Joseph Romani Selasini afanya kweli Rombo

Joseph Romani Selasini afanya kweli Rombo

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2015
Posts
14,242
Reaction score
34,917
selasini.jpg


Mbunge wa jimbo la Rombo mkoa wa Kilimanjaro kupitia CHADEMA ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Kilimanjaro JOSEPH ROMAN SELASINI siku ya tar 29/10/2018 amechangia maendeleo ya jimbo lake hilo baada ya kuchangia mifungo 100 ya cement kwa kila kata.

Mh Joseph Roman Selasini ambaye amekua Mbunge wa jimbo hilo tangu mwaka 2010 amekabidhi mifuko hio ya cement kwa madiwan wote wa kata za jimbo hilo. Jimbo la Rombo lina jumla ya kata 28 na kata zote zimenufanika na msaada huo wa mifuko 100 kutoka kwa Mbunge Selasini maarufu kama BABA PAROKO.

Madiwan wa kata zote wamemshukuru sana Mbunge wao kwa msaada huo mkubwa ambao utakua chachu ya maendeleo katika kata zao, aidha madiwani hao mmoja mmoja wamesema Mh Selasini ni mfano mkubwa wa kuigwa na wabunge wengine kwani amekua msaada mkubwa kwa jimbo hilo tangu mwaka 2010 alipokua Mbunge kwa Mara ya kwanza.
Pia Mh JOSEPH ROMAN SELASINI (baba paroko) amewashukuru sana madiwani wa jimbo hilo kwa kazi ambazo wanafanya na ushirikiano mkubwa, vilevile Mh SELASINI amewaomba madiwani hao kuendelea kushirikiana na wananchi ambao wanawatumikia ili kuleta maendeleo chanya ya jimbo zima la Rombo
 
Hongera sana kwa Mbunge wetu,ccm wakiona namna hiyo wanatamani kumnunua kwa gharama yoyote!
 
Kagawa kata zote? Hakubagua kata za CCM na Chadema? Mbona Hawa wengine wanachagua kupeleka maendeleo kwenye CCM tu? Hadi mwenyekiti wao alisema wazi wazi
 
Kagawa kata zote? Hakubagua kata za CCM na Chadema? Mbona Hawa wengine wanachagua kupeleka maendeleo kwenye CCM tu? Hadi mwenyekiti wao alisema wazi wazi
Acha ulofa , rejea maneno ya Msigwa akimshukuru mh rais Iringa
 
View attachment 916065

Mbunge wa jimbo la Rombo mkoa wa Kilimanjaro kupitia CHADEMA ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Kilimanjaro JOSEPH ROMAN SELASINI siku ya tar 29/10/2018 amechangia maendeleo ya jimbo lake hilo baada ya kuchangia mifungo 100 ya cement kwa kila kata.

Mh Joseph Roman Selasini ambaye amekua Mbunge wa jimbo hilo tangu mwaka 2010 amekabidhi mifuko hio ya cement kwa madiwan wote wa kata za jimbo hilo. Jimbo la Rombo lina jumla ya kata 28 na kata zote zimenufanika na msaada huo wa mifuko 100 kutoka kwa Mbunge Selasini maarufu kama BABA PAROKO.

Madiwan wa kata zote wamemshukuru sana Mbunge wao kwa msaada huo mkubwa ambao utakua chachu ya maendeleo katika kata zao, aidha madiwani hao mmoja mmoja wamesema Mh Selasini ni mfano mkubwa wa kuigwa na wabunge wengine kwani amekua msaada mkubwa kwa jimbo hilo tangu mwaka 2010 alipokua Mbunge kwa Mara ya kwanza.
Pia Mh JOSEPH ROMAN SELASINI (baba paroko) amewashukuru sana madiwani wa jimbo hilo kwa kazi ambazo wanafanya na ushirikiano mkubwa, vilevile Mh SELASINI amewaomba madiwani hao kuendelea kushirikiana na wananchi ambao wanawatumikia ili kuleta maendeleo chanya ya jimbo zima la Rombo
Mifuko mia ukigawa kwa kata 28 ina maana kila kata mifuko mitatu ya sementi na nusu inatosha kufanyia kazi gani jamani ni heri angejipanga na kuja upya haitasaidia kitu hiyo.
 
Jambo jema sana hili, ila ingependeza zaidi kama ungetujulisha ujenzi unaoendelea katika kata zote, na kama mahitaji yao yanafanana, au ametoa watajua watazifanyia nini "when the need arise"
 
Mifuko mia ukigawa kwa kata 28 ina maana kila kata mifuko mitatu ya sementi na nusu inatosha kufanyia kazi gani jamani ni heri angejipanga na kuja upya haitasaidia kitu hiyo.
Rudia kusoma tena au hata kiswahili hukijui ?
 
Mifuko mia ukigawa kwa kata 28 ina maana kila kata mifuko mitatu ya sementi na nusu inatosha kufanyia kazi gani jamani ni heri angejipanga na kuja upya haitasaidia kitu hiyo.
Hongera zake mifuko 100 x Tshs.18,500 = 1,850,000/= x kata 28 = Tshs.51,800,000/=
Ni kweli "amefanya kweli"
Huu ndo uhalisia wa maisha siyo kwamba kufanikiwa ni bahati anayoipata mtu ila ni mtazamo unaoongoza maisha yake, hapo juu hao watu wawili ni mfano tosha.

Kwanza wote wametumia hesabu katika suala moja linalofanana, wa kwanza anaona yaliyofanywa bado ingebidi mzee ajipange!! Wa pili yeye pia mbinu iliyotumika ni hesabu lakini yeye kaona mchango ambao umetolewa na kiukweli hicho kiasi si mchezo!!

Jaribu kujitengenezea picha chanya katika kila jambo.

Pongezi ziende kwa Mbunge ni hatua nzuri!!

Nawasilisha!
 
Huu ndo uhalisia wa maisha siyo kwamba kufanikiwa ni bahati anayoipata mtu ila ni mtazamo unaoongoza maisha yake, hapo juu hao watu wawili ni mfano tosha.

Kwanza wote wametumia hesabu katika suala moja linalofanana, wa kwanza anaona yaliyofanywa bado ingebidi mzee ajipange!! Wa pili yeye pia mbinu iliyotumika ni hesabu lakini yeye kaona mchango ambao umetolewa na kiukweli hicho kiasi si mchezo!!

Jaribu kujitengenezea picha chanya katika kila jambo.

Pongezi ziende kwa Mbunge ni hatua nzuri!!

Nawasilisha!
Mkuu Paul Nyuti hakusoma uzi kwa undani. yeye ameelewa kuwa, Mbunge katoa mifuko 100 kwa kata zote 28 kumbe sio hivyo! alitoa mifuko 100 kwa kila kata, na kata ziko 28 kwa kiswahili chepesi, kila kata imepata mifuko 100 ya cement au tuseme mifuko ya cement kwa ujumla wake kabla ya kugawiwa kwenye kata ilikuwa ni mifuko 2,800. kwa hiyo ukichukua 2,800/kata 28 kila kata ilipata mifuko 100.
 
Hongera Zake Ila kila wakati mtakuwa mnatangaza?
 
Back
Top Bottom