Mhe. Nassari najua wewe ni member wa JF, hivyo natoa ushauri ambao ninapenda pia uuifikishe kwa VIONGOZI wa juu wa CHADEMA/UKAWA.
Kwanza hongera sana kwa kazi nzuri unayoifanya jimboni kwako, kweli CCM hawana chao Arumeru Mashariki. Just for a comparative Jimbo la Arumeru Mashariki ndiyo linalosikika nchi nzima, lakini jimbo DADA la Arumeru Magharbu halisikiki kabisa. WHY? ni kwasababu ya kazi nzuri unayoifanya. I'm sure hata wananchi wa Arumeru Magharbi can borrow a leaf from Arumeru Mashariki na kuwapatia jimbo la Arumeru Magharibi Upinzani mwaka 2015.
USHAURI WANGU kwako Nassari. CCM wana kawaida ya to disfranchise younger voters. Utakumbuka wakati wa uchaguzi uliokupa wewe ushindi wanafunzi wa Nelson Mandela walijitolea fedha zao, kusafiri kutpka makwao kuja Arumeru kukupigia wewe kura. Hivyo tusichukulie haya mambo for GRANTED.
Ninasema CCM wana kawaida ya ku disfranchise younger voters, kwasababu wanajua kwamba younger voters ndiyo BASE ya opposition. Hivyo CCM watafanya all they can do stop them from voting.
Wana disfranchise youngers voters how? wakati wa kuandikisha wapiga kura kwenye daftari la kuduma la wapiga kura NEC hufanya zoezi hilo wakati VYUO na SEKONDARI vikiwa VIMEFUNGULIWA. Maana yake ni kwamba hao wana vyuo na wanafunzi wa sekondari wanatakiwa kupiga kura siku ya uchaguzi mkuu wakiwa vyuoni na sekondari wanakosomea.
Lakini siku ya kupiga kura kwenye UCHAGUZI MKUU, hufanyika wakati vyuo na sekondari vikiwa VIMEFUNGWA. Hili sio suala la bahati mbaya kabisa, it is by design kuhakikiksha kwamba wanawa disfranchise younger voters.
SWALI, langu kwako na kwa viongozi wa CDM, Je mmejiandaa vipi na hii challange ya CCM to disfranchise younger voters ambao ndiyo BASE YENU YA WAPIGA KURA?!
Kutegemea kwamba kila mwanafunzi na mwanachuo atajisafirisha kurudi chuoni na shuleni alikojiandikisha KUWAPIGIA KURA wagombea wa UPINZANI wkati vyuo na mashule yamefungwa is not REALIBALE and SUSTAINABLE. Naomba oppoistion mkune kichwa jinsi ya kutatua changamoto hiyo itakayokuwa created deliberately na NEC kwa maelekezo ya CCM.
Once again ahsante kwa kazi kubwa unayoifanya jimboni kwako.