The Genius
JF-Expert Member
- May 29, 2018
- 828
- 2,109
Kuna mambo yanastaajabisha na kutia hasira sana. Wiki iliyopita Mwenyekiti wa BAVICHA mkoani Kilimanjaro, Lembruce Mchome alikamatwa mkoani Arusha kwa tuhuma za kupiga picha gari ya Mkurugenzi mkuu wa Usalama wa Taifa Kamishna Diwani Athumani Msuya alipokwenda nyumbani kwao Mwanga.
Hayo ndiyo mashtaka aliyofunguliwa kituo kikuu cha polisi Arusha. Lakini baadae alisafirishwa kuja Dar na hakupelekwa mahakamani kwa zaidi ya wiki moja. Leo amepandishwa mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka ya kusambaza picha za ngono mtandaoni. Yani "charge sheet" imebadilika kutoka kupiga picha gari ya DG wa TISS hadi kupiga picha za ngono.
Unaweza kujiuliza hiyo gari ilikua na maudhui ya ngono au camera aliyotumia ilibadilisha picha za gari kuwa za ngono? Funny but not funny. Au unaweza kuwaza pengine kwa wiki moja polisi waliyokaa nae wamejiridhisha kuwa wangemfungulia kesi ya kupiga picha gari ya usalama wa taifa angewashinda. Pengine si jinai kupiga picah gari ya boss wa TISS. Mbona ya IGP inapigwa picha tukikutana mtaani na haijawahi kuwa big deal.
Lakini kama kweli alipiga picha za ngono na ushahidi wanao kwanini hawakumpeleka mahakamani walipomkamata kule Arusha? Kwa nini wakae nae zaidi ya wiki moja mahabusu? Walikua wanajadili nini wakati sheria inasema ndani ya saa 24 mtuhumiwa apelekwe mahakamani?
Na kwanini kosa lifanyikie Mwanga (Kilimanjaro), mtuhumiwa akamatiwe Arusha halafu apandishwe mahakamani Kisutu? Kwanini hakupelekwa Mwanga anakodaiwa kutendea kosa hilo akashtakiwe huko?
Halafu amenyimwa dhamana wakati kosa hilo linadhaminika. Hakimu anasema amemnyima dhamana baada ya mawakili wa serikali kudai kuwa mshtakiwa akiwa nje ataharibu ushahidi. Kesi imeahirishwa hadi tarehe 2 Juni 2020 na Mchome amepelekwa rumande gereza la Segerea.
#Justice4Mchome
......
Malisa GJ
Sent from my SM-N9005 using JamiiForums mobile app
Hayo ndiyo mashtaka aliyofunguliwa kituo kikuu cha polisi Arusha. Lakini baadae alisafirishwa kuja Dar na hakupelekwa mahakamani kwa zaidi ya wiki moja. Leo amepandishwa mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka ya kusambaza picha za ngono mtandaoni. Yani "charge sheet" imebadilika kutoka kupiga picha gari ya DG wa TISS hadi kupiga picha za ngono.
Unaweza kujiuliza hiyo gari ilikua na maudhui ya ngono au camera aliyotumia ilibadilisha picha za gari kuwa za ngono? Funny but not funny. Au unaweza kuwaza pengine kwa wiki moja polisi waliyokaa nae wamejiridhisha kuwa wangemfungulia kesi ya kupiga picha gari ya usalama wa taifa angewashinda. Pengine si jinai kupiga picah gari ya boss wa TISS. Mbona ya IGP inapigwa picha tukikutana mtaani na haijawahi kuwa big deal.
Lakini kama kweli alipiga picha za ngono na ushahidi wanao kwanini hawakumpeleka mahakamani walipomkamata kule Arusha? Kwa nini wakae nae zaidi ya wiki moja mahabusu? Walikua wanajadili nini wakati sheria inasema ndani ya saa 24 mtuhumiwa apelekwe mahakamani?
Na kwanini kosa lifanyikie Mwanga (Kilimanjaro), mtuhumiwa akamatiwe Arusha halafu apandishwe mahakamani Kisutu? Kwanini hakupelekwa Mwanga anakodaiwa kutendea kosa hilo akashtakiwe huko?
Halafu amenyimwa dhamana wakati kosa hilo linadhaminika. Hakimu anasema amemnyima dhamana baada ya mawakili wa serikali kudai kuwa mshtakiwa akiwa nje ataharibu ushahidi. Kesi imeahirishwa hadi tarehe 2 Juni 2020 na Mchome amepelekwa rumande gereza la Segerea.
#Justice4Mchome
......
Malisa GJ
Sent from my SM-N9005 using JamiiForums mobile app