John Boko aangaliwe nidhamu yake

poposindege

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
453
175
mwananchi.jpg
Nimeamua kuandika walau kwa uchache baada ya kuona na kufuatilia nidhamu ya Kapteni wa timu ya Azam FC, John Boko tangu alipokumbwa na tukio la kudhalilishwa na Juma Nyoso wa Mbeya City.

Boko kama kapteni anatakiwa aoneshe nidhamu zaidi na kuwa mfano kwa wengine. Nimemuangalia katika mechi kadhaa yeye ndiye amekuwa mfano mbaya wa mtu asiye na nidhamu.

Mechi ya jana kati ya timu yake ya azam Fc na Yanga amedhihirisha hilo kwa kupewa kadi nyekundu baada ya kuonywa na kadi ya njano awali kwa mchezo usio wa kiungwana.

Ukifuatilia mchezo wa jana baada ya kuchezewa rafu na Juma Abdul wa Yanga, Boko alionesha kulipiza kwa kumchezea Juma rafu tatu za makusudi kitu ambacho hakikuwa Fair.

Baadae akaingia katika purukushani na Kelvin Yondani kiasi cha kutemeana mate na kurushiana ngumi.

Ni kweli yondani alimtemea mate Boko lakini naye baadae akamtemea mate na kumpiga ngumi.

Tuwe wakweli John Boko kwa muda mrefu nidhamu yake imekuwa si nzuri lakini wengi wamekuwa hawamzingatii. Boko hana tofauti na mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa.

Baadhi ya wachezaji wamekuwa wakilalamika kutukanwa au kusemewa maneno ya hovyo na Boko pale wanapopambana nae. Na hili hata Nyosso amelilalamikia.

Boko alimkita mguu Nyosso kwa makusudi kabisa. Siungi mkono kitendo cha Juma Nyosso lakini anagalia mazingira kabla hajafanya tukio hilo.

John Boko kwa nafasi yake kama mshambuliaji na kapteni wa timu fuatilia kadi alizopewa mpaka sasa.

Boko ni mchezaji mzuri na mwenye kipaji anahitaji kubadilika kuwa mfano wa kuigwa kama kapteni wa timu.
 
Last edited:
Mkuu next time ukiandika vitu kama hivi
sema 'shambulio la aibu'
au 'shambulio la kudhalilisha'

tumia lugha sahihi....
 
Kwa matendo ya mchezo usio wa kiungwana anayoyafanya Kelvin Yondani, ndie alitakiwa kuwa mchezaji mwenye kadi nyekundu nyingi, akifuatiwa na Juuko wa Simba lakini wote huwa hawaadhibiwa kabisa.
 
mi goli lile tuuu watangazaji wa azam walikuwa na kigugumizi hasa mvulla ,hakuwa fair kuajiriwa kunatufanya tusiwe na uhuru ktk kazi zetu jmn
 
Uwanjani kuna mambo mengi sana. Kama hapo bocco alifanya kusudi aisee.
 
Azam wakiwa wanacheza na Simba au Yanga wanacheza bila nidhamu,wanatembeza viatu balaa,na kwenye mechi kubwa za simba na yanga kocha huwaweka wanaocheza rafu,kasumba hii wamekuwa pia wanaitumia hata kwenye timu ya taifa hatimaye algeria akatupiga mkono
 
Kama ambavyo tuliona baada ya Bocco kutolewa angalau kukawa na utulivu uwanjani. Yule jamaa anatakiwa akuwe
 
Tena Boko mstaarabu sana ningelikuwa mimi ningempa za chemba na za uso huyo Jondani wenu.
 
Boko toka ashituliwe na nyoso, ss hvi kila mara anataka tu, hatulii uwanjani, nyoso kamharibu sana
 
Kahusu Nyoso si aliwahi kumwelekezea Kidole Boko kwenye sehemu isiyo husika. Labda Boko analipa kisasi Kwake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom