VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Polisi jamii imezua jambo.Katika Daraja la Ubungo,Stendi ya kuelekea Mwenge,nyakati za usiku kuna matapeli.Hayo nimeyaona jana majira ya saa mbili usiku nilipokuwa nasubiri daladala kuelekea Mwenge.Matapeli hao hujifanya kuwa ni Polisi Jamii ambao wanakamata watu wanaokiuka sheria maeneo hayo.Watu ambao hujitenga pembeni kwa chini kuongea na simu au hata kusubiri gari lifike,huzongwa na watu hao wakimsingizia kuwa amejisaidia na hivyo amechafua mazingira.Kinachofuata ni mmoja wao kutoa kitambulisho(sijui halali au batili) na kutishia kumpeleka Ofisi ya Polisi Jamii Ubungo.Kutokana na wingi wao,inakuwa vigumu kwa mtu kubishana nao tena mkiwa gizani.Kidogodogo kinamtoka msingiziwa.Wanadai kuwa faini kwa kosa hilo ni 50000 au kifungo cha miezi sita.Watu wote niliowashuhudia wakikumbwa na kadhia hiyo jana waliishia kutoa 'rushwa' kwa 'Askari' hao.Wimbo wa zamani kidogo ulikuwa na maneno haya:'Bwana Mangushi nakupoa pole sana kwani hao ni walaghai.walaghai eee,wanaitwa matapeli oooooooooo,oooooooooooo wanaitwa tapeli............Kaa chonjo!!!