NewDawnTz
JF-Expert Member
- Nov 15, 2010
- 1,667
- 362
Kwa wale watazamaji wa ITV au Channel-e ya South Africa watakuwa wanafahamu kipindi maarufu cha mwanasheria anaendesha kesi nje ya majengo ya mahakama (Street Court)....inarahisisha badala ya watu kubanana mahakamani
JK nae ameanza....Sasa ana aina falsafa mpya ya kuiongoza serikali yake...Street Governenace....Hataki kubanwa na kuta kwa mujibu wa taratibu za vyombo vilivyopo.........Anatawala nchi akiwa mitaani....anaongoza serikali mitaani na kwenye vyombo vya habari...Ndivyo ninavyomuona
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka chombo kimoja muhimu san kinachoitwa Baraza la Mawaziri. Pamoja na mapungufu yake, katiba hii kuanzia Ibara ya 54 mpaka ibara ya 59 inaunda rasmi baraza la mawaziri kama chombo kikubwa cha msaada wa karibu kwa utendaji kazi wa Raisi.
Kimantiki, japo si mtaalamu wa Sheria, baraza la mawaziri linaloundwa na mawaziri wote ndiyo sehemu ya Raisi kukaa na mawaziri wake, kujadili utekelezaji wa majukumu mbalimbali ikiwamo usimamizi wa sheria pamoja na namna ya uendeshaji uchumi ikiwamo pia kutoa maazimio na msimamo wa Raisi ambao mawaziri wanapaswa kwenda kutekeleza baada ya kikao cha baraza la mawaziri
Ninapoangalia ziara za Raisi na maagizo yake wizarani, anavyoshushua mawaziri wake kana kwamba yeye ni MWENYEKITI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI, na jinsi baraza lake linavyotofautiana na kujichanganya naanza kuhoji kama nchi hii ina BARZA LA MAWAZIRI.....
Hata hivyo huwa wanakaa vikao vya baraza la mawaziri, Hivi huwa wanafanya nini huko kwenye baraza la mawaziri? Au ni kuijadili CHADEMA tu? Kama sivyo, mbona maagizo ya Kikwete yanaonekana angepaswa kuyatoa kwenye baraza la mawaziri na sio akitembelea wizarani? Je hizi wizara atazitembelea kila mwezi au kila baada ya miezi mitatu? Je hayangekuwa na uzito kama angeyatolea kwenye Baraza la Mawaziri zaidi ya kuyatolea mitaani?
Sikatai wajibu wa Raisi kutembelea wizara, ila ninachohoji ni madhumuni yake na kule kushushua na kuagiza ambako angepaswa kufanya ndani ya baraza la mawaziri
Hayay yote yananifanya niwaze hivi
Achana na "Street Governance" na tumia baraza lako la mawaziri
JK nae ameanza....Sasa ana aina falsafa mpya ya kuiongoza serikali yake...Street Governenace....Hataki kubanwa na kuta kwa mujibu wa taratibu za vyombo vilivyopo.........Anatawala nchi akiwa mitaani....anaongoza serikali mitaani na kwenye vyombo vya habari...Ndivyo ninavyomuona
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka chombo kimoja muhimu san kinachoitwa Baraza la Mawaziri. Pamoja na mapungufu yake, katiba hii kuanzia Ibara ya 54 mpaka ibara ya 59 inaunda rasmi baraza la mawaziri kama chombo kikubwa cha msaada wa karibu kwa utendaji kazi wa Raisi.
Kimantiki, japo si mtaalamu wa Sheria, baraza la mawaziri linaloundwa na mawaziri wote ndiyo sehemu ya Raisi kukaa na mawaziri wake, kujadili utekelezaji wa majukumu mbalimbali ikiwamo usimamizi wa sheria pamoja na namna ya uendeshaji uchumi ikiwamo pia kutoa maazimio na msimamo wa Raisi ambao mawaziri wanapaswa kwenda kutekeleza baada ya kikao cha baraza la mawaziri
Ninapoangalia ziara za Raisi na maagizo yake wizarani, anavyoshushua mawaziri wake kana kwamba yeye ni MWENYEKITI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI, na jinsi baraza lake linavyotofautiana na kujichanganya naanza kuhoji kama nchi hii ina BARZA LA MAWAZIRI.....
Hata hivyo huwa wanakaa vikao vya baraza la mawaziri, Hivi huwa wanafanya nini huko kwenye baraza la mawaziri? Au ni kuijadili CHADEMA tu? Kama sivyo, mbona maagizo ya Kikwete yanaonekana angepaswa kuyatoa kwenye baraza la mawaziri na sio akitembelea wizarani? Je hizi wizara atazitembelea kila mwezi au kila baada ya miezi mitatu? Je hayangekuwa na uzito kama angeyatolea kwenye Baraza la Mawaziri zaidi ya kuyatolea mitaani?
Sikatai wajibu wa Raisi kutembelea wizara, ila ninachohoji ni madhumuni yake na kule kushushua na kuagiza ambako angepaswa kufanya ndani ya baraza la mawaziri
Hayay yote yananifanya niwaze hivi
- Yawezekana ni katika kutafuta huruma ya watanzania kuwa yeye ni mchapakazi ila watendaji wake wanamuangusha na ndio maana anaona akitoa kwenye baraza wananchi hawatamuona "live" zaidi tu ya kusikia kwenye media.....Je ameshapima tija kati ya umaarufu na ziara zake na ulegevu katika utendaji? Naona zinaleta umaarufu zaidi kuliko tija kwa jinsi zinavyoendeshwa
- Yawezekana kwenye baraza la mawaziri hakuna kuelewana kuna mgawanyiko na LABDA Mh. ni mdhaifu kutoa kauli yenye busara yenye kukata maneno na itakayofuatwa na wote
- Au ameamua kuua rasmi baraza la mawaziri kwa kutoendesha hoja zenye msingi na PIA INAONEKANA HAPOKEI TAARIFA ZA UTENDAJI WA WIZARA KWENYE BARAZA LAKE
Achana na "Street Governance" na tumia baraza lako la mawaziri