Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,917
Mbunge wa jimbo la Rombo mkoa wa Kilimanjaro kupitia CHADEMA ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Kilimanjaro JOSEPH ROMAN SELASINI siku ya tar 29/10/2018 amechangia maendeleo ya jimbo lake hilo baada ya kuchangia mifungo 100 ya cement kwa kila kata.
Mh Joseph Roman Selasini ambaye amekua Mbunge wa jimbo hilo tangu mwaka 2010 amekabidhi mifuko hio ya cement kwa madiwan wote wa kata za jimbo hilo. Jimbo la Rombo lina jumla ya kata 28 na kata zote zimenufanika na msaada huo wa mifuko 100 kutoka kwa Mbunge Selasini maarufu kama BABA PAROKO.
Madiwan wa kata zote wamemshukuru sana Mbunge wao kwa msaada huo mkubwa ambao utakua chachu ya maendeleo katika kata zao, aidha madiwani hao mmoja mmoja wamesema Mh Selasini ni mfano mkubwa wa kuigwa na wabunge wengine kwani amekua msaada mkubwa kwa jimbo hilo tangu mwaka 2010 alipokua Mbunge kwa Mara ya kwanza.
Pia Mh JOSEPH ROMAN SELASINI (baba paroko) amewashukuru sana madiwani wa jimbo hilo kwa kazi ambazo wanafanya na ushirikiano mkubwa, vilevile Mh SELASINI amewaomba madiwani hao kuendelea kushirikiana na wananchi ambao wanawatumikia ili kuleta maendeleo chanya ya jimbo zima la Rombo