Kipala
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 3,763
- 700
Samahani kaka historia yako ina udhaifu kidogo.Kihistoria ya siku za karibuni, hicho kipande cha dunia kimekuwa kikibadilishwa jina na kutawaliwa na watu mbali mbali. Mfano hii hapa chini ni bendera ya nchi iliyokuwa inaitwa "The British Mandate for Palestine" ambayo ndiyo iligeuzwa na kuitwa Israel ya sasa (mwaka 1948). Kabla ya hapo ilitawaliwa na Waturuki (ilikuwa ni sehemu ya Ottoman Empire). Ila siku zote wakazi wake asilia ni Wayahudi + pockets za Waarabu
A) Palestina ya Kiingereza haikuendelea kama dola la Israel. Iligawiwa na Umoja wa Mataifa kuwa sehemu 2: ya kiyahudi (>Israel) na ya Kiarabu (iliyotwaliwa baada ya vita ya 1948 na Misri = Gaza na Jordani=sehemu magharibi ya mto Jordan). ling. United Nations Partition Plan for Palestine - Wikipedia, the free encyclopedia
B) Kuhusu wakazi asilia: sehemu hizi hakuna "asilia" kwa maana hii yaani katika historia ndefu wenyeji walibadilisha utamaduni na dini mara kadhaa. (Waarabu Wapalestina wengi wa leo ni wajukuu wa Wayahudi wa siku za Yesu waliokuwa Wakristo baadaye halafu Wasilamu na kutumia Kiarabu)
Kabla ya 1914 wakazi wengi walikuwa Waarabu (Waislamu na Wakristo) pamoja na Wayahudi wachache ("pockets" ukipenda).
Tangu uhamiaji wa Kizionisti idadi ya Wayahudi iliongezeka polepole hadi kufikia 1/3 ya wakazi maana idadi ya wayahudi ilikuwa nusu ya Waarabu mwaka 1947.
C) Wakati wa vita ya 1947/48 Waarabu walifukuzwa au kukimbia ni wachache waliobaki kama 15% za wakazi wa nchi ya Israel.
D) Idadi hii ya raia Waarabu ndani ya Israel imeongezeka kuwa karibu 25% kwa sasa wengine Wayahudi au wenye asili ya Kiyahudi.
E) Nje ya hayo Waarabu wanaoishi katika sehemu za Kipalestina chini ya utawala wa Kijeshi wa Israeli na kanda la Gaza.