubwa inabidi uwe unalifikiria mara kwa mara, unalipigia mahesabu, na unalitafutia hela kulilipa. Lakini kama deni ni halali sisi kutokulipenda deni hilo hakuondoi uhalali wa kutakiwa kulilipa. Kutolipenda deni siyo sababu wala kisingizio cha kutokulilipa.

2. Tuliacha Kulipa kwa Sababu Hatulitaki Deni

Inawezakana tuliacha kuendelea kulipa kwa sababu hatulitaki hilo deni. Hatulitaki kwa sababu linatulazimisha kutumia fedha zetu kuwalipa watu wengine badala ya kutumia fedha hizo kufanya mambo mengine ya maendeleo. Kumlipa mtu mmoja bilioni 33 na ushee wakati nchi ina mahitaji mengine muhimu inaweza kuonekana ni matumizi mabaya ya fedha. Lakini ukweli bado ni ule ule; kama mtu anatudai basi anachodai si chetu ni chake na kutokutaka kulipa hakuondoi uhalali wa yeye kutudai au kutushinikiza kumlipa. Kutokulitaka deni siyo sababu wala kisingizio cha kutokulilipa.

3. Tuliacha Kulipa kwa Sababu Deni ni Kubwa Mno

Unapochukua deni au unapokubali deni hasa haya ya fedha mara nyingi yanakuwa na taratibu za yafuatayo. Kuna deni la msingi (principle), kuna adhabu (punitive damage) na kuna riba (interest). Deni la msingi ni kile hasa kinachodaiwa na adhabu ni kile kilichoamuliwa kuwa ni adhabu kwa sisi kusababisha deni. Riba ni kile kiasi cha asilimia ambacho kinatakiwa kulipwa juu ya deni kwa kila muda au kiasi ambacho deni linakuwa halijapwa.

Riba inaweza kuwa ya aina nyingi; kuna riba zinatakiwa kulipwa kila siku deni halijalipwa, au kila mwezi na inaongezeka kwa kadiri deni halijalipwa.

Kitu kibaya katika riba ni kuwa kama deni halijalipwa kwa wakati uliotakiwa riba inaweza kuwa kubwa sana kiasi hata cha kupita deni lenyewe. Taasisi nyingi za fedha na zinazotoa mikopo zinatengeneza fedha (faida) kwa kupitia riba kuliko deni la msingi. Mtu akikopa shilingi laki moja halafu baada ya mwezi mmoja akarudisha shilingi laki moja yule mtoa mkopa anapata faida gani? Hana! Hivyo riba na adhabu ni namna ambazo mtu, shirika au taasisi inavuna kutoka kwa mkopaji.

Mkopaji hawezi kusema sitaki tena kulipa riba kwa sababu ni kubwa; hili lilitakiwa liwe limekubaliwa wakati wa majadiliano.

4. Tuliacha Kulipa Deni kwa sababu Deni Halilipiki

Sasa wakati mwingine mtu anaweza kujikuta anaacha kabisa kulipa deni (servicing a debt) kwa sababu anaamini na anajua kuwa hata ajaribu vipi hatoweza kumaliza kulilipa deni hilo; ama kutokana na ukubwa wa deni au kutokana na uzito wa adhabu na riba.

Kuelekea mwaka 2000 kulikuwa na kampeni kubwa ya kimataifa ya kutaka madeni ya nchi za dunia ya tatu yasamehewa. Hii ni mojawapo ya kazi kubwa alizofanya Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere kabla ya kifo chake akiwa na watu wengine mashuhuri kama Bono wa U2. Hoja zao zilikuwa za aina mbili tu; kwamba madeni hayo hayalipiki kwa sababu 1. Nchi maskini hazikuwa na uwezo wa kulipa madeni hayo kutokana na umaskini na 2. Madeni hayo yaliingiwa katika mazingira ambayo yaliyafanya yawe ya kionevu (immoral). Nchi tajiri hazikuwa na sababu ya kuwabana maskini wawalipe kutoka katika umaskini wao huku wao matajiri wakizidi kuongeza katika utajiri wao. Na kweli, nchi nyingi tajiri zilifutia nchi maskini madini na kuwapa nafasi ya kuanza upya.

Sasa deni hili linaweza kuangukia huko?
Je, deni la Steyn linaweza kuangukia huku? Kwamba, tumelipa kiasi kikubwa cha deni la msingi, na hata riba tumeilipa lakini inaonekana haiishi na haiwezekani kuisha. Kwamba, nchi yetu bado ni maskini na kulipa fedha hizi zote ni kukubali kuendelea kuwafanya Watanzania waishi kimaskini na kuendeleza umaskini.
Tatizo la hoja hii ni kuwa kama hii ni Imani ya serikali basi ilitakiwa ianishwe na kuwekwa bayana katika vyombo husika vya kimahakama na kufanya mazungumzo na mdai wetu kuweza kukubaliana kile kinachoitwa “settlement”.

Haja ya kuwa “Settlement”

Naomba kupendekeza kuwa kwa sababu yoyote ya hapo juu ni wazi kuwa inatulazimu na serikali inalazimika kufikiria kufikia mwafaka (settlement) na mdai wetu. Mwafaka huo unaweza kulamishwa na matokeo ya kesi iliyofunguliwa na serikali huko Afrika ya Kusini. Mahakama inaweza ikatoa muda kwa ndege kuachiliwa lakini wahusika wakae chini na kukubaliana mwafaka – bila kutafutana uchawi.

Kwamba, tukubaliane badala ya kumlipa bilioni 33 tuwe tayari kumlipa bilioni 15 kwa mkupuo bila riba wala adhabu. Lakini na yeye aondoe madai yote dhidi ya serikali na serikali kuondoa madai yoyote dhidi yake. Na kwa upande wake serikali inaweza kumrudishia ofa yake ya uraia wa Tanzania (inawezekana hili lilimuumiza zaidi).
Kumbe wakati mwingine madeni yanaweza kumalizwa kwa mazungumzo baina ya pande mbili badala ya kutumia visasi. Kwani serikali ikiamua kubana inaweza kubana tena.

Lakini vyovyote tutakavyofanya itakuwa ni kosa kubwa sana kuanza kuwatafuta wachawi nje ya wachawi wenyewe. Na ili tujue mchawi wetu hasa ni nani ni lazima tujibu hili swali: Kwani kwa nini tuliacha kulipa deni ambalo tulishakubali kuwa ni halali na tulishaanza kulilipa?

Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com
Umekwepa uhalisia na umekuwa na mjadala wa upande mmoja kuvictimize Serikali na ukutazama upande wa pili wa Steyn Je ana uhalali wa Kulipwa pamoja na kuwa alishalipwa ...Kuwa Tajiri sio dhambi, dhambi ni njia ambazo zitatumika kupata utajiri huo, Twapasa kuwa wakweli wa KILICHO CHA KWELI , Je ni kweli TUNASTAHIKI KULIPA manake ata kama raia wa Taifa letu walihusika kumpa Uhalali wa Kisheria, si Uhalali wa UJWELI au UHALISi basi turudi kwenye KUTAFUTA UKWELI lakini si KULAZIMISHA KULIPA VITU VYA KIOVU ETI KWA SABABAU VIMEPEWA HAKI ZA KISHERIA UHALALI WA KISH
 
Ukiwa mtawala jeuri dhambi nyingi utaziona ,fikiria huko Mbeya leo wananchi wanapigwa polisi wanaiba kwenye maduka,mkuu wa mkoa anasema maliza wanakijiji wote,sasa Nani atakaa alilie uzalendo?
 
Mwanakijiji imeandika vizuri. Lakini kusema kuwa kwenye suala hili taifa limegawanyika kambi mbili ni kuweka chumvi. Ukweli ni kwambà Watanzania wanaelewa kuwa serikali yetu inatumia nguvu kukataa kumalizia kulipia deni halali. Watanzania ni watu wastaarabu, wapole na wanaopenda haki. Hawawezi kufurahia kitendo cha serikali kutotenda haki. Wanaoshabikia ubabe wa serikali ni kikundi kidogo kilichopandikizwa mitandaoni kwa ajili ya kuihami serikali yetu kwenye jambo lolote jema au baya!
 
Fikra zangu:
Mpaka ndege inadakwa maana yake request za Steyn hazikuwa na taswira yoyote kuwa Serikali Itamlipa na katika hatua zipi.Hivyo basi unaweza kusema wanasheria wetu wanashindwa kutafsiri sheria au wanang'ang'aniza vitu kwa kutumia kauli "serikali isishindwe kesi" kitu ambacho sio sahihi kabisa kama watendaji hawakuwa makini wakati wa tukio,ni jukumu la serkali kuhakikisha mzani umeelekea upande sahihi, ata sisi RAIA kuna vitu tunavidai kwa serikali, pia serikali inatudai..muda mrefu kasumba walizonazo baadhi ya maofisa zimekuwa zikiipa Serikali nguvu ambayo ata katiba haijawahi kuonesha kitu kama hicho.
Citizen/Individual akiidai serikali anapata shida sana ata kama uhalisia mzani ulitakiwa umpe haki.
Mfano wangekubali kumlipa steyn kwa makubaliano maalum,ndege ingekuwa imeruka siku ya pili tu baada ya kuzuiliwa..Air Tanzania inachafuka na Taifa linaonekana kuwa la watu wasio makini sababu ya watu wachache wenye itikadi zao..Mimi kama mwanachi mpenda maendeleo naona ifike mahali wanasheria,watu wa hazina,bunge na ikulu waanze utekelezaji katika maswala yote yanayonekana yataleta shida kwa Air Tanzania,haiwezekani tukaendelea kuwa na wasiwasi katika kurusha ndege kwenda nje ya nchi.Tushakubali kuwa na ndege na zinatumia fedha nyingi,pia zina depreciate zikitumika na zisipotumika.Tujiulize tu Tulipe ndege iruke,Tushinde kesi akate rufaa alafu tukamatwe tena?
Kwa nini kila deni au tatizo la Serikali watu wa nataka kulihamishia katika Air Tanzania,Serikali ifanye nini kuepusha Air Tanzania kuwa ina uhusiano nayo wa moja kwa moja katika matatizo,kama Air Tanzania ni legal person kwa nini Waziri,Balozi hajakamatwa ila mali ya ATCL?
 
Ikithibitika kuna Mtanzania yoyote aliyemsaidia Muzungu na najua wapo na wanajulikana kwa namna yoyote ile kukamata Mali yetu, hiyo ni treason.

Kwa maoni yangu wala Serikali isimfungulie mashitaka na kuanza kukimbizana Mahakamani na kuwapa umaarufu, Serikali iende stealth na kudili nao kimafia, kama ni Mawakili futa kibali cha Uwakili JMTZ, kama wana biashara no leseni na watumiwe TRA walipe deni lolote lililopo, marufuku kutumia kumbi yoyote hapa TZ hata kwa harusi ya wanafamilia, watoto wao wawe blacklisted hakuna kuajiriwa TZ hata watu binafsi na atakaye waajiri TRA imvae, pensheni yao futa, wakiomba passport ya JMTZ wao na familia zao hakuna kupata, ardhi yoyote hata kama ni ya familia irudi Serikalini, marufuku kutumia Airport yetu mpya n.k.

Kama anaweza kwenda mbali kiasi hicho halafu tunachekeana? What’s next? Hapa ni lazima fundisho litolewe vinginevyo tutakuwa hatuna nchi!
Si hamjaribiwi nyie? Mbona sasa mnajambajamba tu na vitisho kibao?
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna watu wanasema ‘lipeni deni la watu’ na wengine wanasema ‘dawa ya deni ni kulipa’. Katika sakata la kushikiliwa ndege ya Tanzania huko Afrika Kusini kambi mbili kubwa zimeibuka zikiwagawa Watanzania. Kambi hizi zinaonekana zinafuata mwelekeo wa kisiasa. Kuna kambi ya wanaoona kuwa serikali imejitakia na hivyo inastahili inachokipata na kambi nyingine ambayo inaonekana kuwa serikali inahujumiwa na kikundi Fulani.

Kukamatwa kwa ndege hiyo wiki iliyopita kumeacha maswali ya aina nyingi na hisia nyingi miongoni mwa wananchi. Ukimsikiliza msemaji wa Serikali Dkt. Abbas alipozungumza na waandishi wa habari leo unaweza kuona kuwa hata ndani ya serikali watu wamegawanyika na kuwa kuna hisia kuwa kilichotokea ni njama Fulani za kumkwamisha Rais Magufuli. Msimamo wa serikali kuwa itawashughulikia wale wote waliohusika katika kufanikisha kukamatwa kwa ndege hili kwa ‘kuhujumu uchumi’ linahitaji kuangaliwa kwa karibu na kufikiriwa kwa umakini mkubwa.

Mchawi Wetu ni Nani?

Swali kubwa ni kuwa ni nani alisababisha ndege hii ikamatwe kwa deni ambalo sreikali ilikuwa inalijua? Hili ni swali moja tu. Kukamatwa kwa ndege hii inaonekana kulifanywa kimkakati wa kisheria na waliohusika na waliinyemelea ndege bila vyombo vyetu vyovyote kujua au kuwa na taarifa na matokeo yake ni kile kilichotokea.

Je, mchawi wetu ni mdeni wetu Bw. Steyn? Au mchawi wetu ni wale wanasheria (wakiwemo Watanzania) ambao walibuni mkakati huu mkali? Au wachawi wetu ni vyombo vya Afrika ya Kusini ambao majuzi tu tumepokea ugeni wao na kuwaonesha ukarimu wetu na udugu wa damu? Je, Afrika Kusini ingejaribu hata kutukonyeza tu kutuambia ndege isiende Afrika Kusini kwa sababu kuna watu wanainyemelea? Au wachawi wetu ni serikali yenyewe ambayo ikijua kuwa imetia saini makubaliano ya kutekeleza hukumu za nchi za SADC na ilijua inadaiwa na kuwa mahali popote katika nchi ya SADC watu wanaweza kudai hukumu itekelezwe? Kwamba AG hakutoa ushauri mzuri wa matokeo ya kupeleka ndege huku bado kuna deni na madai dhidi ya serikali?

Haya si Maswali Muhimu Kivile

Naomba kupendekeza kuwa maswali haya siyo muhimu kivile kuliko hili swali linalofuatia. Binafsi swali ambalo ningependa nione linajibiwa na serikali ni hili: Kwanini deni la Bw. Steyn liliachwa kulipwa wakati tayari serikali ilishakubali, ilishaanza kulipa na ilikuwa inaendelea kulipa? Ndugu zangu hatuwezi kumpata mchawi au msaidizi wa mchawi bila kujua kwanza mchawi alitumia ungo gani! Hili ni swali muhimu sana; kama tuliacha kulipa deni ambalo ni deni halali basi hakuna mchawi. Mdai wetu alikuwa katika haki zake zote za kudai na kutulazimisha kumlipa. Lakini naomba kupendekeza yafuatayo katika kuangalia hili la kuamua kutokulipa deni.

1. Tuliacha Kulipa kwa Sababu Hatulipendi Deni

Hakuna mtu anayependa kudaiwa. Kudaiwa kunadhalilisha, kunafedhehesha na kwa kila kipimo kunafanya uwe unawiwa kihisia na kiakili. Ukiwa na deni kubwa inabidi uwe unalifikiria mara kwa mara, unalipigia mahesabu, na unalitafutia hela kulilipa. Lakini kama deni ni halali sisi kutokulipenda deni hilo hakuondoi uhalali wa kutakiwa kulilipa. Kutolipenda deni siyo sababu wala kisingizio cha kutokulilipa.

2. Tuliacha Kulipa kwa Sababu Hatulitaki Deni

Inawezakana tuliacha kuendelea kulipa kwa sababu hatulitaki hilo deni. Hatulitaki kwa sababu linatulazimisha kutumia fedha zetu kuwalipa watu wengine badala ya kutumia fedha hizo kufanya mambo mengine ya maendeleo. Kumlipa mtu mmoja bilioni 33 na ushee wakati nchi ina mahitaji mengine muhimu inaweza kuonekana ni matumizi mabaya ya fedha. Lakini ukweli bado ni ule ule; kama mtu anatudai basi anachodai si chetu ni chake na kutokutaka kulipa hakuondoi uhalali wa yeye kutudai au kutushinikiza kumlipa. Kutokulitaka deni siyo sababu wala kisingizio cha kutokulilipa.

3. Tuliacha Kulipa kwa Sababu Deni ni Kubwa Mno

Unapochukua deni au unapokubali deni hasa haya ya fedha mara nyingi yanakuwa na taratibu za yafuatayo. Kuna deni la msingi (principle), kuna adhabu (punitive damage) na kuna riba (interest). Deni la msingi ni kile hasa kinachodaiwa na adhabu ni kile kilichoamuliwa kuwa ni adhabu kwa sisi kusababisha deni. Riba ni kile kiasi cha asilimia ambacho kinatakiwa kulipwa juu ya deni kwa kila muda au kiasi ambacho deni linakuwa halijapwa.

Riba inaweza kuwa ya aina nyingi; kuna riba zinatakiwa kulipwa kila siku deni halijalipwa, au kila mwezi na inaongezeka kwa kadiri deni halijalipwa.

Kitu kibaya katika riba ni kuwa kama deni halijalipwa kwa wakati uliotakiwa riba inaweza kuwa kubwa sana kiasi hata cha kupita deni lenyewe. Taasisi nyingi za fedha na zinazotoa mikopo zinatengeneza fedha (faida) kwa kupitia riba kuliko deni la msingi. Mtu akikopa shilingi laki moja halafu baada ya mwezi mmoja akarudisha shilingi laki moja yule mtoa mkopa anapata faida gani? Hana! Hivyo riba na adhabu ni namna ambazo mtu, shirika au taasisi inavuna kutoka kwa mkopaji.

Mkopaji hawezi kusema sitaki tena kulipa riba kwa sababu ni kubwa; hili lilitakiwa liwe limekubaliwa wakati wa majadiliano.

4. Tuliacha Kulipa Deni kwa sababu Deni Halilipiki

Sasa wakati mwingine mtu anaweza kujikuta anaacha kabisa kulipa deni (servicing a debt) kwa sababu anaamini na anajua kuwa hata ajaribu vipi hatoweza kumaliza kulilipa deni hilo; ama kutokana na ukubwa wa deni au kutokana na uzito wa adhabu na riba.

Kuelekea mwaka 2000 kulikuwa na kampeni kubwa ya kimataifa ya kutaka madeni ya nchi za dunia ya tatu yasamehewa. Hii ni mojawapo ya kazi kubwa alizofanya Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere kabla ya kifo chake akiwa na watu wengine mashuhuri kama Bono wa U2. Hoja zao zilikuwa za aina mbili tu; kwamba madeni hayo hayalipiki kwa sababu 1. Nchi maskini hazikuwa na uwezo wa kulipa madeni hayo kutokana na umaskini na 2. Madeni hayo yaliingiwa katika mazingira ambayo yaliyafanya yawe ya kionevu (immoral). Nchi tajiri hazikuwa na sababu ya kuwabana maskini wawalipe kutoka katika umaskini wao huku wao matajiri wakizidi kuongeza katika utajiri wao. Na kweli, nchi nyingi tajiri zilifutia nchi maskini madini na kuwapa nafasi ya kuanza upya.

Sasa deni hili linaweza kuangukia huko?
Je, deni la Steyn linaweza kuangukia huku? Kwamba, tumelipa kiasi kikubwa cha deni la msingi, na hata riba tumeilipa lakini inaonekana haiishi na haiwezekani kuisha. Kwamba, nchi yetu bado ni maskini na kulipa fedha hizi zote ni kukubali kuendelea kuwafanya Watanzania waishi kimaskini na kuendeleza umaskini.
Tatizo la hoja hii ni kuwa kama hii ni Imani ya serikali basi ilitakiwa ianishwe na kuwekwa bayana katika vyombo husika vya kimahakama na kufanya mazungumzo na mdai wetu kuweza kukubaliana kile kinachoitwa “settlement”.

Haja ya kuwa “Settlement”

Naomba kupendekeza kuwa kwa sababu yoyote ya hapo juu ni wazi kuwa inatulazimu na serikali inalazimika kufikiria kufikia mwafaka (settlement) na mdai wetu. Mwafaka huo unaweza kulamishwa na matokeo ya kesi iliyofunguliwa na serikali huko Afrika ya Kusini. Mahakama inaweza ikatoa muda kwa ndege kuachiliwa lakini wahusika wakae chini na kukubaliana mwafaka – bila kutafutana uchawi.

Kwamba, tukubaliane badala ya kumlipa bilioni 33 tuwe tayari kumlipa bilioni 15 kwa mkupuo bila riba wala adhabu. Lakini na yeye aondoe madai yote dhidi ya serikali na serikali kuondoa madai yoyote dhidi yake. Na kwa upande wake serikali inaweza kumrudishia ofa yake ya uraia wa Tanzania (inawezekana hili lilimuumiza zaidi).
Kumbe wakati mwingine madeni yanaweza kumalizwa kwa mazungumzo baina ya pande mbili badala ya kutumia visasi. Kwani serikali ikiamua kubana inaweza kubana tena.

Lakini vyovyote tutakavyofanya itakuwa ni kosa kubwa sana kuanza kuwatafuta wachawi nje ya wachawi wenyewe. Na ili tujue mchawi wetu hasa ni nani ni lazima tujibu hili swali: Kwani kwa nini tuliacha kulipa deni ambalo tulishakubali kuwa ni halali na tulishaanza kulilipa?

Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com
Kwa maoni yangu mm nimeona kuna kosa kubwa sana hichi chombo kinachojiita usalama wa taifa kwa kutopata kwa wakat taarifa za kiintelijensia ambazo wangechukua hatua za haraka kama usafir mbadala ambao ungewasafirisha hao abiri alaf na sisi tubadilishe routes zetu za S. A huku kimya kimya tunalifanyia kaz hilo deni bila ya watanzania kujua.

Swala lingine la hao wanasheria wa tz hili swala jamani wale nao wanatafuta riziki zao,na kila taaluma ina miiko yake, imagine kaka yako kapewa iyo deal . Au trump baada ya uchaguz angeanza deal na Mrs Clinton na washirika wake, unadhani kuna progress yeyote wangefanya katika ilo tiaifa, swala ilo la wansheria inabid hata serikali iwachukulie kama watu muhimu ambao watakuja lisaidia taifa kwenye changamoto kama hizi... Niwajuavyo waafrika sisi huwaga hatu deal na matatizo tuna deal na watu kutatua matatzo ndio maana hatuendelei

Elimu kitu muhimu sana.. Maana uwezo mdogo wa kupambanua mambo ni kutokata na kupata elimu ya viwango vidogo
 
Umekwepa uhalisia na umekuwa na mjadala wa upande mmoja kuvictimize Serikali na ukutazama upande wa pili wa Steyn Je ana uhalali wa Kulipwa pamoja na kuwa alishalipwa ...Kuwa Tajiri sio dhambi, dhambi ni njia ambazo zitatumika kupata utajiri huo, Twapasa kuwa wakweli wa KILICHO CHA KWELI , Je ni kweli TUNASTAHIKI KULIPA manake ata kama raia wa Taifa letu walihusika kumpa Uhalali wa Kisheria, si Uhalali wa UJWELI au UHALISi basi turudi kwenye KUTAFUTA UKWELI lakini si KULAZIMISHA KULIPA VITU VYA KIOVU ETI KWA SABABAU VIMEPEWA HAKI ZA KISHERIA UHALALI WA KISH

Ama kweli tumeshenzika! Hizi ndizo hoja za nguvu; hoja za kibabe ni kinyume kabisa na mapokeo mazuri ya nchi hii. Mimi nadhani hii kadhia ni mtihani kwa nchi yetu. Katiba yetu inatamka wazi kuwa chombo pekee cha kutoa haki kwenye nchi yetu ni mahakama. Mahakama ndiyo iliamua mkulima alipwe fidia na kiasi gani. Serikali yetu ilikubali kwa moyo mweupe kwa sababu ndiyo haki na kusema kweli kila ilipotaifisha mali ya mtu binafsi ilikuwa inalipa fidia. Ndiyo maana haikuona hata sababu ya kukata rufaa. Badala ya kupata rufaa serikali iliona ni busara kuzungumza nje ya mahakama na madeni wake ili kupata maelewano na kupunguza kiwango cha fidia kilichoamuliwa na mahakama. Mwafaka ukapatikana. Inasikitisha kuwa sasa kauli za serikali hazizungumzii tena msingi wa mgogoro uliopo na yake ni kutuhumu kuwa inahujumiwa!
 
Ikithibitika kuna Mtanzania yoyote aliyemsaidia Muzungu na najua wapo na wanajulikana kwa namna yoyote ile kukamata Mali yetu, hiyo ni treason.

Kwa maoni yangu wala Serikali isimfungulie mashitaka na kuanza kukimbizana Mahakamani na kuwapa umaarufu, Serikali iende stealth na kudili nao kimafia, kama ni Mawakili futa kibali cha Uwakili JMTZ, kama wana biashara no leseni na watumiwe TRA walipe deni lolote lililopo, marufuku kutumia kumbi yoyote hapa TZ hata kwa harusi ya wanafamilia, watoto wao wawe blacklisted hakuna kuajiriwa TZ hata watu binafsi na atakaye waajiri TRA imvae, pensheni yao futa, wakiomba passport ya JMTZ wao na familia zao hakuna kupata, ardhi yoyote hata kama ni ya familia irudi Serikalini, marufuku kutumia Airport yetu mpya n.k.

Kama anaweza kwenda mbali kiasi hicho halafu tunachekeana? What’s next? Hapa ni lazima fundisho litolewe vinginevyo tutakuwa hatuna nchi!
Duuu
 
Aliye mfukuza huyu mkulima Tanzania ni nani?

Serikali inapo sema kuna kikundi kinahujumu serekali, inamaana hatudaiwi tunasingiziwa?

Wadeni wetu wamesha jua madhaifu yetu na wanajua wapi pakutushikia, yaani sioni faida za hizi ndege sasa, maana hata zikienda ulaya lazma zitakamatwa....

Jamani mabeberu tuoneeni huruma, Tanzania tupo yatima miaka 20 sasa tunaishi bila baba...
Hivi baba alipokufa alituacha bila mlezi?
 
Unajua mtu anaweza kukudai hadi ukimuona unabadilisha njia...na kama anakungoja nyumbani basi hurudi...unatuma mtoto kuangalia kama "jamaa keshaondoka"

Na kama kuna kitu awamu ya 5 hakipendi kabisa ni ikidaiwa hasa madeni ya miongo mitatu iliyopita kwani inaamini inachelewesha miradi yake! Hata hivyo serikali hiyo hiyo isiyopenda kulipa madeni, siyo ajabu ikavunja rekodi katika kukopa!
 
Aaliwahi sema Kabudi kuwa, awamu hii imeandamwa na kesi nyingi na madai mahakamani kuliko awamu zote zilizotangulia.
Wañaotafuta mchawi, kama wana nia ya dhati kweli kumpata, na hawajampata; watakuwa na tatizo kubwa; na hata kama wakija kumpata huyo mchawi hawatoweza kumshughulikia.
Ikiwa kama mtu anaumwa malaria kwa muda mrefuna asijue kiwa tatizo ni malaria, atakuja kugundua atakapopata kichaa, basi kumtibu si lelemama.
 
Back
Top Bottom