JIPU: Walimu wasio na sifa ktk shule binafsi/za Jumuiya ya Wazazi Tz

Amoxlin

JF-Expert Member
May 30, 2016
3,782
4,111
Habari wana-jamvi.

Katika kipindi hiki kumekuwa na ushindani mkubwa sana ktk sekta ya elimu hapa nchini.

Ushindani huo upo katika utoaji wa elimu bora, ajira kwa walimu sambamba na ufaulu mzuri wa wanafunzi ili kujiongezea wateja (soko) ktk shule binafsi.

Katika shule nyingi kumekuwa na wimbi kubwa la walimu wasio na sifa (hawajasomea ualimu / walioshindwa kuhitimu kutokana na maendeleo mabaya kitaaluma) ambao kazi yao ni kuwakaririsha wanafunzi vitabu hata kama vimekosewa kwakuwa sio fani yao.

Walimu hawa vishoka kwa kawaida hufundisha masomo yote, kila somo yeye twende... Ilimradi kuziba nafasi zisizo na walimu ila ufanisi hakuna.

Kwanini walimu wasio na sifa?
Wakuu wa shule binafsi hasa zilizopo chini ya jumuia ya wazazi ambazo baadhi huendeshwa kisiasa na sio kisayansi huajiri walimu wasio na sifa ili kuwalipa mishahara midogo sana bila kujali wanafunzi wanaathirika vipi darasani.

Baadhi ya walimu hao wasio na sifa ni ndugu wa viongozi wa ngazi za juu za shule au chama (katika shule zilizopo chini ya jumuia ya wazazi).

Kutokana na hali hii ya kuwa na walimu wasio na sifa kwa kawaida kunakuwa na kamati ya ufundi ambayo kazi yake kubwa ni kuhakikisha wanafunzi hao wanafaulu hata kwa kupitia goli la mkono.

Wito wangu:
Wakaguzi wa masuala ya elimu wazikague shule binafsi hasa zilizopo chini ya jumuiya ya wazazi ambazo huendeshwa kisiasa ili kujiridhisha na hali halisi.

Wasikague tu maandalio ya somo ila wakague na vyeti vya walimu ktk shule hizo kwani wapo walimu wenye sifa mitaani ila hawapati ajira kutokana na kukumbatia vishoka wanaoteketeza taifa letu.

Mpango huu uanzie ktk mkoa wa Kilimanjaro wilaya ya Moshi, Mwanga, Rombo nk. Pia ktk mkoa wa Tanga ambapo hali hazitofautiani sana kutokana na wingi wa shule hizi.
 
Kiukweli hilo ni tatizo sana kwa shule nyingi za binafsi,mtu anakuwa na degree ya Public administration anaajiriwa kufundisha watoto wetu,au amesoma computer science yupo busy kufundisha,sababu kubwa wanalipwa kiduchu ili ajipatie pesa za kujikimu kidogo,madhara yake kwa hakika ni makubwa kwa Wateja(wanafunzi).
Hili limekuwa tatizo sana hata kwa shule za dini,including zile za Kikatoliki!!!
 
Habari wana-jamvi.

Katika kipindi hiki kumekuwa na ushindani mkubwa sana ktk sekta ya elimu hapa nchini.

Ushindani huo upo katika utoaji wa elimu bora, ajira kwa walimu sambamba na ufaulu mzuri wa wanafunzi ili kujiongezea wateja (soko) ktk shule binafsi.

Katika shule nyingi kumekuwa na wimbi kubwa la walimu wasio na sifa (hawajasomea ualimu / walioshindwa kuhitimu kutokana na maendeleo mabaya kitaaluma) ambao kazi yao ni kuwakaririsha wanafunzi vitabu hata kama vimekosewa kwakuwa sio fani yao.

Walimu hawa vishoka kwa kawaida hufundisha masomo yote, kila somo yeye twende... Ilimradi kuziba nafasi zisizo na walimu ila ufanisi hakuna.

Kwanini walimu wasio na sifa?
Wakuu wa shule binafsi hasa zilizopo chini ya jumuia ya wazazi ambazo baadhi huendeshwa kisiasa na sio kisayansi huajiri walimu wasio na sifa ili kuwalipa mishahara midogo sana bila kujali wanafunzi wanaathirika vipi darasani.

Baadhi ya walimu hao wasio na sifa ni ndugu wa viongozi wa ngazi za juu za shule au chama (katika shule zilizopo chini ya jumuia ya wazazi).

Kutokana na hali hii ya kuwa na walimu wasio na sifa kwa kawaida kunakuwa na kamati ya ufundi ambayo kazi yake kubwa ni kuhakikisha wanafunzi hao wanafaulu hata kwa kupitia goli la mkono.

Wito wangu:
Wakaguzi wa masuala ya elimu wazikague shule binafsi hasa zilizopo chini ya jumuiya ya wazazi ambazo huendeshwa kisiasa ili kujiridhisha na hali halisi.

Wasikague tu maandalio ya somo ila wakague na vyeti vya walimu ktk shule hizo kwani wapo walimu wenye sifa mitaani ila hawapati ajira kutokana na kukumbatia vishoka wanaoteketeza taifa letu.

Mpango huu uanzie ktk mkoa wa Kilimanjaro wilaya ya Moshi, Mwanga, Rombo nk. Pia ktk mkoa wa Tanga ambapo hali hazitofautiani sana kutokana na wingi wa shule hizi.
Mkuu hilo suala lipo na nimeliona shule ya wazazi ujiji iliyopo kigoma, mwalimu form six kafeli yeye anafundisha o'level na anarisit mitihani ya six shule hiyohiyo karibu mwaka wa sita sasa hajapata principal na anaendea kuwafundisha watoto
 
Mkuu hilo suala lipo na nimeliona shule ya wazazi ujiji iliyopo kigoma, mwalimu form six kafeli yeye anafundisha o'level na anarisit mitihani ya six shule hiyohiyo karibu mwaka wa sita sasa hajapata principal na anaendea kuwafundisha watoto
Mmmmmh hii Kali....!
 
unge taja angalau shule moja ya jumuiya ya wazazi/ private wenye hako kamchezo
 
kuna chuo flan cha private nlikuwa nafundisha siku wakaguzi walikuja gafla kama kufumania hivi mzee mmoja akasema vyeti vyake vya diploma&degree vilibebwa na maji hana hata copy nlichekaga sana
 
kuna chuo flan cha private nlikuwa nafundisha siku wakaguzi walikuja gafla kama kufumania hivi mzee mmoja akasema vyeti vyake vya diploma&degree vilibebwa na maji hana hata copy nlichekaga sana

Nitajie jina la huyo Mzee.
 
Back
Top Bottom