BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 654
- 1,598
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali maombi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliotaka kuruhusiwa kuendelea na shughuli za kisiasa, baada ya zuio lililowekwa kutokana na kesi ya mgawanyo wa mali za chama hicho.
Akizungumza baada ya uamuzi huo Agosti 18, 2025, Wakili wa CHADEMA, Hekima Mwasipu, amesema walitarajia Mahakama ingetengua amri ya awali ya Juni 10, 2025, iliyozuia Bodi ya Wadhamini na Katibu Mkuu wa chama hicho kufanya shughuli za kisiasa pamoja na matumizi ya mali za chama.
Soma Pia: Mahakama yatupilia mbali maombi ya bodi ya wadhamini CHADEMA. Kesi yapigwa tena Kalenda hadi Agosti 28
Ameongeza kuwa, baada ya amri hiyo, mawakili waliwasilisha maombi mapya wakiiomba Mahakama itengue uamuzi huo kwa maelezo kuwa haukuzingatia misingi ya kisheria na kwamba wateja wao hawakupata haki ya kisheria ipasavyo, hata hivyo, maamuzi yamekuja vinginevyo.