Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 876
JUMA Nkamia ni Mbunge wa Kondoa Kaskazini (CCM). Kabla ya hapo alikuwa msoma habari na mtangazaji wa mpira katika Shirika la Habari la Taifa (TBC) na baadaye mashirika ya nje ya BBC na VOA.
Kwa utambulisho huo inamaana Nkamia ni mwanafamilia mwenzetu katika tasnia ya habari, japo matendo yake sasa tangu achaguliwe kuwa mbunge yanaonesha kuwa uandishi wa habari haujui au kasahau.
Nkamia amekuwa mtu wa kubwatuka bungeni na kuwasema vibaya waandishi wa habari kana kwamba ni watu masikini, ombaomba wenye kuburuzwa na matajiri kuandika uongo dhidi ya serikali.
Kila akipata nafasi bungeni kuuliza swali kwenye wizara ya habari, vijana, utamaduni na michezo, Nkamia anahoji ni lini muswada wa habari utaletwa bungeni ili kuwadhibiti waandishi makanjanja wanaotumiwa.
Nkamia amefika Ulaya na Amerika kikazi lakini si kweli kwamba hiyo ni sababu ya yeye kujua sana mambo kuliko wanahabari wengine. Ziko sababu nyingi za kufika huko yawezekana hata ikiwa walivutiwa na sauti yake tu.
Lakini tangu amekuwa mbunge Nkamia amekuwa na mtazamo hasi kwa tasnia hii. Anaiona ni ya watu wasiojua, wasio na maadili, wasiolipwa mishahara minono, wasioajirika na mengine mengi.
Kwa uelewa wake huo, kwenye Bunge la bajeti lililopita wakati wa kujadili hotuba ya Wizara ya Habari, Nkamia alilituhumu Baraza la Habari Tanzania (MCT) na Jukwaa la Wahariri kuwa vyombo hivyo vilivyoanzishwa kwa masilahi binafsi ya watu.
Nikiri kwanza kuwa Nkamia hana viwango vya kumjadili kwenye safu hii ya fikra mpya lakini kutokana na kituko alichokifanya wiki hii bungeni nalazimika kumleta kwenu tushauriane masuala kadhaa dhidi yake.
Baada ya wapinzani kutoka nje wakisusia mjadala wa muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2013, Nkamia alikuwa miongoni mwa wabunge wengi wa CCM waliochangia hoja bila kujielekeza kwenye hoja husika (wapiga kelele).
Kwa dakika zake kumi alitumia takribani dakika tano kuonesha umbumbu wake kwenye tasnia ya habari kwa kutojua habari ni ipi kwa wanahabari makini.
Mbunge huyo alianza kwa kujitapa kuwa amefanya kazi ndani na nje ya nchi kwenye mashirika makubwa, kwamba hajawahi kuona wanahabari wa ajabu kama hawa wa Tanzania.
Nkamia akadai kuwa wakati wapinzani wanatoka nje vile vile wanahabari wote waliondoka ukumbini na kuwafuata huko nje. Kwa upeo na maono yake wapinzani hawakuwa na habari bali habari ilikuwa ndani kwa wabunge waliobaki ukumbini.
Akaongeza kuwa kama wamekimbilia kwa wapinzani wataandika taarifa wala si habari. Huyu ndiye mwandishi anayejiita nguli kwenye tasnia, alifanya kazi Ulaya za kusoma habari na kutangaza mpira.
Mpaka naandika safu hii sijamuelewa Nkamia alikuwa analenga kusema nini kwamba habari za kuwapelekea Watanzania ziliachwa ndani ya Bunge halafu wanahabari wanakimbilia nje kuwahoji wapinzani.
Muswada ulisomwa, wabunge wa CCM wakaupigia makofi kwa ishara kwamba wanakubaliana na kile kilicholetwa na serikali yao. Walipoanza kuujadili hakuna aliyejikita kwenye vipengele badala yake wakaanza pongezi, kejeli, kashfa na matusi ya nguoni kwa wapinzani.
Sasa pengine Nkamia kwa uzoefu wake wa kufanya kazi ndani na nje ya nchi, aliona habari ilikuwa wapi hapo ya waandishi kuandika wakati wananchi walikuwa wanataka kujua hasa sababu za wapinzani kutoka nje na kuacha kujadili muswada.
Kimsingi kote kulikuwa na habari lakini zaidi nje walikokwenda wapinzani ndiko kulikuwa kwa muhimu sana kwani wananchi walitaka wajue wawakilishi wao huko walikokwenda imekuwaje.
Na hii ilikuwa ni kazi ya kufanywa na TBC1 ambayo ndiyo inaonesha vikao hivyo moja kwa moja. Lakini kwa utashi wao pengine na maelekezo ya wakubwa waliishia kutuonesha meza ya spika na mawaziri.
Kumbe ulikuwa ni wakati muafaka kwa wanahabari makini kukimbia nje upesi na kuzungumza na wapinzani kupata sababu za msingi zilizowatoa nje pamoja na hatua wanayokusudia kuichukua.
Lakini Nkamia alituambia hiyo ni taarifa si habari. Sipendi kuhoji mwalimu wake kama alimwelewa ila nahoji alikosoma uandishi wa habari kiasi cha kushindwa kutofautisha habari na taarifa.
Kama ilivyo kwa wabunge wengi kutaka wapigiwe makofi wakati wa kuzungumza nadhani hata yeye baada ya kuona hana hoja ya kuchangia kwenye muswada ule aliamua kuwashambulia waandishi ili apigiwe makofi.
Yawezekana Nkamia ni mwanahabari kweli lakini kama matatizo ya wanahabari wenzake hayajui ni vizuri akajielekeza kuzungumzia kero za wapiga kura wake kama wanavyofanya wanahabari wenzake, Ester Bulaya na Lucy Mayenga, ambao wameamua kujiweka mbali na wanahabari. Tafakari!
Kwa maoni yangu
Hii kauli ya Nkamia nadhani inatafuta cheo mahala.Tukae tusubiri kama hata zawadiwa wizara hiyo ya kubana magazeti na waandishi.
Aliingia fomu 6 RTD baadae nadhani alipewa shavu kwenda kusoma.Ni kama walivyo kina Gerson Msigwa na Benjamin Rwegasira.
Kwa utambulisho huo inamaana Nkamia ni mwanafamilia mwenzetu katika tasnia ya habari, japo matendo yake sasa tangu achaguliwe kuwa mbunge yanaonesha kuwa uandishi wa habari haujui au kasahau.
Nkamia amekuwa mtu wa kubwatuka bungeni na kuwasema vibaya waandishi wa habari kana kwamba ni watu masikini, ombaomba wenye kuburuzwa na matajiri kuandika uongo dhidi ya serikali.
Kila akipata nafasi bungeni kuuliza swali kwenye wizara ya habari, vijana, utamaduni na michezo, Nkamia anahoji ni lini muswada wa habari utaletwa bungeni ili kuwadhibiti waandishi makanjanja wanaotumiwa.
Nkamia amefika Ulaya na Amerika kikazi lakini si kweli kwamba hiyo ni sababu ya yeye kujua sana mambo kuliko wanahabari wengine. Ziko sababu nyingi za kufika huko yawezekana hata ikiwa walivutiwa na sauti yake tu.
Lakini tangu amekuwa mbunge Nkamia amekuwa na mtazamo hasi kwa tasnia hii. Anaiona ni ya watu wasiojua, wasio na maadili, wasiolipwa mishahara minono, wasioajirika na mengine mengi.
Kwa uelewa wake huo, kwenye Bunge la bajeti lililopita wakati wa kujadili hotuba ya Wizara ya Habari, Nkamia alilituhumu Baraza la Habari Tanzania (MCT) na Jukwaa la Wahariri kuwa vyombo hivyo vilivyoanzishwa kwa masilahi binafsi ya watu.
Nikiri kwanza kuwa Nkamia hana viwango vya kumjadili kwenye safu hii ya fikra mpya lakini kutokana na kituko alichokifanya wiki hii bungeni nalazimika kumleta kwenu tushauriane masuala kadhaa dhidi yake.
Baada ya wapinzani kutoka nje wakisusia mjadala wa muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2013, Nkamia alikuwa miongoni mwa wabunge wengi wa CCM waliochangia hoja bila kujielekeza kwenye hoja husika (wapiga kelele).
Kwa dakika zake kumi alitumia takribani dakika tano kuonesha umbumbu wake kwenye tasnia ya habari kwa kutojua habari ni ipi kwa wanahabari makini.
Mbunge huyo alianza kwa kujitapa kuwa amefanya kazi ndani na nje ya nchi kwenye mashirika makubwa, kwamba hajawahi kuona wanahabari wa ajabu kama hawa wa Tanzania.
Nkamia akadai kuwa wakati wapinzani wanatoka nje vile vile wanahabari wote waliondoka ukumbini na kuwafuata huko nje. Kwa upeo na maono yake wapinzani hawakuwa na habari bali habari ilikuwa ndani kwa wabunge waliobaki ukumbini.
Akaongeza kuwa kama wamekimbilia kwa wapinzani wataandika taarifa wala si habari. Huyu ndiye mwandishi anayejiita nguli kwenye tasnia, alifanya kazi Ulaya za kusoma habari na kutangaza mpira.
Mpaka naandika safu hii sijamuelewa Nkamia alikuwa analenga kusema nini kwamba habari za kuwapelekea Watanzania ziliachwa ndani ya Bunge halafu wanahabari wanakimbilia nje kuwahoji wapinzani.
Muswada ulisomwa, wabunge wa CCM wakaupigia makofi kwa ishara kwamba wanakubaliana na kile kilicholetwa na serikali yao. Walipoanza kuujadili hakuna aliyejikita kwenye vipengele badala yake wakaanza pongezi, kejeli, kashfa na matusi ya nguoni kwa wapinzani.
Sasa pengine Nkamia kwa uzoefu wake wa kufanya kazi ndani na nje ya nchi, aliona habari ilikuwa wapi hapo ya waandishi kuandika wakati wananchi walikuwa wanataka kujua hasa sababu za wapinzani kutoka nje na kuacha kujadili muswada.
Kimsingi kote kulikuwa na habari lakini zaidi nje walikokwenda wapinzani ndiko kulikuwa kwa muhimu sana kwani wananchi walitaka wajue wawakilishi wao huko walikokwenda imekuwaje.
Na hii ilikuwa ni kazi ya kufanywa na TBC1 ambayo ndiyo inaonesha vikao hivyo moja kwa moja. Lakini kwa utashi wao pengine na maelekezo ya wakubwa waliishia kutuonesha meza ya spika na mawaziri.
Kumbe ulikuwa ni wakati muafaka kwa wanahabari makini kukimbia nje upesi na kuzungumza na wapinzani kupata sababu za msingi zilizowatoa nje pamoja na hatua wanayokusudia kuichukua.
Lakini Nkamia alituambia hiyo ni taarifa si habari. Sipendi kuhoji mwalimu wake kama alimwelewa ila nahoji alikosoma uandishi wa habari kiasi cha kushindwa kutofautisha habari na taarifa.
Kama ilivyo kwa wabunge wengi kutaka wapigiwe makofi wakati wa kuzungumza nadhani hata yeye baada ya kuona hana hoja ya kuchangia kwenye muswada ule aliamua kuwashambulia waandishi ili apigiwe makofi.
Yawezekana Nkamia ni mwanahabari kweli lakini kama matatizo ya wanahabari wenzake hayajui ni vizuri akajielekeza kuzungumzia kero za wapiga kura wake kama wanavyofanya wanahabari wenzake, Ester Bulaya na Lucy Mayenga, ambao wameamua kujiweka mbali na wanahabari. Tafakari!
Kwa maoni yangu
Hii kauli ya Nkamia nadhani inatafuta cheo mahala.Tukae tusubiri kama hata zawadiwa wizara hiyo ya kubana magazeti na waandishi.
Aliingia fomu 6 RTD baadae nadhani alipewa shavu kwenda kusoma.Ni kama walivyo kina Gerson Msigwa na Benjamin Rwegasira.