Julius Malema: Kenya ni koloni la Marekani

Julius Malema: Kenya ni koloni la Marekani

kimsboy

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
11,126
Reaction score
24,419
Kiongozi wa Upinzani Afrika Kusini asema Kenya ni koloni la Marekani, akipigia chapuo Kiswahili

Kiongozi maarufu wa upinzani nchini Afrika Kusini amekosoa vikali safari ya hivi karibuni ya Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya nchini Marekani na mazungumzo yake na rais wa nchi hiyo, Donald Trump.

Julius Sello Malema, ambaye ni kiongozi wa chama cha upinzani cha Economic Freedom Fighters (EFF), ameongeza kuwa, Kenya ni koloni la Marekani na kwamba hakuna 'uhuru kamili' katika nchi hiyo kwani Marekani inadhibiti mambo mengi yanayojiri Kenya.

Aidha amesema kuna haja kwa nchi za bara la Afrika kujikwamua kutoka katika tatizo hilo la ukoloni mamboleo.
Mapema mwaka huu Trump alizitukana nchi za Afrika kuwa ni 'shimo la kinyesi' jambo ambalo lilikosolewa vikali na viongozi wa Afrika.

Kwingineko Malema amependekeza bara la Afrika liungane na liwe na sarafu yake moja kama ilivyo kwa nchi za Ulaya na kutumia lugha moja ya Kiswahili ili kuepuka lugha za kikoloni ambazo zinatumiwa kututenganisha.

Malema aliyasema hayo Agosti 29, 2018 kwenye mkutano na waandishi wa habari ulioandaliwa na chama chake cha EFF kama sherehe ya miaka mitano tangu chama hicho kianzishwe. Aidha alizungumza kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo ujumbe wa Rais wa Marekani kwenye mtandao wa Twitter kuhusu marekebisho ya sheria ya ardhi Afrika Kusini ambapo amesema bara la Afrika haliwezi kukubaliana na Trump ambaye anawatetea Wazungu makaburu waliopora ardhi za Waafrika wazalendo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Malema anapiga siasa tu hamna lolote hapo. Marekani akiamua muokote makopo, mtaokota siku hiyo hiyo. Awaulize Venezuela, Iran, Turkey nk.
Slave mwingine, afrika tuna maadui wazungu design ya akina trump na waafrika design yako, nyinyi ndio sumu ya hatari zaidi. Mtashughulikiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Malema anapiga siasa tu hamna lolote hapo. Marekani akiamua muokote makopo, mtaokota siku hiyo hiyo. Awaulize Venezuela, Iran, Turkey nk.

bila shaka we utakuwa mzungu mweusi unawatetea ndugu zako!!!
 
Malema anapiga siasa tu hamna lolote hapo. Marekani akiamua muokote makopo, mtaokota siku hiyo hiyo. Awaulize Venezuela, Iran, Turkey nk.

Mkuu Iran tokea enzi na enzi wanaishi na vikwazo ,bado wanadunda. Baadhi ya hao wanosifiwa na kupendwa na Marekani ni nchi zisokuwa na maendeleo yoyote ya kutisha.
 
Malema amekasirika toka Trump alipotweet kuwa Afrika kusini wanauawa wazungu na kunyang'anywa mashamba bila kulipwa Trump kamuelekeza Pompey aliangalie hilo swala la Afrika kusini vizuri na atoe taharifa hii imetokea wiki iliyopita mpaka serikali ya Lamaphosa imekutaka na uongozi wa USA hapo Pretoria ili kuweka mambo sawa wanachotegemea SA ni Nchi za Afrika ziungane kuipinga USA sasa hivi Nchi nyingi zinaangalia mambo yao ya ndani wao watatue tatizo lao la Ardhi bila kuingilia Nchi zingine...Malema fanya siasa ya ndani mtatue matatizo makubwa ya rushwa,crime na swala la ardhi...Uhuru asiende USA kisa mna ugomvi na USA akili za wapi hizo...
 
Kiongozi wa Upinzani Afrika Kusini asema Kenya ni koloni la Marekani, akipigia chapuo Kiswahili
Kiongozi maarufu wa upinzani nchini Afrika Kusini amekosoa vikali safari ya hivi karibuni ya Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya nchini Marekani na mazungumzo yake na rais wa nchi hiyo, Donald Trump.
Julius Sello Malema, ambaye ni kiongozi wa chama cha upinzani cha Economic Freedom Fighters (EFF), ameongeza kuwa, Kenya ni koloni la Marekani na kwamba hakuna 'uhuru kamili' katika nchi hiyo kwani Marekani inadhibiti mambo mengi yanayojiri Kenya.
Aidha amesema kuna haja kwa nchi za bara la Afrika kujikwamua kutoka katika tatizo hilo la ukoloni mamboleo.
Mapema mwaka huu Trump alizitukana nchi za Afrika kuwa ni 'shimo la kinyesi' jambo ambalo lilikosolewa vikali na viongozi wa Afrika.
Kwingineko Malema amependekeza bara la Afrika liungane na liwe na sarafu yake moja kama ilivyo kwa nchi za Ulaya na kutumia lugha moja ya Kiswahili ili kuepuka lugha za kikoloni ambazo zinatumiwa kututenganisha.
Malema aliyasema hayo Agosti 29, 2018 kwenye mkutano na waandishi wa habari ulioandaliwa na chama chake cha EFF kama sherehe ya miaka mitano tangu chama hicho kianzishwe. Aidha alizungumza kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo ujumbe wa Rais wa Marekani kwenye mtandao wa Twitter kuhusu marekebisho ya sheria ya ardhi Afrika Kusini ambapo amesema bara la Afrika haliwezi kukubaliana na Trump ambaye anawatetea Wazungu makaburu waliopora ardhi za Waafrika wazalendo

Sent using Jamii Forums mobile app
Wengi tunakubaliana na hili, kwani ulitegemea nini toka kwa manyang'au?!
 
Malema anafaa kuendelea kuwa mwanaharakati ila akishika dola watu watatamani afe, atageuka dikteta mmoja wa kutisha na atafanya mambo ya ajabu sana S.A ataiepeleka shimoni.
Ni mzuri akibaki kuwa mwanaharakati tu na siyo kiongozi mwenyhe mamlaka makubwa
 
Ahaaa haaa haaa

Nilifikiri ni sisi waTanzania ndiyo tunaojua unafiki wa Kenya kuwa kibaraka wa wazungu.
 
Back
Top Bottom