John Heche hamia ACT Wazalendo

Shocker

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2012
Posts
2,175
Reaction score
4,179
Kama kuna mtu ndani ya CHADEMA mwenye uwezo wa kuwa Rais na kuleta mabadiliko ya kweli, basi ni John Heche.

Anaongea mambo ya msingi sana hoja zake ni za kisiasa, zenye uzito, na zinawagusa wananchi moja kwa moja. Lakini changamoto yake kubwa ni kuwa yupo pahala pasipo, yaani mazingira aliyonayo sasa yanamzuia kung'ara ipasavyo.

Kutokana na hilo, mara nyingine analazimika kuzungumza kwa kufuata upepo wa kisiasa, badala ya kusimamia ukweli wake. Hata hivyo, akipata nafasi ya kutulia na kuongea kwa uhuru, anaibomoa CCM kwa hoja nzito kabisa.

Kwa upande mwingine, kama kuna mtu ambaye ameathiri maisha ya watu wengi kwa namna mbaya kisiasa, basi ni Tundu Lissu. Amevunja matumaini ya watu wengi waliomwamini. Kwa hiyo, kama siasa ni safari ya matumaini, basi kwa wengi bora wahame njia hiyo.

John Heche, jiunge na Zitto Kabwe. Kuna kitu ndani yangu kinaniambia nyie wawili mkishikamana, mnaweza kushinda uchaguzi.
 
Hahahaaa. Sio CHAUMMA? CHAUMMA CHA UPEPO, UKIPITA NACHO KINAPOTEA
 
Mbona Zanzibar CUF/ACT walishinda chaguzi zote za vyama vingi ?
Kilichowanyima ushindi wao sio Tume na kama mnakumbukumbu sio madodosa ,
Habari ya ushindi iliwahi kutangazwa Shirika la habari la Tanzania Daresalaam .
Kilichotokea ni Alhaji Kikwete kutua Zanzibar na kuangamiza waislamu wenzake kwa kutumia Jeshi sijui atafanya wema gani aingie filjannah maana zulma katika uislamu hukumu yake nyingine kabisa ,lazima uliemzulumu akusamehe.

Mara mbili baada ya ushindi Wazanzibari walitaka kukinukisha ,ila ni wachache sana ukilinganisha na Tanganyika hivyo waliamua kukaa kimya. Ila ukweli huo hakuna mtu asieujua wala kuusikia.

Huku Tanganyika wananchi ni wengi kuliko police kikinuka hakizimiki. kwa kama wakizunguuka Unguja Mjini umemaliza na ndio ukaona Wananchi wa Zanzbar walizunguukwa na polisi isipokuwa Pemba ambako polisi wa ziada waliagizwa kutoka Tanganyika ,WaTanganyika mlikaa kimya ,wacha leo yawakute.

Kosa kubwa la Lisu ni kutaka kukinukisha wakati sio ndio nikaamini kama alitumika au kutumiwa na CCM hawa akina Lema wanacheza ngoma wasioielewa au wasio na ufundi nayo.

Sasa wachaneni na Lisu Heche na wengine wahamie ACT subiri uchaguzi subiri matokea ,harafu ibainike CCM wamekwiba hapo ndio kitanuka. Lisu anatumika kuiuwa Chadema na mwisho atafungwa mwezi mmoja na kuachiwa na yeye ataishukuru serikali kwa kumsamehe. Kazi aliyotumwa ameimaliza. msemo wetu 1979 baada ya kumtoa nduli Nje ya Uganda kazi mliyotutuma tumeimaliza.
Mahesabu ya CCM makubwa lisu amehudhuria kesi kanenepa mlio nje mnachezea virungu.
Pale mahakamani anatoa ujeuri anaicheza ngoma inavyopigwa.
 
No Reforms No Election
 
heche is overrated

yeye ni comparison politics,which a stupid dude can do

maybe uniambie zitto,ameliamsha na IPTL,hizo ndio siasa sio hizi soga!

tatizo heche IQ ndogo
 
Nani kakutuma?.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…