Jinsi ya kutumia simu yako kama CCTV camera

Jinsi ya kutumia simu yako kama CCTV camera

jamaikatz

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2023
Posts
380
Reaction score
1,312
Unataka kuangalia nyumbani kwako ukiwa kazini au shuleni? Hakuna haja ya kununua CCTV ya bei ghali!

Tumia simu ya zamani kama kamera ya ulinzi kwa kutumia app moja rahisi sana:

App: Alfred Camera

Faida:
  • Unaiona nyumba live kutoka simu nyingine
  • Ina motion detection (ikigundua mtu inarekodi)
  • Inaweza kuplay audio (unaweza kusikia na kuongea)
  • Huhitaji Wi-Fi ya nguvu sana

Trick:
1. Chukua simu ya zamani yenye kamera
2. Install Alfred Camera
3. Iconnect na akaunti yako ya Google
4. Iweke sehemu unayotaka ku-monitor
5. Tumia simu yako ya sasa kuangalia live

Kwa usalama zaidi, weka simu hiyo kwenye chaji muda wote na ifunge na app lock.
 
Hata kama itafanya kazi ni option ya gharama sana
Portable cctv camera yenye solar panell, wifi na motion detector inagaharimu chini ya laki mbili, na hii hata nje kwenye jua na mvua inakaa,
 
Back
Top Bottom