JK apata Kamati Kuu mpya Ya CCM.

JK apata Kamati Kuu mpya Ya CCM.

babalao 2

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
5,426
Reaction score
3,308
HATIMAYE Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, amekamilisha kuunda safu mpya ya wajumbe wa Kamati Kuu (CC) ya chama hicho ambayo mwaka jana alishindwa kuiunda mjini Dodoma, Tanzania Daima Jumapili limedokezwa.

Habari kutoka ndani ya chama hicho tawala zilisema kuwa, Rais Kikwete anatarajia kuwatangaza wajumbe hao wapya Februari mjini Dodoma wakati wa kikao cha kwanza cha wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).

Vyanzo vyetu vya habari kutoka ndani ya CCM, vilisema kuwa haikuwa kazi rahisi kwa Rais Kikwete kupata wajumbe hao, ndiyo maana alihitaji muda mrefu aweze kuwajua ili kuepuka kufanya uteuzi wa sura na majina yaliyozoeleka.

Kwa mujibu wa habari hizo, CC hiyo ina baadhi ya sura mpya na uteuzi wake umezingatia uwakilishi wa mikoa, hasa Kanda ya Ziwa ambayo safari hii haina hata mjumbe mmoja wa sekretarieti.

“Kuna sura mpya, zipo pia sura zilizozoeleka, lakini baadhi ya mawaziri waliotupwa kwenye uteuzi wa Rais Kikwete mwaka jana, wamo kwenye Kamati Kuu,” kilisema chanzo chetu cha habari.

Mara baada ya kuteua sekretarieti mpya chini ya Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana mwaka jana, Rais Kikwete alishindwa kuunda Kamati Kuu.

Rais Kikwete alisema anahitaji muda zaidi kuwajua baadhi ya wajumbe wapya wa NEC ili kuepuka kuteua majina na sura. zilezile.

“Nimewaomba wajumbe wa NEC wanipe muda kidogo wa kufanya uteuzi wa wajumbe wa Kamati Kuu, kwa sababu tuna wajumbe wengi wapya ambao nahitaji kuwajua kwanza,” alisema Kikwete wakati akizungumza na wajumbe wa NEC mjini Dodoma.

Katika uteuzi wake huo mpya wa sekretarieti, Kikwete alimtupa nje aliyekuwa Katibu Mkuu, Wilson Mukama na nafasi yake kutwaliwa na kada mkongwe na mzoefu, Kinana.

Aliwateua wajumbe wapya wanane, wakiwamo wanawake wawili, Zakhia Meghji, ambaye amerithi mikoba ya. Katibu wa NEC Uchumi na Fedha, Mwigulu Nchemba, anayekuwa Naibu Katibu Mkuu Bara, hivyo kumtupa nje, John Chiligati, aliyekuwa akishikilia wadhifa huo.

Mwanamke mwingine aliyechomoza katika sekretarieti hiyo mpya ni Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, ambaye anavaa viatu vya Januari Makamba, kwenye nafasi ya Katibu wa Siasa na Mambo ya Nje.

Makamba ameachwa ili abaki na nafasi yake ya Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.

Hata hivyo, kitendo cha Kikwete kumuingiza Dk. Migiro kwenye sekretarieti na kuwa mjumbe wa NEC na CC, kimetafsiriwa na wachambuzi wa siasa kuwa ni kumjengea mazingira ya kuwania urais mwaka 2015.

Nafasi ya Naibu Katibu Mkuu Zanzibar imeendelea kushikiliwa na Vuai Ali Vuai, huku Nape Nnauye, ameendelea kushikilia nafasi yake ya Katibu wa Itikadi na Uenezi, ambayo ameonekana kuimudu vema
tangu alipoteuliwa.

Mohammed Seif Khatib, amekuwa Katibu wa Oganaizesheni, ambayo awali ilishikiliwa na Asha Abdallah Juma, ambaye safari hii ametupwa nje.

Mohamed Seif Khatib na Kinana wanaingia kwenye Kamati Kuu (CC), kutokana na nafasi zao.
 
mambo ya 2015 hayo.

mambo yapi hayo? Hii habari ni ya kuunga unga tu. Amepata kamati kuu bila wa-nec kuwachagua hao wajumbe?

Hii post haina jipya sababu hajatangaza majina 21 ambayo halmashauri kuu itapigia kura kuunda cc , sekretariet inafahamika toka novemba.

Factcheck: Kichwa cha habari kimekuwa rated " upotoshaji", tusubiri feb sio mbali
 
Apata maana ni wapya

babalao 2 kinachoendelea ni recycling of the same old faces...................wakishindwa kukubalika kwa wananchi wanahamishiwa utendaji ndani ya chama wakakiharibu kama walivyoyaharibu majimbo yao:-

Kinana..............hachaguliki hapa Arusha baada ya kutuibia washing machines mbili heavy duty na kuwaanzisha ndugu zake falcon dryers...............azirudisha kabla haajaanza filimbi za kupambana mafisadi wakati yeye ni fisadi aliyebobea.

Meghji.......................ufisadi wake BOT na EPA bado hatujausahau na hawezi kugombea hata uongozi wa shina lake akachagulika.......................

Nape jr...................jina la baba kuwa nape na baba alikuwa kamati kuu ndiyo imemweka hapo.............eti huyo ndiyo mwakilishi wa vijana.........hata shule bado hajasoma na kumalizia................give me a huge break on this list of shame........

Asha Rose Migiro.........Anajiita katibu mkuu mstaafu lakini bosi wake kule UN alimtimua kwa utendaji mbovu na kila siku matibabu yasiyo na tiba.........................

na wengineo akina...........Mohammed Seif Khatib nimemsikia huyu babu tangia baraza la nyerere alikuwa naibu waziri sijui...ni wa long lakini wamwona mpya..........ni walewale....................walioiharibu nchi wanajipanga upya kuiharibu zaidi...........
 
Kumbe chanzo TANZANIA DAIMA gazeti la UDAKU huo ni uongo mtupu,
 
Mhariri wa gazeti ona aibu kwa habari hii,hadhi ya gazeti,inaporomoka.
 
Huyo Migiro kwenye kamati kuu ndiyo ule utabiri wa yule shekhe au, kwamba rais ajae ni mwanamke
 
Hakuna jipya. JK Hakutea kamati kwa sababu ya kashfa ya wengi kuingia ktk nafasi zao. Mhariri wa Tz Daima amebadilishwa nini? Gazeti halitofautiani na yale makorokocho (udaku)
 
Timu ya wajumbe wa kamati kuu ya CCM ambayo ndiyo dira ya ushindi ya chama hicho kuelekea uchaguzi wa 2015 ni sawa na kuziba tundu la panya kwa kutumia mkate.Namaanisha safu hii kujaa walafi walioshindikana ndani na nje ya serikali kwa tuthuma mbalimbali.

Mwangalie Kinana meli yake imekamatwa na pembe za ndovu,Zakia Meghji amemaliza misitu yetu huko Rufiji,Lindi na Mtwara kwa kutoa vibali vya kuuza magogo.Mwigulu Mchemba bingwa wa kukiuka maadili ya jamii na bingwa wa matusi.Kwa stahili hii chama kinazidi kuzamisha jahazi lake kwa kutegemea kuziba matundu yaliyo tobolewa na panya kwa kutumia mkate.Haiwezekani mwizi kupewa majukumu ya kulinda nchi na nchi ikabaki salama
 
Watafurahi wanakutana na watu makini cdm kitaeleweka tu hamna mjinga tena wacha iwe mbaya
 
Hii ni moja ya kamati kuu makini nani timu ya ushindi wewe endelea kupiga majungu jibu utalipata 2015,
 
Adui yako muombee njaa.

Hapo sasa CDM wamepata turufu ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015
 
Mimi nashangaa, huyu meghji ana nini kwa JK? Kila wakati ni chaguo la Jk. Kwenye sakata la EPA tuliona alivyochemsha kumuwekea Balali kifua halafu madudu yakatokea!!!
 
Back
Top Bottom