Ili kuwahakikishia juu ya hili wiki mbili zilizopita baraza la madiwani la bukombe lilikwenda katika eneo la tukio na mwandishi wa habari wa mwanaharisi kuhoji uhalali wa kampuni hiyo kuwepo katika eneo hilo. Wahusika walisema mmiliki anaishi NETHERLAND na mmoja ni mtanzania ambae waligoma kumtaja. Kampuni inayojihusisha na kazi hiyo inaitwa TANCAN. Mbunge aliyepita amekuwa akionekana mara kwa mara katika eneo hilo, pia Lidhiwani Kikwete amekuwa akifika Bukombe mara kwa mara. lakini hufikia Kahama kwenye hotel ya RIVERMARK na kuigia Bukombe kwa siri. Pia hakuna kiongozi aliyehoji juu ya hili isipokuwa madiwani tu, hii ni wazi watu hawa wanahusika. lakini kwa vile liko mezani kwa mwanahalisi ukweli ujulikana tu.
Ninaomba wanaoweza kufuatilia wachunguze madai haya na kuleta data hadharani. Vi inzi mpo?Kwa kifupi ni hivi, kampuni ya utafiti ya Tancan mining ambayo ina leseni ya
utafiti katika msitu wa kigosi imeanza kuchimba dhahabu kimya kimya kwa
kushirikiana na mafisadi wazoefu katika nchi hii. Wanaotajwa katika scandal hii
ni Rostam na Ridhiwani kikwete. taarifa zisizo rasmi zinasema Ridhiwan huwa
anaenda kuchukua mzigo (dhahabu) kwa siri kutoka Bukombe nyakati za usiku.
Maswali ya kujiuliza ni je lini serikali imetangaza kuwa Tanzania ina mgodi
mwingine hata kama ni mdogo kiasi gani unazalisha dhahabu? Na ilikuwaje mpaka
Ridhiwan either mara zote au siku moja moja awe ndio mbebaji wa hiyo dhahabu
kuitoa msituni?
uKWELI NI KWAMBA MMILIKI NINJOSEPH KAHAMA KWA TITLE YA PRESIDENT DIRECTOR
inashangaza mpaka sasa thread ya kijinga kama hii haijafutwa. Mtu anaamka tu huko alikotoka anaandika upuuzi kabisa. Nasema ni upuuzi kwa sababu hakuna ushahidi wala maelezo yoyote yenye mantiki. Inakuwa kama anawaletea mada watu wa vijiweni. Si mbaya mtu kuleta habari, ila leta basi na proof. Lakini habari tu mara ooh riziwani anakwenda usiku kubeba mzigo ni maneno ya hovyovhoyo kabisa.
Napita tu wakuu
hakika inashangaza kuona kwamba muda wote huu tuna-entertain pumba za ng'ombe huyu. Kilichomo humu ni uvumi na speculation za kipuuzi ambazo hazipaswi kupewa nafasi katika dunia ya leo. Eti mtu anatoa tuhuma then anazama msituni kutafuta namna ya kuhalalisha ukweli wa tuhuma na hata hivyo anashindwa. Hakuna ushahidi wowote zaidi ya ule wa kwamba tancan ndiyo wamiliki wa hicho kinachoitwa mgodi na shareholders wa kampuni hiyo, nje na ndani wanafahamika. Sasa leo mtu anakurupuka na michuki yake na kuanza kuingiza jina la rais bila hata kufanya utafiti, na kuhisi kwamba eti ridhiwan anakwenda usiku. Hivi ana sababu ya kwenda usiku kweli wakati angeweza kutuma tu watu wakamletea mzigo huo tena akiwa sebuleni kwake dar?
Watu wajue kwamba humu jf kuna watu werevu kuliko huyu ng'ombe na kwa hiyo anapokuja na uvumi na porojo zake watu wataona kwamba huu ni mzaha ambao haustahili hata kupewa muda wa kusikilizwa. Ifike wakati tuwe responsible kwa matamshi yetu na siyo wewe kuonekana champion kwa kujaza ma-thread ya uongo na kutafuta sifa. Kila aliyechangia humu ameona kwamba thread hii ni kamba kama lilivyo jina lake na kwa kweli huyu ng'ombe ana bahati kwamba thread hii bado inaendelea kuishi!
riziwani alisoma masters hull university uk lakini mungu akumjalia kufaulu, kwa hiyo amerudi bila cheti. kama dr bana angekuwa anafundisha hull university basi riziwani lazima angefaulu maanake dr bana ni mwalimu mzuri sana.Hakuna mzalendo kama jk. Hakuwahi somesha mwanae nje ya nchi
Ndugu watanzania naomba mjue viongozi wetu walivyo wezi, jk na aliyekuwa mbunge wa bukombe (2005-2010) wanamiliki mgodi wa dhahabu ndani ya hifadhi ya Taifa ya KIGOSI kinyume na utaratibu. Hakuna kiongozi wa wilaya wala mkoa aliyekemea swala hilo, hata waziri wa maliasili na utalii anayetamba kusafisha wizara hiyo yuko kimya katika suala hilo.Wananchi wa kawaida wakikata kuni tu tatizo, naomba viongozi wa serikari, siasa, kidini, wanajf na wananchi wote tulisemee suala hili ili waondoke katika hifadhi hii kwa amani kabla nguvu ya umma haijawatoa kwa aibu.