Justification kwenye swala la huyu kijana aliyejirusha rock city mall

dengue f

Member
Jun 4, 2017
18
47
Kufuatia tukio la kujiua kwa kijana Musa Ally aliyejirusha kutoka juu ya Jengo la Rock City Mall huko Mwanza, nitoe rai fupi.
Musa ameacha ujumbe unaoashiria kuwa sababu ya kujiua kwake ni kukosa ajira. Lakini kukosa ajira hakuwezi kuwa sababu ya kujiua, bali ni sababu iliyopelekea Musa kupata maradhi ya akili, kisha kujiua.

Mara nyingi kujiua, au kufikiria kujiua ni matokeo ya maradhi ya akili, kwa kesi ya Musa tunaweza sema ni maradhi ya Sonona (Depression), au "Bipolar Mania" au mengineyo. Baada ya kipindi cha sononeko, kujitahidi na hatimaye kukata tamaa, mtu hukosa sababu ya kuendelea kuishi. Mipango yake na matarajio yake vimeyeyukia hewani. Mwanga wa jua unamfanya kipofu, usiku wa giza unamuumiza macho, hakuna kinachomsaidia, au kwa ufasaha zaidi, hakuna anachoweza kukifanya kimsaidie, kwa sababu ni mgonjwa. Kwahiyo huamua kujiua.

Kujiua hutokea baada ya kufikiria mara kadhaa kufanya hivyo, au wakati mwingine mtu hujaribu kujiua bila kufanikiwa. Akirudia jaribio lake la kujiua, hufanya kwa uhakika ili asishindwe tena. Jambo la uhakika ni kuwa, kama Musa alikuwa na Sonona, basi alikwisha kuwaza kujiua kabla ya siku ya kifo chake. Kujirusha kutoka juu ya jengo refu, ni tendo la uhakika wa kujiua.

Uwepo wake juu ya jengo refu unaweza kuwa kichocheo, pengine angekuwa chini asingekufa. Pombe inayosemekana kwamba alikunywa, pia inaweza kuwa kichocheo. Pombe inasababisha athari ya kisaikolojia inayoitwa 'Disinhibition effect', ambapo mtu hushindwa kujizuia na matendo ya hatari anayowaza kuyafanya akiwa amelewa.

Zaidi kuhusu Sonona tunaweza kuelezana baadaye, leo hoja zangu ni mbili.

Kwanza, ni vema jamii ikaanza kuyapa kipaumbele maradhi ya akili, ambayo yapo kwa watanzania wengi. Na athari zake zinaonekana kwenye jamii yetu. Bahati mbaya tunayachukulia maradhi ya akili tofauti sana. Badala ya kwasaidia wagonjwa tunawapa majina ya dhihaka, kama vichaa, mataahira, mtambo, network error', dishi limecheza nk. Pengine watu hawa wangeweza kusaidiwa na kupona, lakini tunapuuza. Baadaye unasikia mtu amejiu, au ameua mke au mume au mtoto na kumkatakata kama nyama ya buchani, ni maradhi ya akili.

Pili, pasina lengo la kumtupia lawama mtu, lakini nathubutu kusema wizara inayohusika na vijana na ajira, imeshindwa kuwasaidia vijana. Tanzania 'imejifungia' chumbani wakati huu wa ulimwengu wa teknolojia na mawasiliano. Kuna fursa nyingi za ajira kwa vijana endapo tutawapa vijana nafasi ya kujipambanua kimataifa. Zipo kazi nyingi za kuingia kipato kupitia mitandao, lakini kwa mifumo ya kifedha ya Tanzania, haziwezekani. Kuna michezo mingi duniani, karibu kila siku kuna mashindano makubwa ya michezo ya kimataifa sehemu fulani duniani, watanzania wamejifungia chumbani.
Yapo mambo mengi mepesi, ambayo vijana wa nchi zingine wanafanya, lakini huwezi kufanya ndani ya Tz kwa sababu za kimfumo.

Tunahitaji mabadiliko makubwa, kwenye mifumo yetu ya elimu, shuleni, vyuoni na mitaani.
Musa, ni mtu mmoja ambaye amefikia kujiua, wapo waliokwisha kujiua na watakaojiua. Lakini athari za Sonona sio kujiua tu, ni pamoja na kuua wengine au kufa bila kujiua. Wengine wanaweza wakabaki hai, lakini wakashindwa kufanya chochote maishani hadi wanakufa.

Let's get up. Tuzungumze kujisaidia na kuwasaidia wengine.
 
Hamna jambo linaumiza sana kama ukosaji wa ajira......siku hizi inakatisha tamaa sababu hata kujitolea hawataki tena

Halafu unawaTazama hao wanaohamasisha vijana kujiajiri wakati historia za maisha yao hawakuwahi hata kufungua kigenge zaidi kuajiriwa na serikali mwanzo mwisho.

Kibaya sana wao wakiwa vijana waliajiriwa na serikali halafu wamepata nafasi kubwa wanawaambia vijana wa kizazi hiki hatutoi ajira mjiajiri........shame on you
 
Huu ni ushauri wa rasta mugabe kwa wale wapumbavu wanaowaambia vijana wajiajili ilihali wao wameajiliwa na wanazeekea ofisini
tapatalk_1545539194754.jpeg
 
Tuombe Mungu atusaidie awape Viongozi wetu Hekima na Maarifa ili watukumbuke vijana, wawe na roho za huruma upendo na kujali kama ambavyo wao walipata kutoka kwa babu zetu, Mwaka wa tatu unaenda wa4 sasa hakuna Ajira zozote seeikalini, Biashara nyingi zinafungwa, Kampuni zinapunguza wafanyakazi huku vyuo vikuu na veta zikimwaga wahitimu maelefu kila mwaka, Kilimo hakina tija mfuko wa mbolea elfu60 gunia la mahindi elfu20 kupata mfuko mmoja wa mbolea unahitaji kuuza magunia matatu ya mahindi eeh MwenyeziMungu tunyooshee kidole utukumbuke waja wako
 
Kwanza, ni vema jamii ikaanza kuyapa kipaumbele maradhi ya akili, ambayo yapo kwa watanzania wengi. Na athari zake zinaonekana kwenye jamii yetu. Bahati mbaya tunayachukulia maradhi ya akili tofauti sana. Badala ya kwasaidia wagonjwa tunawapa majina ya dhihaka, kama vichaa, mataahira, mtambo, network error', dishi limecheza nk.
sijui ni lini bongo hili litatambulika & kutiliwa mkazo stahili...
juzi ule utafiti ulio sema wabongo wengi vichaa watu waliuchukulia poa kisa tu hawatembei uchi barabarani
 
Kazi hakuna, biashara hakuna, babe wa kufarijiana hakuna, marafiki hakuna simu kwa siku zinaingia msg za tigo, kula kwenyewe shida uhakika hata wa milo miwili hakuna, mbaya zaidi kuna mtoto anakutgegemea kwa asilimia zote akiamka cha kwanza anadai chakula kwa kilio hasa.

Kuna siku nlitamani tujiue sema yule anayepitisha sumu ya panya, kunguni viroboto hakupita siku ile.
 
Sonona hiyo ila imeshapata daktari
Kazi hakuna, biashara hakuna, babe wa kufarijiana hakuna, marafiki hakuna simu kwa siku zinaingia msg za tigo, kula kwenyewe shida uhakika hata wa milo miwili hakuna, mbaya zaidi kuna mtoto anakutgegemea kwa asilimia zote akiamka cha kwanza anadai chakula kwa kilio hasa.

Kuna siku nlitamani tujiue sema yule anayepitisha sumu ya panya, kunguni viroboto hakupita siku ile.
 
Nlichojifunza watanzania wanafiki sana ukiwa na tatizo kila mtu pembeni, ila ukitokea kitu mtu amefariki wanapoibuka sasa na vilio.

Naimani kijana wa Mwanza aliwashirikisha tatizo lake hata kumsikiliza tu atoe ya moyoni hawakumpa muda, matokeo yake sasa mtu anaumia ndani kwa ndani mpaka kufikia hapo.
 
Kazi hakuna, biashara hakuna, babe wa kufarijiana hakuna, marafiki hakuna simu kwa siku zinaingia msg za tigo, kula kwenyewe shida uhakika hata wa milo miwili hakuna, mbaya zaidi kuna mtoto anakutgegemea kwa asilimia zote akiamka cha kwanza anadai chakula kwa kilio hasa.

Kuna siku nlitamani tujiue sema yule anayepitisha sumu ya panya, kunguni viroboto hakupita siku ile.
Pole Cresida
 
Kufuatia tukio la kujiua kwa kijana Musa Ally aliyejirusha kutoka juu ya Jengo la Rock City Mall huko Mwanza, nitoe rai fupi.
Musa ameacha ujumbe unaoashiria kuwa sababu ya kujiua kwake ni kukosa ajira. Lakini kukosa ajira hakuwezi kuwa sababu ya kujiua, bali ni sababu iliyopelekea Musa kupata maradhi ya akili, kisha kujiua. Mara nyingi kujiua, au kufikiria kujiua ni matokeo ya maradhi ya akili, kwa kesi ya Musa tunaweza sema ni maradhi ya Sonona (Depression), au "Bipolar Mania" au mengineyo. Baada ya kipindi cha sononeko, kujitahidi na hatimaye kukata tamaa, mtu hukosa sababu ya kuendelea kuishi. Mipango yake na matarajio yake vimeyeyukia hewani. Mwanga wa jua unamfanya kipofu, usiku wa giza unamuumiza macho, hakuna kinachomsaidia, au kwa ufasaha zaidi, hakuna anachoweza kukifanya kimsaidie, kwa sababu ni mgonjwa. Kwahiyo huamua kujiua. Kujiua , hutokea baada ya kufikiria mara kadhaa kufanya hivyo, au wakati mwingine mtu hujaribu kujiua bila kufanikiwa. Akirudia jaribio lake la kujiua, hufanya kwa uhakika ili asishindwe tena. Jambo la uhakika ni kuwa, kama Musa alikuwa na Sonona, basi alikwisha kuwaza kujiua kabla ya siku ya kifo chake. Kujirusha kutoka juu ya jengo refu, ni tendo la uhakika wa kujiua.
Uwepo wake juu ya jengo refu unaweza kuwa kichocheo, pengine angekuwa chini asingekufa. Pombe inayosemekana kwamba alikunywa, pia inaweza kuwa kichocheo. Pombe inasababisha athari ya kisaikolojia inayoitwa 'Disinhibition effect', ambapo mtu hushindwa kujizuia na matendo ya hatari anayowaza kuyafanya akiwa amelewa.

Zaidi kuhusu Sonona tunaweza kuelezana baadaye, leo hoja zangu ni mbili.

Kwanza, ni vema jamii ikaanza kuyapa kipaumbele maradhi ya akili, ambayo yapo kwa watanzania wengi. Na athari zake zinaonekana kwenye jamii yetu. Bahati mbaya tunayachukulia maradhi ya akili tofauti sana. Badala ya kwasaidia wagonjwa tunawapa majina ya dhihaka, kama vichaa, mataahira, mtambo, network error', dishi limecheza nk. Pengine watu hawa wangeweza kusaidiwa na kupona, lakini tunapuuza. Baadaye unasikia mtu amejiu, au ameua mke au mume au mtoto na kumkatakata kama nyama ya buchani, ni maradhi ya akili.

Pili, pasina lengo la kumtupia lawama mtu, lakini nathubutu kusema wizara inayohusika na vijana na ajira, imeshindwa kuwasaidia vijana. Tanzania 'imejifungia' chumbani wakati huu wa ulimwengu wa teknolojia na mawasiliano. Kuna fursa nyingi za ajira kwa vijana endapo tutawapa vijana nafasi ya kujipambanua kimataifa. Zipo kazi nyingi za kuingia kipato kupitia mitandao, lakini kwa mifumo ya kifedha ya Tanzania, haziwezekani. Kuna michezo mingi duniani, karibu kila siku kuna mashindano makubwa ya michezo ya kimataifa sehemu fulani duniani, watanzania wamejifungia chumbani.
Yapo mambo mengi mepesi, ambayo vijana wa nchi zingine wanafanya, lakini huwezi kufanya ndani ya Tz kwa sababu za kimfumo.

Tunahitaji mabadiliko makubwa, kwenye mifumo yetu ya elimu, shuleni, vyuoni na mitaani.
Musa, ni mtu mmoja ambaye amefikia kujiua, wapo waliokwisha kujiua na watakaojiua. Lakini athari za Sonona sio kujiua tu, ni pamoja na kuua wengine au kufa bila kujiua. Wengine wanaweza wakabaki hai, lakini wakashindwa kufanya chochote maishani hadi wanakufa.

Let's get up. Tuzungumze kujisaidia na kuwasaidia wengine.
Asante kwa somo kamanda
 
Back
Top Bottom