Jinsi ya ku-design Blog inayolipa (Part 1)

Jinsi ya ku-design Blog inayolipa (Part 1)

Shukrani mkuu kwa maelezo ya awali.Kwa upande wangu naona uzi huu unatosha sana kwa kila somo linalo husu blog.

Ila naomba kuuliza ni wapi naweza kununua Domain,na pia nasikia kuna jinsi ya kuilipia ili iwe inapatikana mwanzo katika matokeo ya mtu akitafuta kitu.wanasema hii ni njia rahisi pia watu kuitembelea,vipi mkuu kwa hili inawezekana ikawa ni kweliii?.

Natanguliza shukrani zangu za dhati kwa somo hili kaka.Asante
 
Ila naomba kuuliza ni wapi naweza kununua Domain,

Mkuu, zamani ndiyo ilikuwa shida kuwaza wapi ununue domain, siku hizi kuna wauzaji wengi hawana hata idadi na uzuri zaidi ni kuwa unaweza kununua hata wewe mwenyewe kama una account bank na una credit au debit card na karibu bank zote zinatoa card hizi kwa sasa.

Mimi yangu nilinunua kutoka godady, lakini pia kuna waTanzania wengi wanauza domain.




na pia nasikia kuna jinsi ya kuilipia ili iwe inapatikana mwanzo katika matokeo ya mtu akitafuta kitu.wanasema hii ni njia rahisi pia watu kuitembelea,vipi mkuu kwa hili inawezekana ikawa ni kweliii

Hapo sasa unaongelea kitu kingine kinaitwa Search Engine Optimization (S.E.O) Ambacho tutakijadili hapo baadaye tutakapozungumzia kuhusu traffic ya blog
 
Shukrani mkuu,basi nitafanya taratibu za kibenki


Pia naamini tutakua pamoja katika hili la (S.E.O).Kama ulivyotangulia kueleza mkuu.

Shukrani sana
 
Fadhili Paulo mbali na kwamba unajua unachokieleza,
ubora wako mwingine ni katika kuandika lugha fasaha
na inayoeleweka kwa urahisi sana. Hongera sana Mkuu.
Mimi ntahitaji kupata domain mkuu tayari ninayo blogu.
Kwa hapa tanzania ni wapi na kina nani watafaa zaidi.
Ushauri waki plz
 
Kazi nzuri mzee.. Mimi niko vizuri sana kwenye html5, php, mysql na java iko siku tutakuja kufanya kazi pamoja...
 
Fadhili Paulo mbali na kwamba unajua unachokieleza,
ubora wako mwingine ni katika kuandika lugha fasaha
na inayoeleweka kwa urahisi sana. Hongera sana Mkuu.
Mimi ntahitaji kupata domain mkuu tayari ninayo blogu.
Kwa hapa tanzania ni wapi na kina nani watafaa zaidi.
Ushauri waki plz


Nashukuru sana mkuu kwa feedback hiyo yenye kutia moyo.

Kama nilivyosema wauzaji ni wengi sana ila kwa hapa naweza kumpa credit Donn mtafute kwenye PM atakusajiria hiyo domain ndani ya dakika kadhaa tu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Fadhili Paulo,

Ahsante kwa darsa zuri na binafsi ningependa sana kukazia hapo kwenye UNIQUE CONTENT/MAKALA ZA KIPEKEE ORIJINO coz' ni eneo ambalo ndo nalifahamu vizuri but am not some IT guy!! Kama ulivyosema, hili eneo ndo muhimu and probably ndo eneo gumu kuliko yote linapokuja suala la blogging coz' in ongoing task! Hapa wapo watakaokushauri some automation mara hiki na kile but CONTENTS ndo everything... content ndiyo inafanya users watulie kwenye blog yako kwa dakika kadhaa and probably hours na kesho au hata baadae kurudi tena na tena! Pamoja na mambo mengine lakini CONTENT (including how you write them) ndizo zinachangia blog yako kutokea kwenye Google search engine and don't forget kwamba uandishi wa Web Content ni tofauti na uandishi wa articles za kwenye printed newspapers/magazines ambako hakuna emphasize kwenye matumizi ya keywords.

Anyway, kwa hofu ya kuchelea kubadilisha mwelekeo wa mada, endelea na darsa ambalo sina shaka watu litawafaidisha sana ila itoshe tu kusema kwamba, lengo la blogger si kuifanya blog yake kuwa just a transit blog but to let it being a main terminal where web users will settle! Ukiwa mvivu wa kuandika na matokeo yake unaamua kuchakua first few lines za Content X from Blog Y then unaweka link ( AND YOU MUST DO IT) to Blog Y then blog yako always itakuwa just a transit na watu wataenda kule uliko-direct link na kule ndiko wata-settle coz' watakuta contents zingine ambazo zime-origin pale!

REMEMBER: Unapoandika contents don't cheat... unatakiwa kuwa na contents ambazo ni original. Ninaposema contents ambazo ni original simaanishi uandike vitu ambavyo havijawahi kuandikwa popote pale; HELL NO! Ikiwa unaandika Content sawa na ya Fadhili Paulo hapo juu, that's "Jinsi ya ku-design Blog inayolipa" then andika kwa kutumia maneno yako mwenyewe! Sometimes Google wanakuwaga wanoko sana especially wanapotaka kukufanyia evaluation ya Google Adsense! Moja ya mambo wanayoangalia ni originality ya content... rule of thumb, inabidi iwe at least 90% original... sio inapitishwa kwenye plagiarism-checker wanakuta 60% original kwa kila content... trust me, wanaweza kukupiga hata ban coz' unawafanya wao wawe ndo chanzo cha kusambaza contents za watu wengine ambazo zingine ni copyrighted.
 
Last edited by a moderator:
Paulo Fadhili Somo lako ni muhimu sana endelea kutusaidia
kupata elimu nzuri
 
Last edited by a moderator:
Jinsi ya ku-design Blog inayolipa (Part 2):

Tunaendelea na sehemu ya pili ya somo letu

2. UNIQUENESS (UPEKEE)

Blog inayolipa lazima iwe ni ya kipekee (Unique). Hapa uwe makini kidogo maana hili ndilo lililo mhimu kuliko yote. Kama huwezi kumshawishi mtembeleaji mpya wa blog yako kuiona blog yako ni ya tofauti, nini kitamfanya aendelee kubaki hapo akisoma au arudi tena kesho kuona kama kuna jipya?

Njia pekee ya uhakika ya kuifanya blog yako ni tofauti na blog nyingine ni UPEKEE. Kama hakuna vitu vya kipekee kwenye blog yako usitegemee mtembeleaji wa kwanza au mpya wa blog yako kurudi tena au kuitafuta tena hiyo blog.

Ninaposema upekee kwenye blog naongelea vitu vikuu viwili ambavyo ni;

1. UNIQUE DESIGN/MUONEKANO WA KIPEKEE


Blog yako ili ilipe lazima iwe na muonekano wa kipekee. Muonekano wake kwa maana ya rangi, menu zake, namna inavyowasiliana na kujibizana na watembeleaji uwe ni wa kipekee na usiobadilika kila mara, mfano leo nimetembelea blog yako nakuta in background ya blue, kesho nakuta ina background nyekundu!, hapana, haiwi hivi. Unaweza kubadili muonekano wa blog yako baada ya miezi 6 au mwaka mmoja au miaka kadhaa, lakini siyo kila mara kwa sababu inaweza hata kuathiri kiasi cha uaminifu wa wasomaji wako kwako.


Hivyo unapofikiria kuanzisha blog yako fikiria pia juu ya kumpata mtengenezaji au designer wa blog atakayekutengenezea blog yenye muonekano wa pekee kwa maana kwamba blog yako haifanani fanani na blog nyingine kirahisi ili kukufanya wa tofauti.

2. UNIQUE CONTENT/MAKALA ZA KIPEKEE ORIJINO


Hapa ndiyo penye shida sana hasa kwa bloggers wengi wa Tanzania. Yaani Bloggers wengi wanachofanya ni kusubiri website ya gazeti fulani au blogger fulani aandike makala na wengine wote wana-copy na ku-paste kwenye blog zao kwa kichwa cha habari kile kile na maelezo yale yale!. Ni vigumu kuwa na blog inayolipa kwa staili hii.


Ili kuwa na Blog inayolipa, blogger unatakiwa ushiriki kwenye kutayarisha, kuandaa na kuandika makala za blog yako wewe mwenyewe. Sasa kuna sababu gani ya mimi kutembelea blog yako kama makala zako zote una-copy toka blog ya Shigongo?, ni heri nifunguwe kila siku blog ya Shigongo ambako nitapata orijino stori badala ya kuja kwako. Hii inaathari nyingi ikiwemo kukosa traffic kutoka search engines kama vile google.

Kuna vitu vingi sana unavyoweza kuviandika. Lakini wengi wanapenda kuandika tu juu ya mapenzi, michezo na siasa. Unaweza kuandika juu ya somo lolote iwe ni hesabu au biolojia, unaweza kuandika kuhusu kilimo, ufugaji, ujasiriamali, uchumi, afya, utalii, hoteli, shule, saikolojia, ushauri, malezi, na mengine mengi bila idadi na ukaeleimisha jamii inayokuzunguka.

Kwanini watu wanatembelea blog yako? Kwa sababu kuna jambo wanataka kusoma au kujifunza. Ukiwa blogger huna tofauti na mwalimu. Mwalimu au profesa wa chuo kikuu analipwa mshahara kwa sababu kuna kitu fulani anachofundisha.

Anzisha blog, chagua mada maalumu na udumu kwenye mada hiyo ukiifundisha kila mara kidogo kidogo. Andika habari au makala ambayo haifanani na wengine lakini yenye msaada kwa msomaji. Andika jambo likakamilika.

Kuna ushindani mkubwa na unaozidi kuongezeka siku hadi siku kwenye sekta hii ya uandishi. Andika kitu cha pekee (unique story) na mhimu kuliko yote, stori iwe ni yenye kumsaidia au kumuongezea thamani msomaji wako.

Kwa ufupi, sehemu hii ya pili inagusia kwenye jambo la UPEKEE, Upekee kwenye muonekano wa blog, kazi ambayo siyo yako wewe blogger bali ni kazi ya msanifu/designer wako na upekee kwenye makala au stori zako, kazi ambayo ni yako moja kwa moja.

UVIVU ndilo neno pekee linaloweza kusomeka na likaleta maana ukianzia kulisoma upande wowote iwe ni kushoto au kulia.

Tutaendelea na sehemu ya tatu …

Karibuni kwa michango

Asante sana.. Nimependa hii sehemu ya pili ya tutorial yetu.. Hasa katika matumizi ya lugha fasaha na pia logical connection na ile sehemu ya kwanza. Ila mapendekezo yangu tu ungeextend kidogo hadi kwenye intermediate cos naona umejikita zaidi kwenye basics.. Mf: Hujagusia kiundani kwenye issues za themes, templates etc.. All in all kazi nzuri. Keep it up..
 
Back
Top Bottom