Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Your browser is not able to display this video.
Mnyika amesema mambo hayo yanafanyika kutaka kukitoa chama kwenye ajenda yao ya NO REFORM NO ELECTION.
Amesema hayo leo tarehe 25 Machi 2025 wakati akifungua mafunzo ya uongozi kwa viongozi wa BAWACHA na BAVICHA kutoka Kanda ya Kusini. Mafunzo hayo yanafanyika Masasi, mkoani Mtwara. Katibu Mkuu amembatana na Mkurugenzi wa Mafunzo, Oganaizesheni na Uchaguzi John Pambalu katika mafunzo hayo.
Ikumbukwe, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imetoa muda wa Wiki moja kufikia Machi 31, 2025 kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwasilisha maelezo kuhusu malalamiko ya mjumbe wa Baraza Kuu wa Chama hicho, Lembrus Mchome.
Lembrus Mchome ambaye ni Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Mwanga, alimuandikia barua Msajili wa Vyama vya Siasa kufanya uchunguzi juu ya uhalali wa Kikao cha Baraza Kuu la chama hicho kilichofanyika Januari 22, 2025 na kumpitisha John Mnyika kuwa Katibu Mkuu wa Chama.
Mchome alisema kwa utaratibu wa Chama, wanaoshiriki Baraza kuu ni Wajumbe pekee na sio wawakilishi lakini siku ya Baraza kuu palikuwa na Watu ambao si wajumbe na walishiriki kupiga kura.