Julio Anaidai Timu ya Simba

Julio Anaidai Timu ya Simba

Amavubi

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2010
Posts
30,156
Reaction score
13,267



Mgombea wa nafasi ya makamu wa urais katika klabu ya Simba amesema anaidai klabu hiyo zaidi ya Sh. milioni 200.

Jamhuri Kihwelo ‘Julio' amesema anadai kitita hicho kilichotokana na kuvunja mkataba wakati akiwa kocha, lakini madai ya mishahara na marupurupu yake.

Tokea enzi za uongozi wa (Hassan) Dalali, Simba ina fedha zangu na hadi leo hawajanilipa. Zaidi ya Shilingi milioni mia mbili, nawadai na hata mzee Dalali analijua hilo, hivyo ninataka kulipwa.

Wasipofanya hivyo sitakuwa na msamaha, nitawapeleka mahakamani, alisema Julio. Julio amechukua fomu za ugombea nafasi ya makamu na kufanikiwa kurejesha kwa wakati mwafaka.

Sasa atapambana na Swedi Nkwabi pamoja na Geofrey Nyange ‘Kaburu'.
 
1. Je alikua anaripoti kazini?
 
Ina maana alikua na waume wawili?



  1. Simba SC
  2. Mwadui ya Shinyanga?
 
Back
Top Bottom