DiasporaUSA
JF-Expert Member
- Aug 27, 2016
- 23,291
- 29,485
Numbisa unaujua mkunungu ?
Safi sana hapo full kujilamba.MAHITAJI
1.Karanga za kusagwa
2.Chumvi
3.Unga wa mlenda
4.Maji
Jinsi ya kuandaa
Chukua karanga zilizosagwa vizuri loweka kwenye bakuli la maji,baada ya muda anza kuzikoroga utokee uji mzito kiasi
Bandika sufuria lako jikoni hakikisha moto sio mkali,maana moto mkali unawahi unguza mboga
Baada ya hapo mimina ule uji wa karanga kisha koroga taratibu mpaka uchemkie(ukiacha kukoroga utaungulia kwa chini)
Uji ukishachemkia(kutokota au kupogoma)weka unga wa mlenda unaweza weka vijiko vya chakula vitatu(hapa ni kulingana na mahitaji yako usiukoleze sana mlenda kwa kujazia unga wake.
Kisha weka chumvi
Koroga kama unasonga ugali,usitumie nguvu sana ni rahisi tu
Baada ya hapo epua,mlenda wako tayari.
NB: sina utaalamu sana wa vipimo vya upishi,ndio maana sijaweka vipimo sahihi vya upishi huu
Okay natumaini uta enjoyThank u kwa nyongeza,nilikua sijui ntaijaribu hii njia
Ni unga unga unaotumika kupika mlenda. Kwa wakazi huenda wanaujua.Inaweza kua naujua ila jina ulilotumia ni geni,ni mboga gani hio?
YamposutaPupweeee haaaa
PossiblyNdio huu niliouandika,wengine wanauita nswalu.
Unatokana na kutwangwa kwa majani ya maboga na mchanganyiko mwingine sijui wa majani gani
Nswalu na mkunungu ni vitu viwili tofauti, nswalu inatoka shinyanga, tabora, kahama, singida, nswalu ni kinyiramba na nzubyo ni kisukuma ila mchanganyiko ni huo huo, mkunungu unatoka iringa, ili upate unga wa nswalu kuna majani yapo ya mlenda unaitwa mlenda bata, mlenda wima na mwingine unaitwa wibhela unachanganywa na majani ya limbe zinakaushwa kwa pamoja au kutenganishwa zikikauka unatwangwa unachekechwa tayari kwa matumizi, mwingine unakausha bamia zikiwa zimekatwa katwa na msusa au majani ya maboga zikikauka zinatwangwa tayari kwa matumizi.MAHITAJI
1.Karanga za kusagwa
2.Chumvi
3.Unga wa mlenda
4.Maji
Jinsi ya kuandaa
Chukua karanga zilizosagwa vizuri loweka kwenye bakuli la maji,baada ya muda anza kuzikoroga utokee uji mzito kiasi
Bandika sufuria lako jikoni hakikisha moto sio mkali,maana moto mkali unawahi unguza mboga
Baada ya hapo mimina ule uji wa karanga kisha koroga taratibu mpaka uchemkie(ukiacha kukoroga utaungulia kwa chini)
Uji ukishachemkia(kutokota au kupogoma)weka unga wa mlenda unaweza weka vijiko vya chakula vitatu(hapa ni kulingana na mahitaji yako usiukoleze sana mlenda kwa kujazia unga wake.
Kisha weka chumvi
Koroga kama unasonga ugali,usitumie nguvu sana ni rahisi tu
Baada ya hapo epua,mlenda wako tayari.
NB: sina utaalamu sana wa vipimo vya upishi,ndio maana sijaweka vipimo sahihi vya upishi huu
Nswalu na mkunungu ni vitu viwili tofauti, nswalu inatoka shinyanga, tabora, kahama, singida, nswalu ni kinyiramba na nzubyo ni kisukuma ila mchanganyiko ni huo huo, mkunungu unatoka iringa, ili upate unga wa nswalu kuna majani yapo ya mlenda unaitwa mlenda bata, mlenda wima na mwingine unaitwa wibhela unachanganywa na majani ya limbe zinakaushwa kwa pamoja au kutenganishwa zikikauka unatwangwa unachekechwa tayari kwa matumizi, mwingine unakausha bamia zikiwa zimekatwa katwa na msusa au majani ya maboga zikikauka zinatwangwa tayari kwa matumizi.
ili kupika chota vijiko viwili vya karanga na kijiko kimoja cha chakula cha nswalu weka kwenye sufuria na maji kidogo ili mboga iwe nzito koroga mpaka uwe uji mzito weka chumvi weka mboga koroga vizuri weka jikoni ukiwa mzito ongeza maji kidogo usiwe mgumu sana moto uwe mdogo ili isiungue haraka ikianza kutoa mafuta tayari kajilambe.