PreGE2025 Jumuiya ya Wazazi CCM Jimbo la Mchinga yadaiwa kumchangia laki moja ya kuchuka fomu Mama Salma Kikwete kugombea Ubunge

PreGE2025 Jumuiya ya Wazazi CCM Jimbo la Mchinga yadaiwa kumchangia laki moja ya kuchuka fomu Mama Salma Kikwete kugombea Ubunge

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Jumuiya ya wazazi ya chama cha mapinduzi CCM Jimbo la Mchinga imemuunga mkono Mbunge wa Jimbo hilo mama Salma Rashid Kikwete kwa kumchangia Fedha kiasi cha shilingi laki moja zitakazomsaidia kwenda kuchukua fomu ya kugombea Ubunge muda utakapofika.

Makabidhiano hayo yamefanyika Katika ofisi ya Jimbo hilo iliyopo Kata ya Mchinga manispaa ya Lindi ambapo wajumbe wa jumuiya hiyo wakaeleza kuwa miongoni mwa sababu ya kumchangia kiasi hiko cha pesa ni kutokana na kazi nzuri alizofanya Mbunge huyo.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Aidha Mama Salma Kikwete ameishukuru Jumuiya hiyo kwa kuthamini kazi anayoifanya Katika kufikisha Maendeleo kwenye Jimbo hilo.

 
Wale hacker wa bybit wa NK si waje wa hack BoT yetu. Bora fedha wafaidi wengine kuliko hawa wakoloni weusi.
 
Back
Top Bottom