Jinsi ya kupika mlenda wa unga

Numbisa

JF-Expert Member
Dec 12, 2016
267,878
1,093,859
MAHITAJI
1.Karanga za kusagwa
2.Chumvi
3.Unga wa mlenda
4.Maji

Jinsi ya kuandaa
Chukua karanga zilizosagwa vizuri loweka kwenye bakuli la maji,baada ya muda anza kuzikoroga utokee uji mzito kiasi

Bandika sufuria lako jikoni hakikisha moto sio mkali,maana moto mkali unawahi unguza mboga

Baada ya hapo mimina ule uji wa karanga kisha koroga taratibu mpaka uchemkie(ukiacha kukoroga utaungulia kwa chini)

Uji ukishachemkia(kutokota au kupogoma)weka unga wa mlenda unaweza weka vijiko vya chakula vitatu(hapa ni kulingana na mahitaji yako usiukoleze sana mlenda kwa kujazia unga wake.

Kisha weka chumvi

Koroga kama unasonga ugali,usitumie nguvu sana ni rahisi tu

Baada ya hapo epua,mlenda wako tayari.

NB: sina utaalamu sana wa vipimo vya upishi,ndio maana sijaweka vipimo sahihi vya upishi huu
 
MAHITAJI
1.Karanga za kusagwa
2.Chumvi
3.Unga wa mlenda
4.Maji

NB: sina utaalamu sana wa vipimo vya upishi,ndio maana sijaweka vipimo sahihi vya upishi huu

Ha ha ha, bila kuweka vipimo unatuacha bila kutufikisha, maana hapa unaweza kushindwa kubalancisha msosi.

emmyta atakuwa anajua mambo ya vipimo, ngoja nimcheki aje kumalizia hii.
 
Hahaha vipimo shughuli kubwa.

Emmy akikufundisha vipimo nishtue na mie,kizuri kula na nduguyo
Ha ha ha, bila kuweka vipimo unatuacha bila kutufikisha, maana hapa unaweza kushindwa kubalancisha msosi.

emmyta atakuwa anajua mambo ya vipimo, ngoja nimcheki aje kumalizia hii.
 
Hahahaa hawa jamaa wanazingua,wamesuntana wee mpaka watazamaji tumechoka,si wachapane tu yaishe
Hahahahaha lol! Trump akianza kuangusha mabomu nistue ili tuangalie utaratibu wa kuja kukuokoa. :):)
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Safi kabisa,mboga ikiiva pia mnikaribishe ntakuja na poti la ugali wa dona.

Ukisubiri mpaka mboga iive unaweza kuta tumemaliza kula, maana lengo ni mlenda tu, ukiiva tunaula hivyo hivyo, hatuna muda wa kusonga ugali.
 
Aah mpaka tumechoka maana watu wamesha bet tayari tayari kwa kudaka mapesa
Wanazinguana tu kila mtu anamuhofia mwenzie wamebaki kuweka mikwara mizito.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Haa jamani yaan nakupa ofa unanikatisha tamaa kabisa
Ukisubiri mpaka mboga iive unaweza kuta tumemaliza kula, maana lengo ni mlenda tu, ukiiva tunaula hivyo hivyo, hatuna muda wa kusonga ugali.
 
Trump kaonywa usicheze na huyo mwehu anaweza kuisambaratisha dunia na baada ya missiles zake mkorea kwenda alijojo naye kaingia woga.

Aah mpaka tumechoka maana watu wamesha bet tayari tayari kwa kudaka mapesa
 
Angekua bush angeshaenda vitan zamani trumph ujanja wake upo kwenye biashara na vitisho
Trump kaonywa usicheze na huyo mwehu anaweza kuisambaratisha dunia na baada ya missiles zake mkorea kwenda alijojo naye kaingia woga.
 
  • Thanks
Reactions: BAK

Similar Discussions

Back
Top Bottom