Jinsi ya kupika mlenda wa unga

MAHITAJI
1.Karanga za kusagwa
2.Chumvi
3.Unga wa mlenda
4.Maji

Jinsi ya kuandaa
Chukua karanga zilizosagwa vizuri loweka kwenye bakuli la maji,baada ya muda anza kuzikoroga utokee uji mzito kiasi

Bandika sufuria lako jikoni hakikisha moto sio mkali,maana moto mkali unawahi unguza mboga

Baada ya hapo mimina ule uji wa karanga kisha koroga taratibu mpaka uchemkie(ukiacha kukoroga utaungulia kwa chini)

Uji ukishachemkia(kutokota au kupogoma)weka unga wa mlenda unaweza weka vijiko vya chakula vitatu(hapa ni kulingana na mahitaji yako usiukoleze sana mlenda kwa kujazia unga wake.

Kisha weka chumvi

Koroga kama unasonga ugali,usitumie nguvu sana ni rahisi tu

Baada ya hapo epua,mlenda wako tayari.

NB: sina utaalamu sana wa vipimo vya upishi,ndio maana sijaweka vipimo sahihi vya upishi huu
Safi sana hapo full kujilamba.
*Nyongeza:unaweza kutumia maziwa fresh badala ya maji
 
MAHITAJI
1.Karanga za kusagwa
2.Chumvi
3.Unga wa mlenda
4.Maji

Jinsi ya kuandaa
Chukua karanga zilizosagwa vizuri loweka kwenye bakuli la maji,baada ya muda anza kuzikoroga utokee uji mzito kiasi

Bandika sufuria lako jikoni hakikisha moto sio mkali,maana moto mkali unawahi unguza mboga

Baada ya hapo mimina ule uji wa karanga kisha koroga taratibu mpaka uchemkie(ukiacha kukoroga utaungulia kwa chini)

Uji ukishachemkia(kutokota au kupogoma)weka unga wa mlenda unaweza weka vijiko vya chakula vitatu(hapa ni kulingana na mahitaji yako usiukoleze sana mlenda kwa kujazia unga wake.

Kisha weka chumvi

Koroga kama unasonga ugali,usitumie nguvu sana ni rahisi tu

Baada ya hapo epua,mlenda wako tayari.

NB: sina utaalamu sana wa vipimo vya upishi,ndio maana sijaweka vipimo sahihi vya upishi huu
Nswalu na mkunungu ni vitu viwili tofauti, nswalu inatoka shinyanga, tabora, kahama, singida, nswalu ni kinyiramba na nzubyo ni kisukuma ila mchanganyiko ni huo huo, mkunungu unatoka iringa, ili upate unga wa nswalu kuna majani yapo ya mlenda unaitwa mlenda bata, mlenda wima na mwingine unaitwa wibhela unachanganywa na majani ya limbe zinakaushwa kwa pamoja au kutenganishwa zikikauka unatwangwa unachekechwa tayari kwa matumizi, mwingine unakausha bamia zikiwa zimekatwa katwa na msusa au majani ya maboga zikikauka zinatwangwa tayari kwa matumizi.
ili kupika chota vijiko viwili vya karanga na kijiko kimoja cha chakula cha nswalu weka kwenye sufuria na maji kidogo ili mboga iwe nzito koroga mpaka uwe uji mzito weka chumvi weka mboga koroga vizuri weka jikoni ukiwa mzito ongeza maji kidogo usiwe mgumu sana moto uwe mdogo ili isiungue haraka ikianza kutoa mafuta tayari kajilambe.
 
Asante sana cute. Nimejifunza upishi mpya kwako. Be blessed
Nswalu na mkunungu ni vitu viwili tofauti, nswalu inatoka shinyanga, tabora, kahama, singida, nswalu ni kinyiramba na nzubyo ni kisukuma ila mchanganyiko ni huo huo, mkunungu unatoka iringa, ili upate unga wa nswalu kuna majani yapo ya mlenda unaitwa mlenda bata, mlenda wima na mwingine unaitwa wibhela unachanganywa na majani ya limbe zinakaushwa kwa pamoja au kutenganishwa zikikauka unatwangwa unachekechwa tayari kwa matumizi, mwingine unakausha bamia zikiwa zimekatwa katwa na msusa au majani ya maboga zikikauka zinatwangwa tayari kwa matumizi.
ili kupika chota vijiko viwili vya karanga na kijiko kimoja cha chakula cha nswalu weka kwenye sufuria na maji kidogo ili mboga iwe nzito koroga mpaka uwe uji mzito weka chumvi weka mboga koroga vizuri weka jikoni ukiwa mzito ongeza maji kidogo usiwe mgumu sana moto uwe mdogo ili isiungue haraka ikianza kutoa mafuta tayari kajilambe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom