JWTZ inapelekwa vitani bila ruhusa ya Bunge?

JWTZ inapelekwa vitani bila ruhusa ya Bunge?

anjo

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2009
Posts
299
Reaction score
97
Moderator, napenda kuanzisha topic hii muhimu sana kwa nchi na wananchi wetu kwa sasa na siku za mbeleni.

Nchi yoyote lazima iwe na utaratibu wa kuchukua maamuzi magumu hasa yale yanayoweza kusababisha vifo kwa wananchi wake. Mawazo yangu ni kuwa nchi yoyote inaweza kumudu kupoteza hata mtu mmoja endapo interest za nchi zitavamiwa na nchi au kikundi kisichopenda maendeleo ya nchi.

Tumeshuhudia jeshi letu likipelekwa vitani Comoro bila ridhaa ya wananchi kupitia wawakilishi wao BUNGE. Je amiri jeshi mkuu hawajibiki kwa yeyote? Je, mwanajeshi anapokufa, familia itakuwa compensated vipi? Wanapata haki?

Kwa hivi sasa tumesikia jeshi letu linaelekea DRC na kwa jinsi ilivyo mpaka sasa hamna jitihada yoyote ya serikali kutaka ruhusa ya Bunge. Kwa kifupi, Bunge si kitu chochote juu ya maamuzi kama haya.

Japokuwa hakuna uharaka wa Amiri Jeshi Mkuu (Rais) kuchukua maamuzi ya kuamuru jeshi kupigana kutokana na kwamba nchi yetu haijavamiwa na interest zetu Kama nchi hazijaingiliwa ki hivyo; itakuwa busara kwa uongozi wa nchi yetu kufata taratibu zote za kutuma majeshi kwani kuna uwezekano wa kuhusika ki mapigano kama alivyoeleza Waziri Bernard Membe siku za nyuma kidogo.

Kuna uwezekano mkubwa kwamba jeshi letu chini ya Intervention Force under MONUSCO wanaweza kupigana na makundi ya waasi Mashariki mwa DRC Kama vile M23 na vikundi vingine vya Mai Mai. Kama kutakuwa na mapigano basi tuelewe wazi kuwa kutakuwa na baadhi ya majeruhi na vifo. Je, compensation itakuwa jukumu la nani? Je familia za hao wanajeshi watapata kiasi kinachotosha? Haya maswali na mengine mengi hayatakuwa na majibu kama Bunge halitahusishwa. Anayeona si tatizo aulize yaliyotokea Msumbiji. Ndugu wameshamaliza tofauti zao na watanzania waliokufa imekuwa historia.

Nadhani wabunge wana haki ya kuhoji vitu vingi hapa. Hivi suluhisho la mgogoro wa Congo ni lipi? Jeshi la Congo Lina wajibu gani na linakubalika kiasi gani kwa wananchi? Je hao waasi wana sababu za msingi kupigana au la? Je serikali ya Congo imejaribu kiasi gani kutatua matatizo ya watu wake? Je, Rais Kabila anakubalika kiasi gani hasa baada ya uchaguzi wa 2011 dhidi ya Etienne Tchisekedi? Tusiingie kusaidia yakawa kama ya msaada kwa Obote!

Mungu ibaraki Tanzania, asanteni kwa kusoma na kuchagia.
 
nADHANI UDHAIFU WAKO KATIKA KUELEWA AMRI ZA KIJESHI KUCHANGIA NA ELIMU DUNIA KIDOGO NDIVYO VINAVYOKUSIBU. Bunge madaraka yake na mipaka yake viko wazi. Tanzania haiongozwi na bunge iko chini ya Rais. Kamwe bunge halina nafasi wala uwezo wa kuamrisha mambo ya kijeshi na wa Tanzania pamoja na nchi nyingine hata zile mnazopenda kuziiga kama uingereza matumizi ya jeshi nguvu na kibali ni kwa Malkia Elizabeith. Sasa bunge lenyewe hili kama unavyoliona ndo ulipe na madaraka ya kuratibu mambo ya jeshi si tutakimbia nchi?? Hii mada yako haieleweki labda ungefanya homework naona haukupita jeshini kwa hiyo unajadili mambo ambayo si size yako
 
Ndugu katiba iliyopo sasa ni ile ya zidumu fikra za mwenyekiti wa Ccm, mwenyekiti huyu yupo juu ya sheria na anapomaliza muda wake wa uraisi hawezi kushtakiwa kwa makosa aliyofanya akiwa Raisi, maamuzi ni ya mwisho hata kama mabovu hakuna wa kumzuia. Mpaka tupate katiba mpya itakayoruhusu raisi kuwajibishwa akiwa ofisini au baada ya kumaliza muda wake, kwa sasa Raisi anaweza kufanya jambo bila kuhusisha mihimili mingine ya serikali.
 
Moderator, napenda kuanzisha topic hii muhimu sana kwa nchi na wananchi wetu kwa sasa na siku za mbeleni.

Nchi yoyote lazima iwe na utaratibu wa kuchukua maamuzi magumu hasa yale yanayoweza kusababisha vifo kwa wananchi wake. Mawazo yangu ni kuwa nchi yoyote inaweza kumudu kupoteza hata mtu mmoja endapo interest za nchi zitavamiwa na nchi au kikundi kisichopenda maendeleo ya nchi.

Tumeshuhudia jeshi letu likipelekwa vitani Comoro bila ridhaa ya wananchi kupitia wawakilishi wao BUNGE. Je amiri jeshi mkuu hawajibiki kwa yeyote? Je, mwanajeshi anapokufa, familia itakuwa compensated vipi? Wanapata haki?

Kwa hivi sasa tumesikia jeshi letu linaelekea DRC na kwa jinsi ilivyo mpaka sasa hamna jitihada yoyote ya serikali kutaka ruhusa ya Bunge. Kwa kifupi, Bunge si kitu chochote juu ya maamuzi kama haya.

Japokuwa hakuna uharaka wa Amiri Jeshi Mkuu (Rais) kuchukua maamuzi ya kuamuru jeshi kupigana kutokana na kwamba nchi yetu haijavamiwa na interest zetu Kama nchi hazijaingiliwa ki hivyo; itakuwa busara kwa uongozi wa nchi yetu kufata taratibu zote za kutuma majeshi kwani kuna uwezekano wa kuhusika ki mapigano kama alivyoeleza Waziri Bernard Membe siku za nyuma kidogo.

Kuna uwezekano mkubwa kwamba jeshi letu chini ya Intervention Force under MONUSCO wanaweza kupigana na makundi ya waasi Mashariki mwa DRC Kama vile M23 na vikundi vingine vya Mai Mai. Kama kutakuwa na mapigano basi tuelewe wazi kuwa kutakuwa na baadhi ya majeruhi na vifo. Je, compensation itakuwa jukumu la nani? Je familia za hao wanajeshi watapata kiasi kinachotosha? Haya maswali na mengine mengi hayatakuwa na majibu kama Bunge halitahusishwa. Anayeona si tatizo aulize yaliyotokea Msumbiji. Ndugu wameshamaliza tofauti zao na watanzania waliokufa imekuwa historia.

Nadhani wabunge wana haki ya kuhoji vitu vingi hapa. Hivi suluhisho la mgogoro wa Congo ni lipi? Jeshi la Congo Lina wajibu gani na linakubalika kiasi gani kwa wananchi? Je hao waasi wana sababu za msingi kupigana au la? Je serikali ya Congo imejaribu kiasi gani kutatua matatizo ya watu wake? Je, Rais Kabila anakubalika kiasi gani hasa baada ya uchaguzi wa 2011 dhidi ya Etienne Tchisekedi? Tusiingie kusaidia yakawa kama ya msaada kwa Obote!

Mungu ibaraki Tanzania, asanteni kwa kusoma na kuchagia.

Yaani kufuatilia maji, kutafuta ajira kwa wananchi na kubadilisha mitaala ya elimu inashindikana itakuwa hili la kwenda vitani? Nahofu hiyo vita itapiganwa mjengoni huku adui akiingia Dodoma.
 
nADHANI UDHAIFU WAKO KATIKA KUELEWA AMRI ZA KIJESHI KUCHANGIA NA ELIMU DUNIA KIDOGO NDIVYO VINAVYOKUSIBU. Bunge madaraka yake na mipaka yake viko wazi. Tanzania haiongozwi na bunge iko chini ya Rais. Kamwe bunge halina nafasi wala uwezo wa kuamrisha mambo ya kijeshi na wa Tanzania pamoja na nchi nyingine hata zile mnazopenda kuziiga kama uingereza matumizi ya jeshi nguvu na kibali ni kwa Malkia Elizabeith. Sasa bunge lenyewe hili kama unavyoliona ndo ulipe na madaraka ya kuratibu mambo ya jeshi si tutakimbia nchi?? Hii mada yako haieleweki labda ungefanya homework naona haukupita jeshini kwa hiyo unajadili mambo ambayo si size yako

Waziri mkuu wa Uingereza hawezi kupeleka jeshi la Malkia vitani bila idhini ya bunge. Endelea na porojo nyingine....
 
Moderator, napenda kuanzisha topic hii muhimu sana kwa nchi na wananchi wetu kwa sasa na siku za mbeleni.

Nchi yoyote lazima iwe na utaratibu wa kuchukua maamuzi magumu hasa yale yanayoweza kusababisha vifo kwa wananchi wake. Mawazo yangu ni kuwa nchi yoyote inaweza kumudu kupoteza hata mtu mmoja endapo interest za nchi zitavamiwa na nchi au kikundi kisichopenda maendeleo ya nchi.

Tumeshuhudia jeshi letu likipelekwa vitani Comoro bila ridhaa ya wananchi kupitia wawakilishi wao BUNGE. Je amiri jeshi mkuu hawajibiki kwa yeyote? Je, mwanajeshi anapokufa, familia itakuwa compensated vipi? Wanapata haki?

Kwa hivi sasa tumesikia jeshi letu linaelekea DRC na kwa jinsi ilivyo mpaka sasa hamna jitihada yoyote ya serikali kutaka ruhusa ya Bunge. Kwa kifupi, Bunge si kitu chochote juu ya maamuzi kama haya.

Japokuwa hakuna uharaka wa Amiri Jeshi Mkuu (Rais) kuchukua maamuzi ya kuamuru jeshi kupigana kutokana na kwamba nchi yetu haijavamiwa na interest zetu Kama nchi hazijaingiliwa ki hivyo; itakuwa busara kwa uongozi wa nchi yetu kufata taratibu zote za kutuma majeshi kwani kuna uwezekano wa kuhusika ki mapigano kama alivyoeleza Waziri Bernard Membe siku za nyuma kidogo.

Kuna uwezekano mkubwa kwamba jeshi letu chini ya Intervention Force under MONUSCO wanaweza kupigana na makundi ya waasi Mashariki mwa DRC Kama vile M23 na vikundi vingine vya Mai Mai. Kama kutakuwa na mapigano basi tuelewe wazi kuwa kutakuwa na baadhi ya majeruhi na vifo. Je, compensation itakuwa jukumu la nani? Je familia za hao wanajeshi watapata kiasi kinachotosha? Haya maswali na mengine mengi hayatakuwa na majibu kama Bunge halitahusishwa. Anayeona si tatizo aulize yaliyotokea Msumbiji. Ndugu wameshamaliza tofauti zao na watanzania waliokufa imekuwa historia.

Nadhani wabunge wana haki ya kuhoji vitu vingi hapa. Hivi suluhisho la mgogoro wa Congo ni lipi? Jeshi la Congo Lina wajibu gani na linakubalika kiasi gani kwa wananchi? Je hao waasi wana sababu za msingi kupigana au la? Je serikali ya Congo imejaribu kiasi gani kutatua matatizo ya watu wake? Je, Rais Kabila anakubalika kiasi gani hasa baada ya uchaguzi wa 2011 dhidi ya Etienne Tchisekedi? Tusiingie kusaidia yakawa kama ya msaada kwa Obote!

Mungu ibaraki Tanzania, asanteni kwa kusoma na kuchagia.
mambo haya yote yanafanyika kwa mujibu wa sheria kanuni na taratibu za kitaifa na kimataifa.kuhusu maslahi ya taifa angalia kwa mapana na marefu utayaona.Kuhusu majukumu ya JWTZ! ANGALIA KWENYE WEBSITE YAO.
 
Dah!? Naona uhuru wa maoni unachukua nafasi yake sasa....sijui katiba mpya itasema "Wananchi kushika hatam zote za uongo" badala ya Serikali tuliyokua tumezoea kusikia...sijui tafsri ya neno serikali nayo omebadirika au matumizi yake yanatofauti na maana halisi???

Nawaza tu na kujiuliza mwenyewe kwa kuandika hapa JF.
 
Yaani kufuatilia maji, kutafuta ajira kwa wananchi na kubadilisha mitaala ya elimu inashindikana itakuwa hili la kwenda vitani? Nahofu hiyo vita itapiganwa mjengoni huku adui akiingia Dodoma.
Hili bunge hamna kitu, nashangaa mnavyotaka kila kitu kipitie huko, umepita muswada wa mafao hakuna aliepiga kelele wala kuukosoa, bahada ya wafanyakazi wa migodi kushtukia inshu, viongozi wetu ndio wanajifanya kushtuka.
Kazi ya mbunge ni kulalamika badala ya kujadili, ndio maana mmekomolewa bunge halitaonekana live, sasa hiyo miswada ndio imepita kimya mwananchi hajui mbunge hajui.

 
Hili bunge hamna kitu, nashangaa mnavyotaka kila kitu kipitie huko, umepita muswada wa mafao hakuna aliepiga kelele wala kuukosoa, bahada ya wafanyakazi wa migodi kushtukia inshu, viongozi wetu ndio wanajifanya kushtuka.
Kazi ya mbunge ni kulalamika badala ya kujadili, ndio maana mmekomolewa bunge halitaonekana live, sasa hiyo miswada ndio imepita kimya mwananchi hajui mbunge hajui.


Kama unavyosema baada ya mtu nje ya Bunge kungamua mkenge basi hapo Wabunge huanzisha kasheshe na mwisho wa siku wanaumbuliwa kuwa wao wenyewe walishiriki kwenye maamuzi.
Kinachowaokowa hawa Wabunge wetu ni hali ya kukata tamaa ya wananchi kwani unafiki wao wanaoufanya wananchi tunaupigia chapuo.
 
Kuna vitu viwili vya kuangalia; Vita ni suala la kisheria - linaongozwa na kanuni na sheria zake. Tanzania ikiingia vitani rasmi (ikitangazwa vita) kuna utaratibu wa jinsi gani Bunge lazima lihusishwe. Rais hawezi kutangaza vita na tukaenda vitani bila kuhusishwa Bunge katika muda ambao umewekwa kikatiba.

Lakini kama siyo vita rasmi na shughuli mbalimbali za kijeshi Katiba imeweka hili ni mojawapo ya vile vinavyoitwa "prerogatives of the presidency". Rais anaweza kulituma jeshi mahali popote ndani na nje kwa shughuli yoyote ile. Hili ni mojawapo. Hatuko vitani na hatujawahi kwenda vitani baada ya vita vya Kagera.
 
Hapa ndo vijana wa YEBOYEBO mnapotuchanganya. Huwezi kuilinganisha Uingereza na Tanzania. Tulikwishatoka huko kwa hiyo hawa wanaotamani kuridisha utawala unaofanana na ule kabla ya Uhuru wamenoa na hawataona ndani. Uingereza wanaongozwa na Waziri Mkuu anayeingia bungeni. Sisi tuna Rais na Nyerere alikwisha toa huo utawala wa kikoloni. Kama unaifahamu vizuri Uingereza basi usingeandika hizi porojo. Baada ya Bunge kujadili ndo linalokwenda kuomba kibali kwa Malkia na siyo eti Malkia akaombe kibalicha Bunge. Vipi vijana someni mbona haya mambo yapo kwenye internate nyie usiku kucha mnajaza Jamii Forum eti ili hoja zenu zisambae kwish neiii
 
Elimu ndogo kuongoza kubwa ndio tatizo lilipo. Wewe ndio mzigo kwa taifa hoja nzito majibu mepesi Kama ya baba ritz



nADHANI UDHAIFU WAKO KATIKA KUELEWA AMRI ZA KIJESHI KUCHANGIA NA ELIMU DUNIA KIDOGO NDIVYO VINAVYOKUSIBU. Bunge madaraka yake na mipaka yake viko wazi. Tanzania haiongozwi na bunge iko chini ya Rais. Kamwe bunge halina nafasi wala uwezo wa kuamrisha mambo ya kijeshi na wa Tanzania pamoja na nchi nyingine hata zile mnazopenda kuziiga kama uingereza matumizi ya jeshi nguvu na kibali ni kwa Malkia Elizabeith. Sasa bunge lenyewe hili kama unavyoliona ndo ulipe na madaraka ya kuratibu mambo ya jeshi si tutakimbia nchi?? Hii mada yako haieleweki labda ungefanya homework naona haukupita jeshini kwa hiyo unajadili mambo ambayo si size yako
 
Wacheni kelele jamani, Jeshi linaenda kulindwa Mwekezaji wa kifansa(Total) ili achimbe mafuta ziwa Tanganyika kwa Amani.
 
anjo said:
Anayeona si tatizo aulize yaliyotokea Msumbiji. Ndugu wameshamaliza tofauti zao na watanzania waliokufa imekuwa historia.
anjo,

..majeshi ya Tanzania na Zimbabwe yasingekwenda kuwasaidia Frelimo leo hii tungekuwa tunazungumza habari nyingine kabisa.

..serikali ya Frelimo ingeanguka maana yake ni kwamba makaburu wa Afrika Kusini na vibaraka wao wa Renamo wangekuja kubisha hodi Tanzania haswa maeneo ya kusini.

..Raisi Mwinyi alichukua uamuzi wa busara kupeleka wanajeshi wetu kupigana Msumbiji na kuepusha vita katika ardhi ya Tanzania.

..kosa lililofanyika ni kutokutolewa kwa elimu ya uraia regarding what was at stake. hata mashujaa wetu waliofariki vitani Msumbiji hawajulikani kwa majina, hakuna siku maalum ya kuwakumbuka.

NB:

..askari wa Tanzania waliofariki Msumbiji wamezikwa ktk eneo la Naliendele mkoani Mtwara.
 
jamani katiba yetu ya sasa inamruhusu rais kupeleka majeshi vitani wakati wowote na anatakiwa aitishe bunge ndani ya siku 14 kulijulisha kinachoendelea.
 
Mmwaisoba, nashukuru kwa mawazo yako ingawa lugha nzuri ni ya muhimu katika kuchangia. Hatukuzaliwa tukiwa na uelewa Kama tulio nao kwa sasa.
Naona unahukumu uelewa wa mtu ingawa mambo ya jeshi inawezekana hunizidi. Kama Rais anaruhusiwa kupeleka jeshi letu bila kuhusisha taasisi za muhimu au muhimili kama Bunge unaona ni kitu kizuri mi naona siyo kabisa. Ndugu hawezi kupoteza maisha ukasema Rais ana madaraka hata ya kumpeleka kupigana na watu aliodhulumiana au kama Rais ana maslahi binafsi basi wanajeshi wafariki bila interest za nchi!
Mwisho, naona umejiunga na hii forum hata Mwaka haujaisha na mchango wako imekuwa kupinga vyama vya siasa tu! Hapa tunajadili mambo yote kwa dhumuni la kukosoa na kurekebisha mambo yasiyoenda sawa.
Nategemea utajifunza siku zinavyokwenda.
 
Wanasheria watusadie...... nijuavyo Tangazo lolote la vita kwa sheria za sasa linatolewa na Amri Jeshi Mkuu ambaye ni Rais wa nchi.................... Rais atashauria na baraza la mawaziri na Jeshi.........katiba mpya tunaweza kuliangalia kwa kuzingatia mahitaji ya leo.
 
wee acha kuzungumzia mambo yanayo husu usalama bila kujua kinachoendelea maana unawezakuta unaingilia usalama wa taifa
 
We Sosthenes, unajiunga na forum hii kwa siku 3?! Angalia na kujifunza namna ya kutoa mchango wako!
 
Back
Top Bottom