Juma P. Makabila.... Singeli limeisha utamu haraka sana...

Jamaa anahisi yeye peke yake ndo anaweza kuimba singeli hataki hata kusikia watunzi wakimshauri kwenye tungo zake.
Sasa subiri watu waanze kusikiliza za wale wengine wakizielewa yeye watamtema baada ya wakati wake wa kutamba ukiisha.Wengine tunatamani libume hata leo,halafu anapenda sans kiki.
 
Kuna siku alitungiwa songi la kuperform mbele ya wageni, mazoezi yameenda vizuri kabisa, sasa muda wa kutumbuiza ulipofika DJ anashangaa vocal haziendani na biti, kuja kushtuka kumbe Juma P Makabila anaimba vitu vyake anatoa kichwani.

Jamaa anamwamrisha ma-DJ, MC, Producers anataka wafanye vile anavyotaka tu yeye, wakikataa anawapiga chini.
 
Kuna siku alitungiwa songi la kuperform mbele ya wageni, mazoezi yameenda vizuri kabisa, sasa muda wa kutumbuiza ulipofika DJ anashangaa vocal haziendani na biti, kuja kushtuka kumbe Juma P Makabila anaimba vitu vyake anatoa kichwani.

Jamaa anamwamrisha ma-DJ, MC, Producers anataka wafanye vile anavyotaka tu yeye, wakikataa anawapiga chini.
Naikumbuka hii show... Watu kidogo wang'oe viti.... Kuna siku atadaiwa Kiingilio huyu.
 
Salam,

Kwanza nikiri kuwa pamoja na kwamba Sikuwa mfuasi wa msanii huyu wa singeli, na wala sikuamini Kama aina yake ya mziki ingetoboa na angetoka.... Lakini kwa Mwaka mmoja wa kwanza tangu Juma Makabila ameanza singeli, nililazimika kuamini kuwa alikuwa anatoka na angetusua.

Akaanza kutafuta Kiki za hapa na pale ili singo zake za mwanzo ziuze... Akapata interview kibao, mpaka akaingia mitandaoni Kama msanii bora wa kiume afrika. Watu tukajua tumeuza.... Zikaja shows na collabo kibao toka kwa majirani zetu wanaocheza aina moja ya mziki.... Makabila akazidi kuwakamata. Mara kidogo katajwa na kituo kikubwa Nigeria, kidogo south, kidogo Marekani..... ikanibidi ni relax nikajua singeli la Makabila lishauza.... Lahaula!!!! Mwaka mmoja ulipoishaaaaa...

Mara show zikakata, collabo za wana zikageuka uadui wakaanza tumtukana na kumsema vibaya... Mara oh! Umeacha singeli unaimba hardcore, Mara umetubadilikia umekuwa matawi.... Loh.
Juzi hapa tukasikia kituo flani sauzi kimemkandia tukajua kwisha habari yetu.

Singeli la Makabila wetu likaisha utamu fastaaaa... Kama takeu ya ndugu yangu mr. Nice.
Ila bado Makabila anahitaji kurudisha singeli lake hewani..... Waungwana tumshauri kwa hekima ana Wakati mgumu ukizingatia garama kubwa alizopoteza kujiweka hapo alipo.
Mshauri juma Makabila singeli lake lirudi hewani.
Baada ya kujiona anajua kuimba aliamua kurusha mic,kumbe sauti yake mbovuuu,ameamua kuitafuta mic kumbe mashabik waliondoka nayo,sasa anapuyanga tuu,na wameanza kumuita Bwana Haambiliki.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom