Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Baada ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche kueleza kuwa Akaunti za chama za X (Twitter) na YouTube zimechukuliwa na John Mrema na kudai alikuwa akipata faida binafsi kupitia mitandao hiyo ya chama, Mrema ametoa ufafanuzi upande wake.
John Mrema ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa CHADEMA amezungumza na JamiiForums kuhusu tuhuma hizo na kueleza kuwa hazina ukweli.
Kusoma alichokisema John Heche, bofya hapa ~ John Heche: John Mrema amekimbia na Akaunti za YouTube na X za Chama, tuligundua kila wiki analipwa Tsh. Milioni 3
JOHN MREMA: WANANICHAFUA, SIKUWA HATA NA PASSWORD YA MITANDAO YAO
Hizo taarifa sio za kweli na hata wao (CHADEMA) wanajua sio kweli, ni propaganda tu, mimi nilikuwa mkuu wa kitengo lakini sikuwa na ‘access’ ya kupost chochote, kuna vijana ambao ndio walikuwa wanafanya hiyo kazi na ndio ambao wapo nao mpaka sasa.
Sina hata password ya hizo akaunti wanazozitaja, nilipokuwa nikitaka kupost taarifa, niliandaa na kuwapa vijana hao waiposti, hata Katibu Mkuu naye alifanya hivyohivyo, sisi hatukuwa watu wa kuposti hata mara moja.
Ukitaka kuamini hilo, mimi niliondoka Januari 2025 lakini hadi Aprili 2025 akaunti zilikuwa zinafanya kazi na walikuwa wakizitumia wao (Uongozi uliopo madarakani kwa sasa), kilichotokea kwa taarifa nilizonazo ni kuwa…
Siku ambayo Mwenyekiti wa Chama chao anakamatwa kulifanyika majaribio kadhaa ya kuingia kwenye akaunti ya Twitter (X) kwa kukosea, hivyo akaunti ifungiwa kwa muda na taarifa kutumwa katika email iliyotumika kufungulia hiyo akaunti.
Hilo wanalijua na walielezana kwenye vikao, Mnyika anajua, Heche anajua na Apolo ambaye alikuwa na access na hiyo akaunti anajua.
Kuhusu YouTube ambayo ilikuwa inaendeshwa na Abulkarim ambaye ana madai yake, akawaeleza wamlipe, Heche akamwambia hayo madai yake ni makubwa wataangalia namna.
John Mrema ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa CHADEMA amezungumza na JamiiForums kuhusu tuhuma hizo na kueleza kuwa hazina ukweli.
Kusoma alichokisema John Heche, bofya hapa ~ John Heche: John Mrema amekimbia na Akaunti za YouTube na X za Chama, tuligundua kila wiki analipwa Tsh. Milioni 3
JOHN MREMA: WANANICHAFUA, SIKUWA HATA NA PASSWORD YA MITANDAO YAO
Hizo taarifa sio za kweli na hata wao (CHADEMA) wanajua sio kweli, ni propaganda tu, mimi nilikuwa mkuu wa kitengo lakini sikuwa na ‘access’ ya kupost chochote, kuna vijana ambao ndio walikuwa wanafanya hiyo kazi na ndio ambao wapo nao mpaka sasa.
Sina hata password ya hizo akaunti wanazozitaja, nilipokuwa nikitaka kupost taarifa, niliandaa na kuwapa vijana hao waiposti, hata Katibu Mkuu naye alifanya hivyohivyo, sisi hatukuwa watu wa kuposti hata mara moja.
Ukitaka kuamini hilo, mimi niliondoka Januari 2025 lakini hadi Aprili 2025 akaunti zilikuwa zinafanya kazi na walikuwa wakizitumia wao (Uongozi uliopo madarakani kwa sasa), kilichotokea kwa taarifa nilizonazo ni kuwa…
Siku ambayo Mwenyekiti wa Chama chao anakamatwa kulifanyika majaribio kadhaa ya kuingia kwenye akaunti ya Twitter (X) kwa kukosea, hivyo akaunti ifungiwa kwa muda na taarifa kutumwa katika email iliyotumika kufungulia hiyo akaunti.
Hilo wanalijua na walielezana kwenye vikao, Mnyika anajua, Heche anajua na Apolo ambaye alikuwa na access na hiyo akaunti anajua.
Kuhusu YouTube ambayo ilikuwa inaendeshwa na Abulkarim ambaye ana madai yake, akawaeleza wamlipe, Heche akamwambia hayo madai yake ni makubwa wataangalia namna.
