JK Brigde: Bei 805bn ni sahihi?

Kwa wale wasiojua, hizo shilingi bilioni 850 zinaweza jenga barabara nyingine ya lami kutoka Dar hadi Shinyanga. Hesabu hii itakuwa imekosewa na mtoa mada. Na kama ni kweli basi sasa tunaibiana kwa lazima!!!????
 
Michael-Jordan-Christopher-Reid-Will-Smith-DJ-Jazzy-Jeff-and-Christopher-Martin.jpg



I just love these days
Naona U great thinker unanipiga chenga hapa.
Kuna uhusiano gani kati ya hii picha ,Tshs 805bn na JK, naomba mtoa post atueleweshe kabla brain yangu sijaipeleka kupark!
 
Habari hii ni ya Gazeti la Uhuru la Chama Cha Magamba (CCM), hebu isome kisha linganisha na habari iliyoandikwa na Habari Leo.

JK akemea wahandisi
WEDNESDAY, 06 JULY 2011 10:38 NEWSROOM


Na Fadhili Abdallah, Kigoma
RAIS Jakaya Kikwete amesema serikali itawachukulia hatua wahandisi washauri wanaoshindwa kuwasimamia ipasavyo makandarasi wa ujenzi wa barabara. Kiongozi huyo pia amewataka Watanzania kusali ili kuhakikisha amani iliyopo nchini inadumishwa kwa ajili ya maendeleo. Rais alisema hayo mjini hapa jana, kwa nyakati tofauti alipozindua ujenzi wa daraja la mto Malagarasi, na alipokuwa akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Kidahwe –Uvinza, yenye urefu wa kilomita 76, inayojengwa kwa kiwango cha lami na kampuni ya Chico ya nchini China. Alisema hatua ya wahandisi hao kushindwa kusimamia kazi kikamilifu imekuwa ikisababisha hasara kubwa kwa serikali, huku barabara nyingi zikijengwa chini ya kiwango. Rais Kikwete akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Kidahwe hadi Uvinza juzi, alisema tatizo la ujenzi chini ya kiwango halitokani na makandarasi pekee, bali ni matokeo ya usimamizi mbovu unaofanywa na wahandisi washauri.

Kuhusu kudumishwa amani, alisema kuvurugika kwake kutakuwa na athari kubwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ukiwemo wa daraja la Malagarasi. Alisema miradi ya barabara na madaraja imekuwa ikitumia mabilioni ya fedha za ndani na nje ya nchi kutoka kwa wahisani, hivyo kuvurugika amani kutawafanya wahisani kusita kutoa fedha za kutekeleza miradi. Rais alisema ametimiza ndoto aliyoingia nayo Ikulu mwaka 2005, kuhusu kuanza ujenzi wa daraja la mto Malagarasi, ambalo lilikuwa kero kubwa kwa wananchi.Alisema makandarasi wamemhakikishia mradi huo utakamilika ndani ya kipindi cha miaka mitatu, na litaleta ukombozi kiuchumi kwa wananchi wa mkoa wa Kigoma.

Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, alisema sh. bilioni 85 zitatumika katika utekelezaji wa mradi huo, gharama ambayo inahusisha ujenzi wa kilomita 48 za barabara kwa kiwango cha lami, kati ya hizo kilomita 24 ni kwa kila upande wa daraja hilo. Dk. Magufuli alisema utekelezaji wa mradi huo unahusisha ujenzi wa daraja kubwa lenye urefu wa mita 200 na madaraja ya pembeni mawili yenye urefu wa mita 50 na mita 25. Pia kutajengwa makaravati 10 makubwa ya zege na mengine 80 madogo.

Naye Balozi wa Jamhuri ya Watu wa Korea nchini, Yoong Hoon Kim, alisema ujenzi wa daraja hilo umeonyesha ushirikiano wa karibu na wa kindugu uliopo kati ya serkali ya Tanzania na Korea. Alisema nchi hiyo itaongeza misaada maradufu. Wakati huo huo, baadhi ya wabunge wamewajia juu wenzao wanaobeza safari za nje zinazofanywa na Rais Kikwete, kwa madai kuwa hazina tija. Wakichangia makadirio ya matumizi ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Stephen Ngonyani (Korogwe Vijijini -CCM), alisema katika awamu ya kwanza ya uongozi wa Rais Kikwete amefanya mengi. Alisema kumekuwa na utawala bora katika nchi ambayo kila Mtanzania amekuwa huru kuzunguza juu ya kero mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuikosoa serikali. Ngonyani alisema rais hajaenda kujifurahisha nje ya nchi, bali kuomba misaada kwa ajili ya Watanzania bila kujali itikadi.

"Hata hapa tumekaa tunatanua midomo kuhusu safari hizo, huu ni utawala bora alioleta Rais Kikwete na tutamkumbuka akiondoka. Tumepata misaada mingi ya kuimarisha miundombinu, wanaomsema vibaya wana husda na urais," alisema.
Naye Said Jafo alisema baadhi ya wabunge wamekuwa wakitumia vibaya midomo yao kwa kumbeza Rais Kikwete.
Alisema rais anapokuwa safarini haendi kwa manufaa ya familia yake, bali kwa Watanzania wote.

Tatizo kubwa la Waandishi wa habari walio wengi walikimbia Hisabati kwa madai kuwa ni somo gumu, sasa angalia wanavyopotosha umma na kusababisha wananchi kuichukia serikali yao hasa kipindi hiki ambapo ufisadi umeshika kasi.
 
1KM=1000M
42KM=42000M
Kama la KIKWETE ni mita 200 inamana limezidiwa na la CHINA mara 208.
yani 42000m (urefu wa hilo la china) gawa kwa 200m (urefu wa hilo la KIKWETE.
Jibu ni 210, toa hizo 200. inabaki 208
sasa tufanye bilioni 805x208=42660. inaman tukitaka kujenga kama la china inatutaka kua ana bilion 42,660.
Lakini ukigawanya kwa uianao wa urefu wa hilo lachina dhidi ya hilo la kikwete ilibidi lijengwe kwa 213.3bilioni.

Labda kama nimekosea mahesabu.
 
Hivi kwenye HGK,HGL & KLF kuna subsidiary ya Applied Mathematics?? tusiwalaumu hao "WAANDISHI" kama hizo numbers siyo part and parcel of their courses! nilikuwa napita tu!
 
Naona U great thinker unanipiga chenga hapa.
Kuna uhusiano gani kati ya hii picha ,Tshs 805bn na JK, naomba mtoa post atueleweshe kabla brain yangu sijaipeleka kupark!

Uhusiano ni kuwa thread za kishabiki hata kwa maendeleo ya taifa zinaboa, sasa jamaa kaamua kuiwekea, pilipili, ukwaju, chachandu ili kuinogesha. Mnaboa jinsi mnavyoichukia nchi yenu.
 
Nchi ya masihara, viongozi wanaolala lala tu na watu wanaoishi kimjinimjini

Wakorea nao ni njaa kuliko sisi, Hivi ile kampuni ya kikorea ya TAKOPA ilirudisha ile mobilisation ya Barabara ya Msata? Ambayo walilipwa na wakufanya chochote.
 
Nyambala, tafadhali rekebisha hiyo habari yako. Nimeingia Google Earth na nikaona haiwezekani hilo daraja liwe na urefu wa mita 200. Vipimo kwa macho yangu na ufahamu wangu wa daraja linavyotakiwa kujengwa, vikaniambia kuwa zile PIER zake zitakuwa karibu sana na mto ambayo huwa inaleta hatari ya kuzolewa na maji siku moja. Unaweza kujenga PIER kati ya mto ndiyo ila huwa inaongeza gharama kubwa sana na ni heri ujenge pembeni kama inavyoonekana kwenye picha hapo sehemu kavu na juu ya mto likapita daraja hadi upande mwingine sehemu kavu ndiyo unaweka PIER nyingine.

Nimeingia kwenye magazeti na yanasema hivi: Gazeti ya Mwananchi:

Fidelis Butahe
SERIKALI kupitia Wakala wa Barabara (Tanroads), imesaini mkataba wa ujenzi wa daraja la Mto Malagarasi, mkoani Kigoma, utakaogharimu Dola za Marekani 56,365,770.

Daraja hilo litakalounganisha Mikoa wa Kigoma na Tabora, litakuwa na urefu wa meta 275 na ujenzi wake utakwenda sambamba na ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa kilometa 48.


Chini nimeweka kwa kukisia urefu ambapo zinaweza kuwepo PIER. Ukiangalia sana, kwa urefu wa mita 50 (sehemu ndefu iliyopo juu ya maji) hauhitaji kusimamisha minguzo ili kujenga daraja na Cables. Hapa inatosha kabisa kujenga PRE-STRESSED bridge na kwa urefu huu, inatosha kabisa. Na uzuri wa hayo madaraja ni kuwa zile BOX zake zinaweza kuwa zinajengwa pembeni (Pre-Cast) na baadaye wanakuja na kuziunga kwa Cables tu (ndani ya Box) na daraja linasimama. Inachukua muda mfupi ila seme tu inabidi kuwa na mashine nzito za kunyenyulia hiyo Mibox...

attachment.php


Malagarasi.JPG
image003.jpg
 
Nyambala, tafadhali rekebisha hiyo habari yako. Nimeingia Google Earth na nikaona haiwezekani hilo daraja liwe na urefu wa mita 200. Vipimo kwa macho yangu na ufahamu wangu wa daraja linavyotakiwa kujengwa, vikaniambia kuwa zile PIER zake zitakuwa karibu sana na mto ambayo huwa inaleta hatari ya kuzolewa na maji siku moja. Unaweza kujenga PIER kati ya mto ndiyo ila huwa inaongeza gharama kubwa sana na ni heri ujenge pembeni kama inavyoonekana kwenye picha hapo sehemu kavu na juu ya mto likapita daraja hadi upande mwingine sehemu kavu ndiyo unaweka PIER nyingine.

Nimeingia kwenye magazeti na yanasema hivi: Gazeti ya Mwananchi:

Fidelis Butahe
SERIKALI kupitia Wakala wa Barabara (Tanroads), imesaini mkataba wa ujenzi wa daraja la Mto Malagarasi, mkoani Kigoma, utakaogharimu Dola za Marekani 56,365,770.

Daraja hilo litakalounganisha Mikoa wa Kigoma na Tabora, litakuwa na urefu wa meta 275 na ujenzi wake utakwenda sambamba na ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa kilometa 48.


Chini nimeweka kwa kukisia urefu ambapo zinaweza kuwepo PIER. Ukiangalia sana, kwa urefu wa mita 50 (sehemu ndefu iliyopo juu ya maji) hauhitaji kusimamisha minguzo ili kujenga daraja na Cables. Hapa inatosha kabisa kujenga PRE-STRESSED bridge na kwa urefu huu, inatosha kabisa. Na uzuri wa hayo madaraja ni kuwa zile BOX zake zinaweza kuwa zinajengwa pembeni (Pre-Cast) na baadaye wanakuja na kuziunga kwa Cables tu na daraja linasimama. Inachukua muda mfupi ila seme tu inabidi kuwa na mashine nzito za kunyenyulia hiyo Mibox...

attachment.php


View attachment 33469
image003.jpg

Got ya! mkuu...
 
Uhusiano ni kuwa thread za kishabiki hata kwa maendeleo ya taifa zinaboa, sasa jamaa kaamua kuiwekea, pilipili, ukwaju, chachandu ili kuinogesha. Mnaboa jinsi mnavyoichukia nchi yenu.

Nimegundua kuna watu wengi hamsomi thread kabla ya kuchangia, kuna mtu anauliza eti hi daraja kwa lina uhusiano gani na JK ikidhaniwa kwamba ni personal attack kwa jK. C'moon guys daraja limezinduliwa na JK na pia litaitwa daraja la JK au kwa kiingereza "JK Bridge". Mwingine amekuja na figa ya bilioni 850 sijui ameitoa wapi hiyo coz all over this thread hakuna mahali imekuwa quoted figa hii.
 
Kwanini Wazawa hawapewi kazi kama hizi?. (Ni wachina, wakorea, Wa- South Africa nk)
 
Kwa hiyo gazeti la Habari Leo limedanganya wananchi? Hivi gazeti linaweza kupewa adhabu gani kwa kupotosha wananchi kiasi hichi?
 
Naona ilikuwa a slippery of the hand,wastani wa km moja ujenzi kwa sasa ni kati ya 1 to 1.3 billion ingawa kwa wachina hufika less than a billion ie 700 to 900 million.
Likijengwa litawatoa kweli wenzetu wa Kigoma
 
Mleta habari anasema ni sh za tz bilioni 805 (kama ilinukuliwa kwa makosa toka kwenye chanzo cha habari husika) siyo dola mill 805


Miradi yote ya bongo lazima kuwe na cha juu,ndiyo namna iliyozoeleka kujipatia vijisenti
 
Back
Top Bottom